Ni wakati muafaka sasa Tanzania inahitaji kuwa na Startup Hubs halisia kwa mazingira yetu

miamiatz

JF-Expert Member
Dec 4, 2017
504
927
Tanzania na Africa kwa ujumla bado tunasua sua kwenye kasi ya maendeleo ya kiteknolojia. Vipaji vingi sana kwenye sector ya teknolojia vinakosa muendelezo na njia sahihi za kupita.

Nadhani inatakiwa viongozi wetu waamke sasa na wajue kuwa hata kwenye IT kuna watu wanaoweza kufanya mambo makubwa wakipata majukwaa sahihi.

Serikali zinaonesha kuthamini wafanya biashara wadogo wadogo kwenye upande wa bidhaa ila zinasahau kuwa hata kwenye huduma za ki IT kuna wafanya biashara wadogo wadogo.

Kuanzishwa kwa startup hubs za ki IT itasaidia sana kuleta mageuzi ya matumizi ya IT kutatua baadhi ya changamoto zinazoikabili jamii.

Kama vile ilivyo kwa upande wa viwanda na wawekezaji wakubwa kuwekewa EPZ, IT sector nayo inatakiwa kuwekewa startup hubs ambazo humo ndani kunakuwa na masharti nafuu ya kuanzisha na kuendesha biashara.

Wengi tunafahamu kuwa ili ujiajiri unatakiwa kujisajili. Usajili wa kitanzania ni ule wa kizamani ambapo unatakiwa kukadiria kodi ya mwaka wa kwanza na kulipa robo yake kabla hata hujapewa TIN, Tax Clearence wala Business License

Pia tunafahamu kuwa IT inahitaji kutest concept na feasibility of the concept kabla hujawekeza kwa kasi.

Huwezi mwambia kijana ajisajili, alipe kodi, apange fremu ili akatest concept yake. If it fails hasara yake.

Changamoto hii inatatuliwa kwa kuweka startup hubs kadhaa na kusajili wote wenye vipaji vya kufaa kuwa humo. Wafanye testing ya concepts zao backend na frontend (ikimaanisha kujaribu pia soko).

Startup hubs za aina hii zinafaa kutokuwa na gharama yoyote ya kujiunga. Cha msingi ni kuthibitisha kipaji chako. Iwe kama sehemu ya kuwapitisha watu wajaribu idea zao kama zina uhalisia ama ni ndoto.

Courtesy of miamiatz
 
Tanzania na Africa kwa ujumla bado tunasua sua kwenye kasi ya maendeleo ya kiteknolojia. Vipaji vingi sana kwenye sector ya teknolojia vinakosa muendelezo na njia sahihi za kupita.

Nadhani inatakiwa viongozi wetu waamke sasa na wajue kuwa hata kwenye IT kuna watu wanaoweza kufanya mambo makubwa wakipata majukwaa sahihi...
Ipo pale costech inaitwa buni hub.. umeshaijaribu?
 
Ipo pale costech inaitwa buni hub.. umeshaijaribu?
Labda kuweka records sawa mimi sipo kwenye sector ya IT. Kilichonifanya niandike hii makala ni baada ya kuona msigano wa sheria na hubs ya costech. As if hii kitu imeundwa kisiwani.

Sheria nyingi za kodi, uwekezaji, usajili, etc zime mention EPZ na kutoa vipaumbele ila hazijamention startup hubs.

Ukitaka kuelewa angalia wanaotengeneza online content as startup businesses kama wanaojaribu wazo la kumiliki onlone tv je unadhani kwa kuwepo costech buni hub inawapa exemption ya tcra na bado akarusha habari?

Tunachohitaji sasa ni kuwa na startup hubs za IT za kibiashara na sio buni hubs za watu kubuni vitu ambavyo sokoni sio viable. Hili litawezekana kwa kuzifanya sheria zetu zote zitambue uwepo wa startup hubs kama zinavyotambua uwepo wa epz.

Exemptions za epz zimetajwa katika sheria za kodi, sheria za usajili, sheria za uwekezaji, etc je exemption za hii buni hub zimetajwa wapi?

Na je nani anamiliki biashara yoyote ya IT ambae yupo buni hub na hiyo biashara ipo sokoni na imeanza angalau kufanya vizuri? Kuna watu wanaunda softwares underground ila hawana pa kutokea. Akiwaza usajili kichwa kinauma.

Ni hivi ilitakiwa mfano sheria za brela ziseme yeyote atakaetaka kusajili kampuni na akawa ni miongoni mwa waliosajiliwa na costech buni hub basi hatolipia ada za usajili.

Same iwe kwa sheria za kodi, etc. Hii itasaidia vijana kumiliki biashara zao kwa vile wanavyovianzisha na wawekewe limit baada ya muda flani unatakiwa kutoka ukapange mtaani na ulipe kodi za serekali.

This was my idea and opinion.

Courtesy of miamiatz
 
Labda kuweka records sawa mimi sipo kwenye sector ya IT. Kilichonifanya niandike hii makala ni baada ya kuona msigano wa sheria na hubs ya costech. As if hii kitu imeundwa kisiwani.

Sheria nyingi za kodi, uwekezaji, usajili, etc zime mention EPZ na kutoa vipaumbele ila hazijamention startup hubs.

Ukitaka kuelewa angalia wanaotengeneza online content as startup businesses kama wanaojaribu wazo la kumiliki onlone tv je unadhani kwa kuwepo costech buni hub inawapa exemption ya tcra na bado akarusha habari?

Tunachohitaji sasa ni kuwa na startup hubs za IT za kibiashara na sio buni hubs za watu kubuni vitu ambavyo sokoni sio viable. Hili litawezekana kwa kuzifanya sheria zetu zote zitambue uwepo wa startup hubs kama zinavyotambua uwepo wa epz.

Exemptions za epz zimetajwa katika sheria za kodi, sheria za usajili, sheria za uwekezaji, etc je exemption za hii buni hub zimetajwa wapi?

Na je nani anamiliki biashara yoyote ya IT ambae yupo buni hub na hiyo biashara ipo sokoni na imeanza angalau kufanya vizuri? Kuna watu wanaunda softwares underground ila hawana pa kutokea. Akiwaza usajili kichwa kinauma.

Ni hivi ilitakiwa mfano sheria za brela ziseme yeyote atakaetaka kusajili kampuni na akawa ni miongoni mwa waliosajiliwa na costech buni hub basi hatolipia ada za usajili.

Same iwe kwa sheria za kodi, etc. Hii itasaidia vijana kumiliki biashara zao kwa vile wanavyovianzisha na wawekewe limit baada ya muda flani unatakiwa kutoka ukapange mtaani na ulipe kodi za serekali.

This was my idea and opinion.

Courtesy of miamiatz
Nakubaliana na wewe ndugu yangu.. nchi hii haina dira wala mwelekeo.. wanawaza uchaguzi na kuua wapinzani.. TZ itaendelea kuwa maskini wa mwisho.. kwa kushindwa kutegua mtego mdogo sana.. mtego wa kodi. Biashara haziwezi kuanzishwa na zilizopo kukua kwa sababu wale kuku wa wizara ya fedha hawawazi zaidi ya kukomoa na kukomesha. Nchi inahujumiwa. Hata venture capitals huku haziwezi kuja kwa sababu kabla biashara haijaanza tozo sijui kodi zishaanza.. nani atakubali ujinga huu? Watu wa IT bora kwenda US au hata SA.. terms zao ni friendly kuliko hapa wanaobambikiza watu makodi na matozo
 
Back
Top Bottom