Ni vigumu sana yeyote kudai yuko neutral kwenye siasa

jd41

JF-Expert Member
Aug 23, 2015
3,756
4,842
Wakuu Salaam.

Kuna watu wanaodai wapo neutral kwenye siasa, kwamba wao hawana upande. Wamekuwa wakirudia kauli zao mara kwa mara kujaribu kuuaminisha umma wanachokisema ni sahihi, japo ni ngumu sana kukipeleka kwenye practical (kiuhalisia).

Hasa ukizingatia kwamba, maisha ya mwanadamu wa kawaida yametawaliwa na hisia kwa kiasi kikubwa, hivyo mtu huweza kujikuta amependa au kuchukia upande fulani, sio tu kwasababu ya kile wanachofanya, bali pia inawezekana mtu akaupenda upande huo kutokana na kupendezwa na mtu fulani aliyepo upande huo.

Hivyo automatically, utapompenda mtu huyo wa upande fulani, ni rahisi sana kujikuta umeangukia upande huo bila wewe mwenyewe kujijua.

Lakini pia, kwenye upande wa waandishi, ili uwe neutral kwenye siasa, jambo la msingi kabisa, ni lazima uhakikishe kwa kila hoja unayoizungumzia, lazima uguse pande zote mbili; mfano: kama jambo fulani limetokea ikaonekana upande mmoja umeonewa na upande mwingine, liseme wazi bila kusita, at the same time ukiutaka upande wa pili kuacha matendo, yake maovu kwa upande ulioonewa, na kinyume chake.

Hili linahitaji ujasiri wa dhati, ili ufanye hivyo sharti la kwanza ni lazima uwe tayari kuonekana mbaya na upande utakaoulamu. Hivyo, kwa mfano upande unaoulaumu ndio wenye nguvu ( polisi, bunge) utajikuta unaogopa kuukemea wazi kwa matendo yake mabaya kuogopa adhabu yao.

Mara nyingi utajikuta unakuwa na tabia ya kun'gata na kupuliza; lakini kwenye siasa hilo ni gumu kutendeka kwasababu matukio yanayotokea yanaonekana wazi, zuri linaonekana, na baya linaonekana pia.

Wakati wewe ukijaribu kuficha lile baya la upande wa wenye nguvu, wengine kwa upande wao wanakuwa tayari walishaliona, hivyo regardless ya chochote utachoandika, watakuwa tayari wanaujua ukweli.

Ni rahisi sana kuegemea kulaumu upande mmoja zaidi kwasababu kwanza; hawa hawana cha kukufanya zaidi ya kelele tu za wapenzi na wanachama wake, pili; kuufurahisha upande wa pili, ambao ndio wa wenye nguvu.

Hivyo, mtu au watu wa aina hii, wanaojinasibu wako neutral, hujikuta wanakosa uhuru wa kuandika ukweli na kujikuta wamefungwa kimawazo, either kwa kujua au kutojua, wataandika yale wanayoamini hayatawasababishia matatizo, na hii ni nature ya kibinadamu, siku zote tunahitaji kuwa sehemu salama, tujihisi salama (kimawazo na matendo).

Matokeo yake hili huondoa ile dhana ya mtu kudai kuwa neutral, mara nyingi utajikuta unaendelea kuegemea kulaumu upande dhaifu, ili kujihakikishia usalama wako.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu nakubalina na wewe kwa kiasi ila inabidi kuchukuwa tahadhari unapozungumzia neno kuwa 'Neutral' Au kutokuwa 'Neutral' kwenye jamii hii, kwa sababu wakati mwingine unachosema na ambacho watu wanakusikia ukisema ni tofauti.

Kwa hali ya siasa zetu ilivyo, kusema ukweli bila Kujali nani ni nani, na nani atanufaika au kuumia kutokana na ukweli huo ndio kitu kinachotakiwa. Yaani penye ukweli unasema ukweli, anayekosea unasema kakosea aunayepatia unasema kapatia na huo ndio u neutral kwa muktadha huu (ukumbuke kwa hatua tuliyofikia ukisema usiwe neutral, watu wanakuelewa unasema utie U CCM au UCHADEMA kwenye kila hoja yako). Pia ikumbukwe kwenye tukio moja linalohusisha pande kadhaa, zote zinaweza kuwa zinakosea kwa namna Fulani nakupatia kwa namna Fulani, au mmoja umekosea mwingine kupatia, au wote wamekosea au wote wamepatia, kwa hiyo pia ni muhimu kulielewa hili.

Kuangalia mambo kwa jicho hilo sio tu kwamba inatakiwa bali ni muhimu sana kuliokoa taifa. Cha msingi ni kutumia lugha ya staha na kushawishi wahusika kubadilika in a positive way na si matusi na kejeli ambazo badala ya kuchochea improvements, yanachochea migogoro ambayo inaelekea kwenye shari.

Kinyume chake, ni mtu kutetea upande (kwa hoja hihyo hiyo ya kwamba hauwezi kuwa neutral) kwa hiyo anapotetea jambo, hatetei kwa kuwa jambo lenyewe anaona ni jema bali kulingana na upande aliopo, na anapokemea jambo hakemei kwa kuwa jambo lenyewe ni baya kwa asili yake bali kwa sababu ya upande aliopo.Hii inakuwa ni mbaya sana kwani inasababisha jamii kushindwa kujua lipi baya na lipi zuri katika ujumla wake na inakuwa ni vurugu na uhuni.

Kwa hiyo hiyo concecept ya kuwa neutral au kutokuwa neutral nayo pia inaweza kutumika vizuri au vibaya au kufanyiwa manipulation kwa maslahi binafsi au ya kundi. La msingi ni kujenga uelewa mpana Zaidi.
 
Na kwa lugha rahisi Zaidi katika kuielewa point ya mleta mada, ni vizuri kurudi kwenye kanuni kuu ya uadilifu. Kufanya maamuzi ambayo ni sahihi hata kama maamuzi hayo yanawanufaisha wengine kuliko yanavyokunufaisha wewe mwenyewe.

Kushughulika na wengina kama ambavyo ungependa wengine wakushughulikie kwenye scenario inayofanana. Kujiweka kwenye nafasi ya unayemuhukumu kabla ya kumhukumu.Kusema ukweli hata kama ukweli huo huupendi lakini ndio haki.
 
Vile vile hapo uliposema "mwenye nguvu", nadhani ishu si mwenye nguvu versus asiye na nguvu. Kwenye suala linalohusika mwenye nguvu anaweza awe sahihi na asiye na nguvu asiwe sahihi na kinyume chake. Kwa hiyo unapotaka kuona vitu katika jicho sahihi, hupaswi kuangalia kwa jicho la mwenye nguvu na asiye na nguvu, bali aliyeko sahihi dhidi ya ambaye amekosea kwenye jambo husika.
 
Mkuu nakubalina na wewe kwa kiasi ila inabidi kuchukuwa tahadhari unapozungumzia neno kuwa 'Neutral' Au kutokuwa 'Neutral' kwenye jamii hii, kwa sababu wakati mwingine unachosema na ambacho watu wanakusikia ukisema ni tofauti.

Kwa hali ya siasa zetu ilivyo, kusema ukweli bila Kujali nani ni nani, na nani atanufaika au kuumia kutokana na ukweli huo ndio kitu kinachotakiwa. Yaani penye ukweli unasema ukweli, anayekosea unasema kakosea aunayepatia unasema kapatia na huo ndio u neutral kwa muktadha huu (ukumbuke kwa hatua tuliyofikia ukisema usiwe neutral, watu wanakuelewa unasema utie U CCM au UCHADEMA kwenye kila hoja yako). Pia ikumbukwe kwenye tukio moja linalohusisha pande kadhaa, zote zinaweza kuwa zinakosea kwa namna Fulani nakupatia kwa namna Fulani, au mmoja umekosea mwingine kupatia, au wote wamekosea au wote wamepatia, kwa hiyo pia ni muhimu kulielewa hili.

Kuangalia mambo kwa jicho hilo sio tu kwamba inatakiwa bali ni muhimu sana kuliokoa taifa. Cha msingi ni kutumia lugha ya staha na kushawishi wahusika kubadilika in a positive way na si matusi na kejeli ambazo badala ya kuchochea improvements, yanachochea migogoro ambayo inaelekea kwenye shari.

Kinyume chake, ni mtu kutetea upande (kwa hoja hihyo hiyo ya kwamba hauwezi kuwa neutral) kwa hiyo anapotetea jambo, hatetei kwa kuwa jambo lenyewe anaona ni jema bali kulingana na upande aliopo, na anapokemea jambo hakemei kwa kuwa jambo lenyewe ni baya kwa asili yake bali kwa sababu ya upande aliopo.Hii inakuwa ni mbaya sana kwani inasababisha jamii kushindwa kujua lipi baya na lipi zuri katika ujumla wake na inakuwa ni vurugu na uhuni.

Kwa hiyo hiyo concecept ya kuwa neutral au kutokuwa neutral nayo pia inaweza kutumika vizuri au vibaya au kufanyiwa manipulation kwa maslahi binafsi au ya kundi. La msingi ni kujenga uelewa mpana Zaidi.
Mkuu nime base zaidi andiko langu kwa kuwalenga baadhi ya waandishi wa habari wanaojinasibu wako neutral, sikumlenga mtu wa kawaida, hivyo nikawa nina express concern zangu kwa hao waandishi, sababu wanachokifanya kina direct influence kwenye society, hivyo wakilazimisha wako neutral lazima waoneshe u- neutral wao kwasababu wanatakiwa kuonekana kama referee.

Lakini kwa mazingira ya sasa hapa nchini kwetu, ni ngumu sana mtu (mwandishi), kudai yuko neutral hasa ukizingatia nguvu zilizopo baina ya makundi mawili.

Kuna kundi moja lina nguvu zaidi ya kundi jingine kimamlaka, hivyo huyu mwandishi anapojinasibu kuwa neutral wakati mwingine anajikuta automatically anaegemea upande wenye nguvu kwa kuhofia adhabu toka upande huo, anajihakikishia usalama wake kwanza.

Ndio nikaonesha kundi jingine lenyewe halina nguvu zaidi ya kelele za wanachama na wapenzi wake. Hivyo ni rahisi sana kuliumiza kundi hili.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vile vile hapo uliposema "mwenye nguvu", nadhani ishu si mwenye nguvu versus asiye na nguvu. Kwenye suala linalohusika mwenye nguvu anaweza awe sahihi na asiye na nguvu asiwe sahihi na kinyume chake. Kwa hiyo unapotaka kuona vitu katika jicho sahihi, hupaswi kuangalia kwa jicho la mwenye nguvu na asiye na nguvu, bali aliyeko sahihi dhidi ya ambaye amekosea kwenye jambo husika.
Sawa nakubaliana na wewe; lakini swali la kujiuliza, je, huyu mwandishi anaedai yuko neutral anaweza kweli kukemea baya la upande wa wenye nguvu bila kuhofia usalama wake? ana uwezo huo hasa ukizingatia hali halisi nchini petu, na matumizi ya taasisi kama bunge?

N.B. Kutumia neno mwenye nguvu au asie na nguvu imekuja automatically, kwasababu naamini kabisa, huyu mwandishi kabla hajanyanyua kalamu yake aanze kukemea upande wowote lazima afanye consideration ya baadhi ya factors, anaweza jikuta yuko mwepesi zaidi kukemea upande mmoja zaidi ya mwingine kwa maslahi ya usalama wake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Eti kuna watu wanadai tume huru, kwamba kwenye hiyo tume hakutakuwa na watu wenye uvyama! Ni hoja ya kitoto sana.
 
Sawa nakubaliana na wewe; lakini swali la kujiuliza, je, huyu mwandishi anaedai yuko neutral anaweza kukemea baya la upande wa wenye nguvu bila kuhofia usalama wake? ana uwezo huo hasa ukizingatia hali halisi nchini petu, na matumizi ya taasisi kama bunge?

Sent using Jamii Forums mobile app
Lakini mkuu kazi za waandishi wa habari profesioanal sio kukemea au kisifu mambo, bali kuripoti na kuchambua habari, na neutrality kwao ni moja ya professional ethics.sasa tunaweza tena kusema waiache?

Kwa hiyo inawezekana kuna vitu tunachanganya hapa.

Vile vile siamini sana kwenye ku attack watu au makundi, naamini ufanisi hutokana na ku attack tatizo na sio mtu au kundi bila kujali nani ni nani, nani ana nguvu nani hana, n.k

Kwa mfano, kama wewe ni shekhe au mchungaji, ukiwa msikitini au kanisani kemea uchawi (kama tatizo) usiseme wewe hasani au Yakobo ni mchawi! Hata kama hao watu kweli wachawi,ukisema hiyo utakuwa unakuza tatizo badala ya kulitatua. Na pia unaweza kutengeneza shida mpya juu ya shida ya msingi
 
Mkuu nakubalina na wewe kwa kiasi ila inabidi kuchukuwa tahadhari unapozungumzia neno kuwa 'Neutral' Au kutokuwa 'Neutral' kwenye jamii hii, kwa sababu wakati mwingine unachosema na ambacho watu wanakusikia ukisema ni tofauti.

Kwa hali ya siasa zetu ilivyo, kusema ukweli bila Kujali nani ni nani, na nani atanufaika au kuumia kutokana na ukweli huo ndio kitu kinachotakiwa. Yaani penye ukweli unasema ukweli, anayekosea unasema kakosea aunayepatia unasema kapatia na huo ndio u neutral kwa muktadha huu (ukumbuke kwa hatua tuliyofikia ukisema usiwe neutral, watu wanakuelewa unasema utie U CCM au UCHADEMA kwenye kila hoja yako). Pia ikumbukwe kwenye tukio moja linalohusisha pande kadhaa, zote zinaweza kuwa zinakosea kwa namna Fulani nakupatia kwa namna Fulani, au mmoja umekosea mwingine kupatia, au wote wamekosea au wote wamepatia, kwa hiyo pia ni muhimu kulielewa hili.

Kuangalia mambo kwa jicho hilo sio tu kwamba inatakiwa bali ni muhimu sana kuliokoa taifa. Cha msingi ni kutumia lugha ya staha na kushawishi wahusika kubadilika in a positive way na si matusi na kejeli ambazo badala ya kuchochea improvements, yanachochea migogoro ambayo inaelekea kwenye shari.

Kinyume chake, ni mtu kutetea upande (kwa hoja hihyo hiyo ya kwamba hauwezi kuwa neutral) kwa hiyo anapotetea jambo, hatetei kwa kuwa jambo lenyewe anaona ni jema bali kulingana na upande aliopo, na anapokemea jambo hakemei kwa kuwa jambo lenyewe ni baya kwa asili yake bali kwa sababu ya upande aliopo.Hii inakuwa ni mbaya sana kwani inasababisha jamii kushindwa kujua lipi baya na lipi zuri katika ujumla wake na inakuwa ni vurugu na uhuni.

Kwa hiyo hiyo concecept ya kuwa neutral au kutokuwa neutral nayo pia inaweza kutumika vizuri au vibaya au kufanyiwa manipulation kwa maslahi binafsi au ya kundi. La msingi ni kujenga uelewa mpana Zaidi.

Azizi umevamia hii mada na kuanza kuijadili kifalsafa kiasi umehama kwenye muktadha halisi. Huyu mleta mada amewalenga wale wanaojitaja kuwa neutral mfano Paskali Mayalla. Ukweli ni kuwa hawa wanaosema wako neutral Ni bora wakae kimya tu maana hata mabandiko yao tunayaona kuwa hayako neutral.
 
Na kwa uelewa wangu, tunapotaka kuona mambo kwenye mwanga bora, tunatakiwa tujiepushe kujenga hoja zetu nyuma ya vivuli vya makundi. Ukijenga hoja yoyote nyuma ya kivuli cha kundi, unatengeneza offensive Vs Deffensive forces.

Ukishatengeneza hiyo nguvu mbili tayari unakuwa umefunga milango ya kufikiri na kuangalia usahihi wa vitu na kufungua milango ya mabishano, mivutano, n.k na kimsingi hiyo ndicho kipindi tunachopita kwa sasa
 
Lakini mkuu kazi za waandishi wa habari profesioanal sio kukemea au kisifu mambo, bali kuripoti na kuchambua habari, na neutrality kwao ni moja ya professional ethics.sasa tunaweza tena kusema waiache?

Kwa hiyo inawezekana kuna vitu tunachanganya hapa.

Vile vile siamini sana kwenye ku attack watu au makundi, naamini ufanisi hutokana na ku attack tatizo na sio mtu au kundi bila kujali nani ni nani, nani ana nguvu nani hana, n.k

Kwa mfano, kama wewe ni shekhe au mchungaji, ukiwa msikitini au kanisani kemea uchawi (kama tatizo) usiseme wewe hasani au Yakobo ni mchawi! Hata kama hao watu kweli wachawi,ukisema hiyo utakuwa unakuza tatizo badala ya kulitatua. Na pia unaweza kutengeneza shida mpya juu ya shida ya msingi

Uko nje ya muktadha, unaposema ww sio muumini wa kuatack watu basi ujue ww ni kama muhubiri, na mara nyingi unapojadili jambo kwa ujumla wake bila kumtaja mtu direct kwa lengo la kuonyesha mfano, hiyo hoja inabaki hewani. Hapa sio kwenye darasa la saikolojia bali ni kwenye mtandao wa kijamii, unapaswa kutoa mifano halisi ili lengo kumfikiria muhusika.
 
Azizi umevamia hii mada na kuanza kuijadili kifalsafa kiasi umehama kwenye muktadha halisi. Huyu mleta mada amewalenga wale wanaojitaja kuwa neutral mfano Paskali Mayalla. Ukweli ni kuwa hawa wanaosema wako neutral Ni bora wakae kimya tu maana hata mabandiko yao tunayaona kuwa hayako neutral.
Neutrality ya mtu ambaye haieleweki anaunga mkono ni ni na haungi mkono nini hiyo ni tatizo moja kwa moja na haikubaliki. Hiyo kwa lugha nyepesi ni unafiki na nivizuri kuiita hiyo kwa sababu maana ya neutrality inaweza kuwa ni kitu cha tofauti kidogo
 
Mkuu nime base zaidi andiko langu kwa kuwalenga baadhi ya waandishi wa habari wanaojinasibu wako neutral, sikumlenga mtu wa kawaida, hivyo nikawa nina express concern zangu kwa hao waandishi, sababu wanachokifanya kina direct influence kwenye society, hivyo wakilazimisha wako neutral lazima waoneshe u- neutral wao kwasababu wanatakiwa kuonekana kama referee.

Lakini kwa mazingira ya sasa hapa nchini kwetu, ni ngumu sana mtu (mwandishi), kudai yuko neutral hasa ukizingatia nguvu zilizopo baina ya makundi mawili.

Kuna kundi moja lina nguvu zaidi ya kundi jingine kimamlaka, hivyo huyu mwandishi anapojinasibu kuwa neutral wakati mwingine anajikuta automatically anaegemea upande wenye nguvu kwa kuhofia adhabu toka upande huo, anajihakikishia usalama wake kwanza.

Ndio nikaonesha kundi jingine lenyewe halina nguvu zaidi ya kelele za wanachama na wapenzi wake. Hivyo ni rahisi sana kuliumiza kundi hili.

Sent using Jamii Forums mobile app

Mkuu tofauti ninayoiona kwako na Aziz, ww unajadili uhalisia wa sasa, Azizi anajadili nadharia za darasani. Kimsingi Azizi ana hoja za msingi lakini hazipo kwenye uhalisia. Huyo nimeshamjua, huwa anajadili inavyopaswa kuwa, na sio ilivyo. Ukibaki naye atakutoa kwenye hoja ya msingi, na atakurudisha darasani muishie kujadili nadharia.
 
Uko nje ya muktadha, unaposema ww sio muumini wa kuatack watu basi ujue ww ni kama muhubiri, na mara nyingi unapojadili jambo kwa ujumla wake bila kumtaja mtu direct kwa lengo la kuonyesha mfano, hiyo hoja inabaki hewani. Hapa sio kwenye darasa la saikolojia bali ni kwenye mtandao wa kijamii, unapaswa kutoa mifano halisi ili lengo kumfikiria muhusika.
Mfano, nikisema wewe tindo mchawi, acha uchawi, uchawi wako tushauchoka n.k, kitakachofuata kama una uwezo utanipiga ngumi, kama mchawi kweli utaniloga, kama unaweza kunihujumu kwa siri au kwa uwazi utanihujumu, ukishindwa yote utaniambia mchawi mwenywewe! Na mimi nitakujibu ,unaniambia hivyo mimi? Ngoja nitakuonesha kazi! wewe utanijibu huwezi nifanya chochote n.k

hapo tunatatua tatizo, au tunatumia tatizo kutengeneza ma tatizo mapya?

Unasema ku attack ma tatizo bila ku attack personalities ni mahubiri? Kwa ni mahubiri ni jambo jema au baya? Nijuavyo mahubiri ni kukemea mabaya na kuhamasisha mema
 
Neutrality ya mtu ambaye haieleweki anaunga mkono ni ni na haungi mkono nini hiyo ni tatizo moja kwa moja na haikubaliki. Hiyo kwa lugha nyepesi ni unafiki na nivizuri kuiita hiyo kwa sababu maana ya neutrality inaweza kuwa ni kitu cha tofauti kidogo

Ndio hapo hoja ya msingi ya mleta uzi ilipo. Mtu anasema yuko neutral, kisha ukiangalia maandishi yake hayako neutral na mazingira hayaruhusu kuwa neutral. Sasa ww unataka kujadili kama ni darasa ambalo watu wanajifunza saikolojia! Aziz mengi ya mabandiko yako yana hoja za msingi, lakini sehemu kubwa kutokana na uhalisia uliopo huwa inageuka kuwa kama kiongozi wa kidini anayefundisha saikolojia. Hatukuzuii kuweka mabandiko yako maana kuna vitu tunapata, lakini huku kwenye mitandao ya kijamii beleshi linaitwa beleshi na sio kijiko kikubwa cha kuchotea mchanga fullstop.
 
Mkuu tofauti ninayoiona kwako na Aziz, ww unajadili uhalisia wa sasa, Azizi anajadili nadharia za darasani. Kimsingi Azizi ana hoja za msingi lakini hazipo kwenye uhalisia. Huyo nimeshamjua, huwa anajadili inavyopaswa kuwa, na sio ilivyo. Ukibaki naye atakutoa kwenye hoja ya msingi, na atakurudisha darasani muishie kujadili nadharia.
Sasa mkuu kwani situnatakiwa kuwa inavyotakiwa tuwe? Au tunapaswa kuwa tulivyo? Mfano ni nadharia gani niliyoeleza isiyotekelezaka kokote kule au kwenye hoja hii?

