Hivi nini kigezo cha mji kuwa na hadhi ya Jiji?

Freddy81

Member
Feb 3, 2009
99
3
Habari wana JF,

Ninachotaka wandugu ni kuwekana sawa. hivi ni vigezo gani vinavyotumika hapa Tanzania kuifanya baadhi ya miji kuwa majiji?

Vigezo ninavyovijua mimi ni:-
1.Idadi ya watu
2.Unachangiaji katika pato la taifa
3.Miundo mbinu ya kutosha,
4.Upatikanaji wa huduma za jamii..Afya,maji safi n.k
5.Maendeleo ya wananchi wake

Sasa najuliza,kwa mfano wa hili la miundombinu na Huduma za jamii ni kweli huwa linazingatiwa uu ni siasa tu? Kweli kuna baadhi ya Miji kam Mwanza inakua kwa kasi, Lakini Je Vipi kuhusu Jiji la Tanga, Jiji la Mbeya na Arusha kama sikosei nalo ni jiji.

Mnazungumziaje na jiji letu Kongwe kabisa la DSM je lina Miundombinu ya Kutosha na mizuri? Nadhani ndo jiji linaloongoza Duniani kwa kujengwa ovyo..

Je ni vigezo vyote hutumika au kikiwepo kimoja kati ya hivyo ndo imewin???? Au ni kamchezo ka siasa tu. Embu tuwekane wazi kuhusu hili wandugu.

Ni Hayo tu
 
Mada yako haina mvuto! Ila kuna vimiji vingine Bongo vimepewa hadhi ya jiji kwa sababu za kisiasa! Mfano Mbeya, yaani mji watu wanalala saa 10 jioni, hamna hata klabu ya usiku ya maana eti nalo ni jiji! Phew!!!
 
Mada yako haina mvuto! Ila kuna vimiji vingine Bongo vimepewa hadhi ya jiji kwa sababu za kisiasa! Mfano Mbeya, yaani mji watu wanalala saa 10 jioni, hamna hata klabu ya usiku ya maana eti nalo ni jiji! Phew!!!

Hivi Arusha na Mbeya wapi pana staili kuwa JIJI?
 
Je mnafahamu kuwa na Moshi iko mbioni kuwa jiji? Uongozi wa Manispaa katika malengo yake ya miaka 10 ijayo ni kuwa Moshi ipate hadhi ya jiji, ukifika ofisi za manispaa pale Moshi kuna bango kubwa limeandikwa malengo yao. Na kwa kweli, kwa waliofika Moshi zamani, wakienda sasa hivi kuna tofauti kubwa
1. Mji wa Moshi toka zamani ulipangika vizuri, una mitaa ya kueleweka, alternative routes kibao
2. Mji ni msafi
3. Huduma za jamii za kueleweka: maji (ni nadra sana usikie eti eneo fulani Moshi halina huduma ya maji), barabara sasa hivi kwa kiasi kikubwa ni lami safi, ile tabia ya mji kwenda kulala baada ya saa 11 haipo tena, sehemu za starehe kwa wingi (kinachosubiriwa sasa ni jumba la sinema ambalo nimesikia linafunguliwa siku za karibuni) nk
4. Vyuo kwa wingi: KCMC, MUCCoBS, Mwenge, Mweka, Sebastian Moshi etc... hivi vimechangia sana kuongeza idadi ya wakaazi na kuuchangamsha mji, pia magari (not necessarily an indicator of progress/ development) yameongezeka na sasa hivi si tu zile 504 na pickup zilizozoeleka zamani

Kilichobaki sasa ni viwanda vingi vilivyokuwepo zamani kufufuliwa baada ya kufa katika ka-mchezo fulani ka kuwaadhibu wenyeji baada ya kusapoti upinzani!!
 
Je mnafahamu kuwa na Moshi iko mbioni kuwa jiji? Uongozi wa Manispaa katika malengo yake ya miaka 10 ijayo ni kuwa Moshi ipate hadhi ya jiji, ukifika ofisi za manispaa pale Moshi kuna bango kubwa limeandikwa malengo yao. Na kwa kweli, kwa waliofika Moshi zamani, wakienda sasa hivi kuna tofauti kubwa
1. Mji wa Moshi toka zamani ulipangika vizuri, una mitaa ya kueleweka, alternative routes kibao
2. Mji ni msafi
3. Huduma za jamii za kueleweka: maji (ni nadra sana usikie eti eneo fulani Moshi halina huduma ya maji), barabara sasa hivi kwa kiasi kikubwa ni lami safi, ile tabia ya mji kwenda kulala baada ya saa 11 haipo tena, sehemu za starehe kwa wingi (kinachosubiriwa sasa ni jumba la sinema ambalo nimesikia linafunguliwa siku za karibuni) nk
4. Vyuo kwa wingi: KCMC, MUCCoBS, Mwenge, Mweka, Sebastian Moshi etc... hivi vimechangia sana kuongeza idadi ya wakaazi na kuuchangamsha mji, pia magari (not necessarily an indicator of progress/ development) yameongezeka na sasa hivi si tu zile 504 na pickup zilizozoeleka zamani

Kilichobaki sasa ni viwanda vingi vilivyokuwepo zamani kufufuliwa baada ya kufa katika ka-mchezo fulani ka kuwaadhibu wenyeji baada ya kusapoti upinzani!!

Injinia ni MOSHI kuwa jiji au KILIMANJARO kuwa jiji???
 
Injinia ni MOSHI kuwa jiji au KILIMANJARO kuwa jiji???


