Uchaguzi 2020 Ni vipi unawashawishi wakazi wa Dar waliobomolewa nyumba kwa upanuzi wa barabara wakati kwa wakazi wa Mwanza ulisema wasibomolewe walikupigia kura?

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,129
18,743
Kuna wakati najiuliza kati ya wanasiasa na wapiga kura ni nani ana kumbukumbu fupi zaidi. Kwa mfano, wakati fulani kulikuwa na kampeni ya kubomoa nyumba bila kulipa fidia hapa Dar, na wananchi wote wakalaani sana kitendo hicho.

Hivi katika wale waliolaani kitendo hicho ndio walewale tunawashudia wakiwa mbele kwenye kampeni za CCM, au wale kule Bukoba waliopata maafa wakaambiwa watajiju wenyenyew, leo wako wapi katika suala la CCM Vs Chadema? Au Watanzania kwa ujumla, waliposikia kauli kwamba wakazi wa Mwanza hawatabomolewa nyumba kama wakazi wa Dar kwa kuwa walimpigia kura mgombea wa CCM, hii inawapa msimamo gani katika kampeni za CCM Vs Chadema?

Au tuliposhuhudia wimbi la utekeji watu na waandishi wa habari wanaoikosoa serikali na viongozi, na hata mauaji yao, na kila mtu kulaani kwamba serikali haichukui hatua huenda hata inahusika, leo watu waliolaani vitendo hivi wako wapi katika suala la kampeni hizi?

Au wafanyakazi kwa ujumla, walipolaani sana suala la kikokoto cha mafao na kikaahirishwa hadi baadae (sijui lini), au pale wanaponyimwa nyongeeza za mishahara ili fedha ya ndani itumike kwenye miradiwanakuwa wapi katika suala nzima la kampeni za CCM Vs Chadema?

Nina mifano mingi lakini hii inatosha. Je, ni nani anakuwa na kumbukumbu fupi katika masuala kama haya, ni wapiga kura au wanasiasa wanaorudi kutuomba kura?
 
Wakazi waliobomolewa wenyewe walikiri kuwa walinunua viwanja/nyumba kutoka kwa wamiliki wa awali ambao walikuwa tayari walishalipwa fidia hivyo waliingizwa mkenge. Wapo pia ambao walikula fidia na kugoma kuondoka ila pia watu hawabomolewi hivi hivi zipo sheria za hifadhi za barabara.

Kwa hapa Mwanza njoo hapa Buswelu uone watu walivyobomolewa nyumba (nimeitaja Buswelu kwasababu ndipo upomoaji wa hivi karibuni maana nyie mnasahau haraka)
 
Mzee kafeli mipango mingi sn, chuki zake na dharau zimemponza sn
Nimemaliza kufanya booking na air tanzania, jioni nipo Dar, fahari sana kusafiri na ndege ya shirika la ndege la nchi yako! Mkuu karibu soko la dhahabu uone vijana wadogo wanavyokamata fedha na hapo ndio utajua kuishi kwa kutegemea madili na wizi kuna life span fupi sna!
 
Wakazi waliobomolewa wenyewe walikili kuwa walinunua viwanja/nyumba kutoka kwa wamiliki wa awali ambao walikuwa tayari walishalipwa fidia hivyo waliingizwa mkenge.
Wee! Wee! Wee! Usiwasemee. Hujui ni maumivu kiasi gani wamepitia kwa ukatili aliyoyafanya huyu

Sasa kama lengo lake ilikuwa kuwabomolea waliokiuka sheria kwann Mwanza sheria haikufuatwa.

Tukutane 28/10/2020 tumfundishe adabu huyu dikteta uchwara
 
Wee! Wee! Wee! Usiwasemee. Hujui ni maumivu kiasi gani wamepitia kwa ukatili aliyoyafanya huyu muuaji.

Sasa kama lengo lake ilikuwa kuwabomolea waliokiuka sheria kwann Mwanza sheria haikufuatwa.

Tukutane 28/10/2020 tumfundishe adabu huyu dikteta uchwara
Eneo gani na lini Mwanza sheria haikufuatwa. Lissu akipata hata wabunge 4 njoo PM nikupe 100,000 ya kununulia bando!
 
Wee! Wee! Wee! Usiwasemee. Hujui ni maumivu kiasi gani wamepitia kwa ukatili aliyoyafanya huyu muuaji.

Sasa kama lengo lake ilikuwa kuwabomolea waliokiuka sheria kwann Mwanza sheria haikufuatwa.

Tukutane 28/10/2020 tumfundishe adabu huyu dikteta uchwara
Soma jina ujue anatokea wapi mkuu ndiyo maana anaongea ujinga
 
Wakazi waliobomolewa wenyewe walikiri kuwa walinunua viwanja/nyumba kutoka kwa wamiliki wa awali ambao walikuwa tayari walishalipwa fidia hivyo waliingizwa mkenge. Wapo pia ambao walikula fidia na kugoma kuondoka ila pia watu hawabomolewi hivi hivi zipo sheria za hifadhi za barabara.

Kwa hapa Mwanza njoo hapa Buswelu uone watu walivyobomolewa nyumba (nimeitaja Buswelu kwasababu ndipo upomoaji wa hivi karibuni maana nyie mnasahau haraka)
Sawa Mkuu, mie sijaja Mwanza, lakini nilichoongea hapa ni kauli kwamba watu wa Mwanza wasibmolewe hawa walinipigia kura. Sasa niambie kama kauli hiyo haikutolewa wakati wakazi wa Dar wakigumia kwa uchungu wa kubomolewa, au kama wahanga wa tetemeko Kagera hawakuambiwa serikali haikuleta tetemeko, na mengine tujadili baadaye
 
Nimemaliza kufanya booking na air tanzania, jioni nipo Dar, fahari sana kusafiri na ndege ya shirika la ndege la nchi yako! Mkuu karibu soko la dhahabu uone vijana wadogo wanavyokamata fedha na hapo ndio utajua kuishi kwa kutegemea madili na wizi kuna life span fupi sna!u
Unajua hata yule mnunuzi wa madege kinachomsumbua ni ushamba na ulimbukeni unaofanana na wako.

Ndege ni usafiri wa kawaida tu kama ulivyo wa mabasi na daladala.
 
Eneo gani na lini Mwanza sheria haikufuatwa. Lissu akipata hata wabunge 4 njoo PM nikupe 100,000 ya kununulia bando!
Unakimbia hoja. Acha mbwembwe tuendelee na hoja ya kubomolea watu nyumba. Mbona Mwanza hakuwabomolea?

Akatamka kwa kinywa kipana mbele ya camera kwamba habomoi kwa vile walimpigia kura.

Hakianani akipata 20% huyu dikteta nakunywa sumu
 
Ni ukatili wa Hali ya juu sana kuwabomolea watu nyumba zao bila kujali kuna watoto, wagonjwa, wazee, wanafunzi eti hisia awakukupigia kura sijui hizo takwimu walipata wapi
 
Wakazi waliobomolewa wenyewe walikiri kuwa walinunua viwanja/nyumba kutoka kwa wamiliki wa awali ambao walikuwa tayari walishalipwa fidia hivyo waliingizwa mkenge. Wapo pia ambao walikula fidia na kugoma kuondoka ila pia watu hawabomolewi hivi hivi zipo sheria za hifadhi za barabara.

Kwa hapa Mwanza njoo hapa Buswelu uone watu walivyobomolewa nyumba (nimeitaja Buswelu kwasababu ndipo upomoaji wa hivi karibuni maana nyie mnasahau haraka)
Bora ufunge domo lako kama hujui maumivu tuliyoyapitia....
 
Wee! Wee! Wee! Usiwasemee. Hujui ni maumivu kiasi gani wamepitia kwa ukatili aliyoyafanya huyu

Sasa kama lengo lake ilikuwa kuwabomolea waliokiuka sheria kwann Mwanza sheria haikufuatwa.

Tukutane 28/10/2020 tumfundishe adabu huyu dikteta uchwara
Safari Hadi Geita Chato wajiandae kupelekewa tingatinga kwa kuhudhiria kwa wingi mikutano ya Lisu.
 
Back
Top Bottom