Ombudsman
JF-Expert Member
- Apr 18, 2012
- 3,565
- 3,729
Kuna mambo mengi sana ya kutisha yaliyotokea kwenye hii awamu ya 5.
Kiongozi kutishiwa na bastola hadharani, kuvamiwa kwa kituo cha tv na mkuu wa mkoa akiwa na silaha za kivita, kuuliwa na kutupwa kwa miili ya watu, kupotea kwa muandishi wa habari na Ben Saa nane, Lissu kumiminiwa zaidi ya risasi 30 kwenye makazi ya viongozi.
Haya yote na mengi yametokea ndani ya miaka miwili ya uongozi wa Rais, sijasema ni yeye amehusika wala sijasema ni serikali yake. Lakini yampasa kutubu kwasababu yametokea chini ya awamu yake, yeye na serikali yake walitakiwa kuwa wa kwanza kukemea na kuchukua hatua kali kuzuia matendo ya kutishia amani yaliyotokea ndani ya hii miaka miwili.
Mkuu wa mkoa kuvamia kituo cha luninga akiwa na silaha za kivita ni jambo la kutisha na kukemewa hadharani na Rais, lakini hakufanya hivyo yeye alimsifia na kusema “chapa kazi” Haya sio maneno ya kusemwa na Rais wa nchi.
Tundu Lissu kumiminiwa risasi katika makazi ya viongozi uko Dodoma, hili ni jambo la kutisha na ni mara ya kwanza kutokea Tanganyika. Lakini mpaka sasa serikali hawajamkamata yeyote aliehusika au kuhisiwa kuwa miongoni mwa wale waliotenda huo unyama.
Hili jambo linaacha maswali mengi sana kwa jamii kuhusu usalama wa wananchi na mali zao.
Kitendo cha kiongozi kutishiwa bastola hadharani nacho ni kitendo cha kukemewa vikali na Rais, lakini hilikua tofauti. Hajawai kusikika akifungua mdomo au kuliongelea hilo jambo, kama kiongozi anatishiwa bastola hadharani, je usalama wa wananchi ukoje?
Kuokotwa kwa miili ya watu waliofungwa kwenyw sandarusi uko Ruvu na Coco beach, ni mara ya kwanza kwa Tanzania kushuhudia uokotwaji wa miili iliyofungwa kwenye sandarusi pembezoni mwa mto Ruvu na bahati ya Hindi.
Mpaka sasa hakuna ripoti inayoonesha hiyo miili ni ya kina nani na kwanini walitupwa hayo maeneo.
Kupotea kwa baadhi ya watu bila ya serikali kujihusisha kuwatafuta, ni mwaka sasa tangu Ben Saanane alivyopotea lakini hakuna ripoti inayoonesha ni kwanini alipotea ni wapi serikali wamefikia katika kuchunguza kupotea kwake.
Sio Ben Saanane tu, kuna mwandishi wa gazeti la Mwananchi nae kapotea kwenye mazingira ya kutatanisha, na mpaka sasa hakuna ripoti inayoonesha maendeleo ya uyafutwaji wake.
Haya yote na mengine mengi kama upinzani kuzuiliwa kufanya siasa, kupigwa kwa wapinzani kwenye chaguzi ndogo, yametokea chini ya uongozi wa Rais aliepo madarakani.
Ni wakati wake sasa wa kutubu na kuanza mwaka 2018 akiwa msafi hili haweze kutumikia wananchi wake kwa usawa, hekima na busara.
Kiongozi kutishiwa na bastola hadharani, kuvamiwa kwa kituo cha tv na mkuu wa mkoa akiwa na silaha za kivita, kuuliwa na kutupwa kwa miili ya watu, kupotea kwa muandishi wa habari na Ben Saa nane, Lissu kumiminiwa zaidi ya risasi 30 kwenye makazi ya viongozi.
Haya yote na mengi yametokea ndani ya miaka miwili ya uongozi wa Rais, sijasema ni yeye amehusika wala sijasema ni serikali yake. Lakini yampasa kutubu kwasababu yametokea chini ya awamu yake, yeye na serikali yake walitakiwa kuwa wa kwanza kukemea na kuchukua hatua kali kuzuia matendo ya kutishia amani yaliyotokea ndani ya hii miaka miwili.
Mkuu wa mkoa kuvamia kituo cha luninga akiwa na silaha za kivita ni jambo la kutisha na kukemewa hadharani na Rais, lakini hakufanya hivyo yeye alimsifia na kusema “chapa kazi” Haya sio maneno ya kusemwa na Rais wa nchi.
Tundu Lissu kumiminiwa risasi katika makazi ya viongozi uko Dodoma, hili ni jambo la kutisha na ni mara ya kwanza kutokea Tanganyika. Lakini mpaka sasa serikali hawajamkamata yeyote aliehusika au kuhisiwa kuwa miongoni mwa wale waliotenda huo unyama.
Hili jambo linaacha maswali mengi sana kwa jamii kuhusu usalama wa wananchi na mali zao.
Kitendo cha kiongozi kutishiwa bastola hadharani nacho ni kitendo cha kukemewa vikali na Rais, lakini hilikua tofauti. Hajawai kusikika akifungua mdomo au kuliongelea hilo jambo, kama kiongozi anatishiwa bastola hadharani, je usalama wa wananchi ukoje?
Kuokotwa kwa miili ya watu waliofungwa kwenyw sandarusi uko Ruvu na Coco beach, ni mara ya kwanza kwa Tanzania kushuhudia uokotwaji wa miili iliyofungwa kwenye sandarusi pembezoni mwa mto Ruvu na bahati ya Hindi.
Mpaka sasa hakuna ripoti inayoonesha hiyo miili ni ya kina nani na kwanini walitupwa hayo maeneo.
Kupotea kwa baadhi ya watu bila ya serikali kujihusisha kuwatafuta, ni mwaka sasa tangu Ben Saanane alivyopotea lakini hakuna ripoti inayoonesha ni kwanini alipotea ni wapi serikali wamefikia katika kuchunguza kupotea kwake.
Sio Ben Saanane tu, kuna mwandishi wa gazeti la Mwananchi nae kapotea kwenye mazingira ya kutatanisha, na mpaka sasa hakuna ripoti inayoonesha maendeleo ya uyafutwaji wake.
Haya yote na mengine mengi kama upinzani kuzuiliwa kufanya siasa, kupigwa kwa wapinzani kwenye chaguzi ndogo, yametokea chini ya uongozi wa Rais aliepo madarakani.
Ni wakati wake sasa wa kutubu na kuanza mwaka 2018 akiwa msafi hili haweze kutumikia wananchi wake kwa usawa, hekima na busara.