Ha ha!! Ni Moshi bwana. Mi sijui kuhusu Kilimanjaro nje ya Moshi. Kwa nini umeuliza hivyo? Nilidhani nilichoandika ni kuhusu mji wenyewe wa Moshi
 
Kwa jumla miji inayo stahili kuwa na sifa ya jiji Tanzania ni DAR, Mwanza na Arusha tu.
 
Unaweza kwenda kuuliza TAMISEMI watakupatia sababu. Lakini lazima ujue kuwa hakuna vigezo vya kimataifa juu ya hadhi ya miji. Hivyo usilinganishe na nchi za wenzetu. Kwa Tanzania kuna sababu za kisisa pia katika kuipandisha hadhi miji.

Kwa mfano Mwaka 2005 lilipitishwa azimio kwamba miji yote ambayo ni makao makuu ya mikoa iwe kwenye ngazi angalau Manispaa. Hivyo Mikindani-Mtwara, Lindi, Ujiji-Kigoma, Songea, Rukwa nk ukapandishwa hadhi toka miji kuwa manispaa. Hivyo kigezo kikubwa ilikuwa ni makao makuu ya mkoa na si vinginevyo.

Mbeya na Mwanza pamoja na vigezo vingine, zimepandishwa toka manispaa kuwa jiji kutokana na kuwa makao makuu ya kanda ya kusini na kasikazini respectively (siyo rasmi). Ninamaanisha kwamba ktk Tanzania kuna kanda licha ya kwamba hazipo rasmi. Miradi au shughuli za Serikali zinazosimamiwa kikanda. Nadhani na Arusha inaingia hapa ila sijui kuhusu Tanga.
 
Kwa jumla miji inayo stahili kuwa na sifa ya jiji Tanzania ni DAR, Mwanza na Arusha tu.


Hapo natofautiana na wewe Magezi. Arusha!! Ile vurugu nayo ni jiji? Ni kwamba tu ina vitu vichache vinavyotakiwa katika jiji lakini the main thing kwa mfano lay-out ya mji (it was originally planned as a small hunting town), huduma ya maji safi na maji taka (you might argue kwamba mbona Dar ni jiji).

Usidanganyike na majengo machache marefu, wingi wa watu (tena wenye hela), uzuri wa magari, viwanja vya starehe nk. Jiulize, je UNICTR wakiondoka Arusha leo, mzunguko wa pesa utakuwa sustained?
 
Ha ha!! Ni Moshi bwana. Mi sijui kuhusu Kilimanjaro nje ya Moshi. Kwa nini umeuliza hivyo? Nilidhani nilichoandika ni kuhusu mji wenyewe wa Moshi

Namaana kwamba , Badala ya kuita Jiji la Dar basi wangeita Jiji la K'ndoni au Ilala Injinia
 
Hapo natofautiana na wewe Magezi. Arusha!! Ile vurugu nayo ni jiji? Ni kwamba tu ina vitu vichache vinavyotakiwa katika jiji lakini the main thing kwa mfano lay-out ya mji (it was originally planned as a small hunting town), huduma ya maji safi na maji taka (you might argue kwamba mbona Dar ni jiji).

Usidanganyike na majengo machache marefu, wingi wa watu (tena wenye hela), uzuri wa magari, viwanja vya starehe nk. Jiulize, je UNICTR wakiondoka Arusha leo, mzunguko wa pesa utakuwa sustained?

Arusha kuwa jiji bila UNICTR inawezekana mkuu, UN-ICTR ni kigezo cha sehemu tu ya mzunguko wa mapesa A-city Mkuu
 
Oh, ok, nimekupata Kimbweka. Nadhani waliokosea ni walioupa mkoa jina la Dar-es-Salaam kwani kilichoanza ni mji/ bandari ya Dar-es-Salaam, hivyo jiji linastahili kuendelea kuitwa kwa jina hilo ila tu mkoa ndio ungetafutiwa jina lingine kama vile "Mkoa wa Ngereko" au kitu kama hicho
 
Arusha kuwa jiji bila UNICTR inawezekana mkuu, UN-ICTR ni kigezo cha sehemu tu ya mzunguko wa mapesa A-city Mkuu


Usinipate vibaya. Mimi mwenyewe Arusha ndio kwetu. Ila kwa kweli hadhi ya jiji haistahili. This is my personal opinion. The TOWN is so disorganized, dirty, cramped...to mention a few negatives. Sikatai kwamba kuna mambo mazuri pale, ila kwa jinsi ulivyo sasa hivi, hapana. Labda wafanye mpango wa kuupanua (jambo ambalo niliwahi kusikia lilipangwa kufanyika ila wenyeji (Waarusha) waligoma kuachia ardhi zao hasa katika maeneo kama Kijenge, Moshono, Njiro chini, Sekei etc) na kuongeza barabara + alternative routes.

Kwa kifupi kwa mawazo yangu Arusha ni jiji only in terms of the lifestyle of it's residents!!
 
huwa wanatumia vigezo gani maana nimefika mbeya mji hauna hata chembe moja ya kuwa jiji unazidiwa hata na wilaya ya kahama jamani
 
kwani kuna jiji tanzania basi kama ndo ivo ukilinganisha na majiji kama new york,tokyo n.k
 
huwa wanatumia vigezo gani maana nimefika mbeya mji hauna hata chembe moja ya kuwa jiji unazidiwa hata na wilaya ya kahama jamani
acha madhereu weye, MBEYA haiwezi linganishwa na kahama. Mbeya ina uchumi mkubwa kuliko kahama==kama umekosa mji wa kulinganisha na Mbeya, sema. Unalinganisha na Kahama ambako kuna njaa toka asubuhi mpaka jioni... hili ni moja tu ninayo mengi sana tatizo muda wa kukukuambia
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom