Ni wakati muafaka wapinzani kujiunga CCM ili kuleta mabadiliko!

Unknown2

JF-Expert Member
Oct 16, 2016
2,344
4,981
Wakuu, nikiwa kama Mtanzania mwenye uchungu na nchi yangu huwa nasikitika sana jinsi akina Lissu, Mdee, Zitto, Kafulila nk jinsi wanavyodhihakiwa huku wakitetea maslahi ya Watanzania.

Binafsi sioni uwezekano vyama vyao kuja kuitoa madarakani hivyo naona njia bora ya kuisimamia serikali ni kuingia kwenye mfumo!

CCM haishauriki ukiwa mpinzani na hata utoe hoja gani utaonekana huitakii mema labda uwepo msuguano ndani yao km enzi za Sitta, Lowasa na Mwakyembe!

Enyi akina Zitto, Lissu ... chondechonde jiungeni CCM kuliokoa taifa! Ni imani yangu kuwa masuala kama Richmond, EPA, Tegeta Escrow na hata hili la ACACIA hayatajitokeza tena.
 
Wakuu, nikiwa kama Mtanzania mwenye uchungu na nchi yangu huwa nasikitika sana jinsi akina Lissu, Mdee, Zitto, Kafulila nk jinsi wanavyodhihakiwa huku wakitetea maslahi ya Watanzania.

Binafsi sioni uwezekano vyama vyao kuja kuitoa madarakani hivyo naona njia bora ya kuisimamia serikali ni kuingia kwenye mfumo!

CCM haishauriki ukiwa mpinzani na hata utoe hoja gani utaonekana huitakii mema labda uwepo msuguano ndani yao km enzi za Sitta, Lowasa na Mwakyembe!

Enyi akina Zitto, Lissu ... chondechonde jiungeni CCM kuliokoa taifa! Ni imani yangu kuwa masuala kama Richmond, EPA, Tegeta Escrow na hata hili la ACACIA hayatajitokeza tena.
Acha wafu wazike wafu wenzao kuiba waibe wao halafu leo hii waje kulilia kwa watz kua wanaibiwa,jana kasema wapinzani washughulikie ndani na nje ya bunge....huyohuyo anaedaiwa anaibiwa anaomba acacia wakae meza moja wazungumze huoni maajabu,mtu ni jambazi,hana leseni,kakuibia trillion 100 unataka ukae nae uzungumze nae.
Hii ni comedy tupu yani kiswahili cha mtaani ni mbwa kala mbwa
 
Shenzi, mabadiliko miaka 55 ya uhuru hamjaleta, mnataka wapinzani wajiunge ccm halafu iweje! Ww unadhani upinzani ulitokea wapi? Ni wkt muafaka kwa CCM kuwa.

Disolved kwenye upinzani na kupima mambo kwa kina kabla ya kufanya maamuzi na pia muachane na habari za kujamba na midomo ndiyooooooooooooooooooooooo......... huku mkigongagonga meza kwa shibe pupupupupu.

Hakuna nchi kama hii chini ya sayari ya jua.
 
Ni muda muafaka kuiambia ccm kuwa sasa yatosha waachie ngazi wenyewe. Wanahusika kupanga na kuratibuu uporaji huu wa mali za Watanzania.
 
Kwa hiyo unawashauri hawa wazee warejee tena CCM?
19029185_1918561991766579_1478087458628773429_n.jpg
 
Kwa hiyo unawashauri hawa wazee warejee tena CCM?
19029185_1918561991766579_1478087458628773429_n.jpg
Hawa hawakuwa na nia ya Dhati ya kutusaidia na bora walivyotoka kwenye mfumo! Binafsi naona watu kama Lissu, Zitto nk wakipewa nafasi kama walizokuwa nazo akina Lowassa nchi itaepuka majanga mengi!
 
Shenzi, mabadiliko miaka 55 ya uhuru hamjaleta, mnataka wapinzani wajiunge ccm halafu iweje! Ww unadhani upinzani ulitokea wapi? Ni wkt muafaka kwa CCM kuwa.

Disolved kwenye upinzani na kupima mambo kwa kina kabla ya kufanya maamuzi na pia muachane na habari za kujamba na midomo ndiyooooooooooooooooooooooo......... huku mkigongagonga meza kwa shibe pupupupupu.

Hakuna nchi kama hii chini ya sayari ya jua.
Jaribu kutumia lugha nzuri kutoa maoni yako mkuu! Naami una uchungu sana na taifa lako lakini hilo lisikupelekee kutumia lugha isiyo na staha
 
Acha wafu wazike wafu wenzao kuiba waibe wao halafu leo hii waje kulilia kwa watz kua wanaibiwa,jana kasema wapinzani washughulikie ndani na nje ya bunge....huyohuyo anaedaiwa anaibiwa anaomba acacia wakae meza moja wazungumze huoni maajabu,mtu ni jambazi,hana leseni,kakuibia trillion 100 unataka ukae nae uzungumze nae.
Hii ni comedy tupu yani kiswahili cha mtaani ni mbwa kala mbwa
Mind set ya viongozi wengi wa CCM ni kupinga kila liletwalo na wapinzani, naona hata mkuu wetu hii inamsumbua so njia rahisi ni kujiunga nao
 
Sasa unafikili bila wapinzani hayo yote yangejili kweli. Magufuli kawa rais sababu ya nguvu ya upinzani
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom