Ni wakati gani sahihi kwa kijana kutoka kwa wazazi wake? Ukweli mchungu

Nyenyere

JF-Expert Member
Sep 9, 2010
14,769
10,650
Ni kawaida katika zama hizi kuona kijana amejitegemea na kuwa na ghetto lake. Hali hii imedumu hata kufikia mahali wazazi kuwataka vijana wao hasa wa kiume kuondoka majumbani na kujitegemea. Jamii forums haibaki salama katika hili, mada nyingi zimeanzishwa humu kuwazodoa vijana wanaopindukia umri fulani kuendela kibaki majumbani mwa wazazi wao. Ukweli ukoje?

Hapo zamani vijana walilelewa kifamilia, wake kwa waume. Lengo lilikuwa kuwafunza stadi za maisha kulingana na kazi wafanyazo wazazi. Kijana angefundishwa kazi za baba mfano uvuvi, useremala, kilimo, ufugaji, biashara n.k. Baba angehakikisha anakuwa bega kwa bega na mwanae katika mambo yake yote. Ilitarajiwa kuwa mwishowe kijana huyu angekuwa na ujuzi wa kutekeleza hayo na zaidi ya hapo, kwani huo ulikuwa ni msingi na unajengwa kuwa tabia ya kijana huyu. Kwa mfano kile wanachofanya jamii ya wahindi leo sio bahati mbaya. Ni utaratibu ambao wamekuzwa nao, na kitu ambacho tumeshindwa kung'amua na kubaki tunawashangaa, wakati ukweli ni kuwa huu uataratibu sio mgeni. Naam, ndio huo huo utaratibu tulioukataa sisi na kukimbilia kuiga akina Puff dady. Kijana angeweza kufanya majukumu ya baba peke yake (kasoro ngono) kuhesabiwa kuwa anatosha kuoa na kujitegemea. Alipimwa uwezo wake wa kufanya maamuzi kutatua changamoto mbalimbali pasipo kumtegemea baba. Mfano wasukuma wana kitu kinaitwa nsumba ntale.

Mabinti nao walilelewa katika mazingira ya kujifunza majukumu ya mama kwenye familia. Hii ilianzia nyumbani mpaka kwenye kazi za kiuchumi. Mfano kama familia ni ya wakulima, familia nzima ingeenda shamba alfajiri, ikifika muda fulani, mara nyingi saa tano, mama na binti zake wangeondoka shamba kwenda kusenya kuni na kuchota maji, huku baba na vijana wakiendelea kulima. Muda wa chakula baba angerejea na vijana wake nyumbani ama chakula kingeletwa shamba. Haya ni mafunzo ya mgawanyo wa majukumu katika familia. Binti angetarajiwa kumudu kutekeleza majukumu ya malezi ya familia kiasi kwamba hata mama asipokuwapo mambo ya nyumbani yanakwenda vema kabisa. Binti wa namna hii alisemwa kuwa tayari kwa majukumu ya ndoa.

Wakati hapo zamani ilikuwa fahari kwa kijana kujitambulisha kwa uhodari wake katika kazi za kiuchumi, leo hii ni fahari kujilinganisha na akina Ja rule. Kama taifa na kama jamii tumepotea. Ungekuta kijana wa miaka 10 anamiliki ekari 5 za mazao ya biashara chini ya uangalizi wa wazazi wake. Kina Mo Dewji hawakutokea tu hewani, ni mfumo uliowaleta hapo walipo sasa. Kina Manji wametengenezwa na wazazi wao. Hebu jiulize wewe mzazi wa zama hizi anamtengeneza mtoto kuwa nani? Mfumo huu ulileta jamii toshelevu, sio kwamba ilikuwa tajiri hapana, ila mahitaji ya msingi yalipatikana muda wote. Hata waliopata utajiri walijiongeza kupitia mfumo huu.

Elimu ilipaswa kumjenga kijana awe na wigo mpana wa kufikiri namna bora ya kuendesha shughuli za kila siku. Haikupaswa kuwa mbadala wa kile kijana anachokipata kutoka kwa wazazi wake. Badala yake elimu imekuja kuandaa vijana wa kutumika maofisini na viwandani. Kama huamini tazama ni wahitimu wangapi wa vyuo wanashinda mabarabarani na vyeti vyao wakitafuta ajira. Ama tafuta humu JF ni mada ngapi zinauliza kampuni inayolipa mshahara mzuri. Elimu imetukomboa kutoka Ujima na kutuingiza kwenye ujinga. Hatufikiri tena ila kila kitu tukifanyacho tunafuata kanuni zilizoandikwa na wasomi waliotangulia. Tumegeuzwa mabingwa wa kukariri na kutoa reference za maisha ya ulaya. Hatutofautiani sana na maroboti. Elimu yetu imetuandaa kuwa watumwa, ingawaje siku hizi kuna neno tamu kidogo, waajiriwa. Wapo ambo elimu imawawezesha kujiajiri, mfano madaktari, waalimu nk. Hao wametumia elimu yao kukamata fursa katika jamii.

Tukirejea kwenye mada, kijana alipofikia umri wa kuoa (yaani uwezo wa kujitegemea), alitakiwa ajiandae kuanza maisha mapya. Wazazi walimsimamia katika hili n kuhakikisha kuwa anajiweka tayari kupokea majukumu. Ni wazazi ndio waliokuwa na uwezo wa kuamua kwamba kijana amefikia umri sahihi kwke kuoa. Ama wangemshauri aoe, ama angeomba mwenyewe ruksa ya kuanzisha familia yake. Mpaka hapo bado alikuwa mikononi mwa wazazi. Ndipo sasa taratibu zingefanyika za kuposa, ikiwa ni pamoja na wazazi kumuuliza kama jicho lake limepata kuona mahali ambapo kuna binti wa kumfaa. Kama hajawahi wazazi wangempa machagua kadhaa kadri walivyoona tabia na mwenendo wake, na kuoanisha na tabia na mwenendo wa familia ya binti yule, ili waendane.

Idhini ya kijana kuondoka kwenye familia yake na kujitegemea ilikuwa ni kuoa. Kijana akipata mke tayari hapawswi tena kukaa nyumbani kwa wazazi wake, isipokuwa kwa baadhi ya jamii zenye mfumo wa kuishi pamoja kama boma. Huo ndio ulikuwa wakati sahihi kwa kijana kuoa, tofauti na ilivyo sasa. Kwa misingi hii ndoa hazikuwa tendo lla kubahatisha kama ilivyo leo. Ndoa ni mfumo wa kikanuni ambao unawawezesha mke na mume kudumu kwa muda mrefu huku kukiwa na asilimia ndogo ya kuachana. Mfumo huu tumeukataa na kujidai kuiga mfumo wa kimagharibi, kitu ambacho ni machukizo makuu.

Kwa wakristo wengi hawajui kwamba hata Mungu hajamruhusu kijana kujitenga na wazazi wake isipokuwa tu awe ameoa. Hata binti ni ndoa tu itakayomtenga na wazazi wake. Kumekuwa na mafundisho potofu katika zama hizi kwamba kijana wa kiume mwenye miaka 18 ajitegemee na ni aibu kuishi kwa wazazi. Ni mafundisho potofu na yamekuwa chanzo ku kuharibu vijana wengi.

Itaendelea......
 
Mi nadhani kijana anapofikia umri wa kuweza kujimudu kimaisha basi anafaa aondoke kwa wazazi wake
 
Mimi naona kijana kaa kwenu ukiona sasa hivi naweza kuhama home hama kweny nenda kaanze maisha mapya sasa unakuja mwingine anafosi tu ili aonekane hakai kwao kodi yenyewe anaomba wanandugu wamchangie, mama, kaka etc yani mpaka unajiuliza sasa umehama nyumbani umehama kwasababu gani
 
Mimi naona kijana kaa kwenu ukiona sasa hivi naweza kuhama home hama kweny nenda kaanze maisha mapya sasa unakuja mwingine anafosi tu ili aonekane hakai kwao kodi yenyewe anaomba wanandugu wamchangie, mama, kaka etc yani mpaka unajiuliza sasa umehama nyumbani umehama kwasababu gani
Labda anaona kwa namna yoyote atoke nyumbani.
 
Ni ajabu leo hii hata viongozi wa dini wanawataka vijana wajitegemee pasipo kuwa na wake. Eti wajifunze maisha wakomae ili waweze kuoa na kutunza familia. Mtazamo huu ni hasi na ni tatizo lwenye ndoa. Kijana asiyefunzwa kujitegemea na wazazi wake atafunzwaje na dunia? Huko kuna kila aina ya vijana waliokata tamaa, hawana future yoyote. Hawa ndio wanatarajiwa wamjenge kijana awe mume bora siku za mbeleni. Matokeo yake ni kujiingiza kwenye wimbi la umalaya, uvutaji bangi, madawa ya kulevya, ujambazi, n.k. Mambo haya si ya kuzaliwa, yanategemea aina ya marafiki na malezi. Ndivyo ilivyo kwa ndoa, inategemea una malezi ya aina gani na marafiki wa aina gani.

Binti pia anatarajiwa akae kwao mpaka aposwe. Ni aibu kuu kuona binti ametoka kwao akajitegemee kwmba eti umri unakwenda. Mwanamke hana uwezo wa kuishi peke yake, kwani kwake ni majaribu makuu. Mwanamke asipoolewa atakaa hivyohivyo kwa wazazi wake na jambo hili ni aibu kwa wazazi pia. Rafiki wa karibu wa binti ni mama mzazi. Ndioo tukapata msemo asiyefunzwa na mamaye hufunzwa na ulimwengu. Kujitegemea ni kukataa mafunzo ya mama na kutafuta kufunzwa na ulimwengu.

Kwa wakristo neno la Mungu linasema hivi:

Mwanzo 2

²⁴ Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja.


Ukisoma vema utagundua kuwa, mwanamume atawaacha wazazi wake ili kuanzisha familia mpya akiwa na mke. Hawaachi wazazi ili kwenda kujiandaa kuanzisha familia. Leo hii imekuwa kinyume, mwanamume anaondoka kwa wazazi kwa sababu jamii haitamwelewa. Anakwenda kutumikia matakwa ya dunia huko na si matarajio ya wazazi.

Ndio maana siku hizi wazazi walio wengi hawakubali kuwaamini vijana wao kwenye kuendesha miradi yao. Unakuta kijana kaondoka kujitegemea, anaishi huko akiendana na maisha ya vijana wengine, akipigika ndipo anarudi kwa baba kutaka kuendesha miradi. Hakuna mzazi atakuruhusu uue biashara zake. Tena wengine pale wazazi wakifa na kuwaachia mali nyingi hushindwa kuitunza na kuishia kuitapanya. Hawana elimu sahihi.
 
Muda sahihi ni pale kijana atakapokuwa yupo tayari kujisimamia kiakili, akiwa na sababu za muhimu za kuondoka nyumbani.
Mimi naona kijana kaa kwenu ukiona sasa hivi naweza kuhama home hama kweny nenda kaanze maisha mapya sasa unakuja mwingine anafosi tu ili aonekane hakai kwao kodi yenyewe anaomba wanandugu wamchangie, mama, kaka etc yani mpaka unajiuliza sasa umehama nyumbani umehama kwasababu gani
Mi nadhani kijana anapofikia umri wa kuweza kujimudu kimaisha basi anafaa aondoke kwa wazazi wake
Kwa dunia ya leo ilivyo, naweza kukubaliana nanyi kwamba kijana ataondoka kwao pale anapoweza kujisimamia mwenyewe kupambana na maisha. Tatizo tulilonalo kwa sasa ni kuwa vijana wanaondoka makwao na kujitegemea halafu ndugu zao ndio wanagharimia maisha yao. Inakuwa haina maana ya kuondoka nyumbani tena
 
Usiwapotoshe vijana,kwa namna ulivyoongelea umeongelea zaid kwa mazingira ya kijijini,vp kuhusu mijin baba ana unga unga hana kazi maalumu ,mama nae anaunga unga sasa kwann kijana wa kiume usijiongeze utoke hom uangalie ustaarabu mwingne kuliko kuongeza mzigo tu nyumbani
 
Usiwapotoshe vijana,kwa namna ulivyoongelea umeongelea zaid kwa mazingira ya kijijini,vp kuhusu mijin baba ana unga unga hana kazi maalumu ,mama nae anaunga unga sasa kwann kijana wa kiume usijiongeze utoke hom uangalie ustaarabu mwingne kuliko kuongeza mzigo tu nyumbani
Sio sawa, wewe ndio umepotoka. Mimi naongelea familia zenye mfumo imara, hiyo kuungaunga ndio matokeo ya kutokuwa na mfumo sahihi. Kama kweli kijana anatoka home aangalie ustaarabu mwingine, basi huo ustaarabu atauangalia hata akiwa home.

Wako vijana wanatoka kwenda mikoani mfano Kiteto kufanya kilimo. Ni jambo zuri sana ila bado wanapaswa kuwa chini ya mamlaka ya wazazi wao, na hivyo watajengeka katika maadili. Ni pale tu watakapoanzisha familia ndipo watakuwa na mamlaka kamili. Sasa ukidharau uangalizi wa wazazi mara nyingi utarudi ukiwa mambo yamekuharibikia, unahitaji huruma.
 
Ukiona unaanza kusimangwa, kila unachokifanya wanakiona kibaya..unapewa majina ya hovyo.. My friend akufukuzae hakwambii toka. Hapo fanya utaratibu usepe haraka iwezekanavyo
Na wazazi wema hawawezi kukusimanga, ila watakukalisha kitako ili kutaka kujua tatizo ni nini. Mambo haya hutokea mara nyingi kwa familia ambazo baba ni mfanyakazi wa ofisini, halafu kijana unashinda home huna mbele wala nyuma kwa vile tu uliaminishwa bila ajira hakuna maisha. Kinachofuata ni wazazi kukuona mzigo kwao badala ya kukuoa mzigo wao ili waone ni namna gani wakusaidie. Mzazi mwema humtengenezea mtoto wake mazingira, huo ni ukweli.
 
Hii mada ni nzuri sana....Ni kweli vijana wanapaswa kuwa chini ya uangalizi wa familia till atakapokuwa tayari kuanzisha familia yake (kuoa/kuolewa), uko sahihi kabisa mkuu, ila fikiria kijana amemaliza masomo yake, na kapata kazi mji wa mbali na makazi yao, hii unaichukuliaje. Sababu kule anaenda kuanza maisha mapya , ya kwake. Tunachopaswa wazazi ni kuhakikisha vijana wetu wanakuwa tayari kwa maisha yajayo, iwe kuendesha miradi ya familia, au kwenda mbali kufanya kazi, ila awe na misingi iliyojengwa na wazazi.
 
Hii mada ni nzuri sana....Ni kweli vijana wanapaswa kuwa chini ya uangalizi wa familia till atakapokuwa tayari kuanzisha familia yake (kuoa/kuolewa), uko sahihi kabisa mkuu, ila fikiria kijana amemaliza masomo yake, na kapata kazi mji wa mbali na makazi yao, hii unaichukuliaje. Sababu kule anaenda kuanza maisha mapya , ya kwake. Tunachopaswa wazazi ni kuhakikisha vijana wetu wanakuwa tayari kwa maisha yajayo, iwe kuendesha miradi ya familia, au kwenda mbali kufanya kazi, ila awe na misingi iliyojengwa na wazazi.
Ume ongea point kubwa,Lakin kinacho fanya wazaz watuchoke nyumban licha ya kumaliza chuo ni vile huwa hatutaki kutafuta kaz na kukalia kuchange tudemu twa mtaani,Kama unajishugulisha siyo rahis wazaz kukuchoka.
 
Ume ongea point kubwa,Lakin kinacho fanya wazaz watuchoke nyumban licha ya kumaliza chuo ni vile huwa hatutaki kutafuta kaz na kukalia kuchange tudemu twa mtaani,Kama unajishugulisha siyo rahis wazaz kukuchoka.
That's why nimesema...ni jukumu letu wazazi kuwaanda vijana wetu.....kama hujamuandaa unategemea nini....atazingua tuu..
 
Jf kwasasa nayenyewe ilishakuwa kigeugeu aiseee. Kuna member humu walikuwa wanatuzodoa sana tuliokuwa tunaishi kwazazi, tukawasikiliza tukatoka home nasasa nimepanga room. Leo hii member mwingine anakuja naswaga nyingine sasa nimsikilize nani? Nipo room ila hakuna nachofanya zaidi yazinaa kwasana maana geto lipo2. Natoka nimepanga tayari nimeshapata mtoto na mwanamke mwingine anamimba nanyumbani hawajui nn kinaendelea huku uraiani.
 
Back
Top Bottom