Sasa kama tunapaswa kuwa tulivyo kuna haja gani ya kujadili, kujifunza, kulalamika, kulaumu n.k?
 
Mimi nipo neutral na nina enjoy being neutral in politics. Ni jambo jepes. Amua kutumia akili na kuweka hisia au mahaba pembeni. Then una enjoy siasa. Utasifu pa kusifu na kukosoa pa kukosoa. Binafsi huwa naweza penda kitu lakini siachi kutumia akili. Love but take your brain with love


Wakuu Salaam.
Kuna watu wanaodai wapo neutral kwenye siasa, kwamba wao hawana upande. Wamekuwa wakirudia kauli zao mara kwa mara kujaribu kuuaminisha umma wanachokisema ni sahihi, japo ni ngumu sana kukipeleka kwenye practical (kiuhalisia).

Ili uwe neutral kwenye siasa, jambo la msingi kabisa, ni lazima uhakikishe kwa kila hoja unayoizungumzia, lazima uguse pande zote mbili; mfano: kama jambo fulani limetokea ikaonekana upande mmoja umeonewa na upande mwingine, liseme wazi bila kusita, at the same time ukiutaka upande wa pili kuacha matendo, yake maovu kwa upande ulioonewa, na kinyume chake.

Hili linahitaji ujasiri wa dhati, ili ufanye hivyo sharti la kwanza ni lazima uwe tayari kuonekana mbaya na upande utakaoulamu. Hivyo, kwa mfano upande unaoulaumu ndio wenye nguvu ( polisi, bunge) utajikuta unaogopa kuukemea wazi kwa matendo yake mabaya kuogopa adhabu yao.

Mara nyingi utajikuta unakuwa na tabia ya kun'gata na kupuliza; lakini kwenye siasa hilo ni gumu kutendeka kwasababu matukio yanayotokea yanaonekana wazi, zuri linaonekana, na baya linaonekana pia.

Wakati wewe ukijaribu kuficha lile baya la upande wa wenye nguvu, wengine kwa upande wao wanakuwa tayari walishaliona, hivyo regardless ya chochote utachoandika, watakuwa tayari wanaujua ukweli.

Ni rahisi sana kuegemea kulaumu upande mmoja zaidi kwasababu kwanza; hawa hawana cha kukufanya zaidi ya kelele tu za wapenzi na wanachama wake, pili; kuufurahisha upande wa pili, ambao ndio wa wenye nguvu.

Hivyo, mtu au watu wa aina hii, wanaojinasibu wako neutral, hujikuta wanakosa uhuru wa kuandika ukweli na kujikuta wamefungwa kimawazo, either kwa kujua au kutojua, wataandika yale wanayoamini hayatawasababishia matatizo, na hii ni nature ya kibinadamu, siku zote tunahitaji kuwa sehemu salama, tujihisi salama (kimawazo na matendo).

Matokeo yake hili huondoa ile dhana ya mtu kudai kuwa neutral, mara nyingi utajikuta unaendelea kuegemea kulaumu upande dhaifu, ili kujihakikishia usalama wako.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mfano, nikisema wewe tindo mchawi, acha uchawi, uchawi wako tushauchoka n.k, kitakachofuata kama una uwezo utanipiga ngumi, kama mchawi kweli utaniloga, kama unaweza kunihujumu kwa siri au kwa uwazi utanihujumu, ukishindwa yote utaniambia mchawi mwenywewe! Na mimi nitakujibu ,unaniambia hivyo mimi? Ngoja nitakuonesha kazi! wewe utanijibu huwezi nifanya chochote n.k

hapo tunatatua tatizo, au tunatumia tatizo kutengeneza ma tatizo mapya?

Unasema ku attack ma tatizo bila ku attack personalities ni mahubiri? Kwa ni mahubiri ni jambo jema au baya? Nijuavyo mahubiri ni kukemea mabaya na kuhamasisha mema

Ngoja nikupe mfano mzuri, tuseme ww ni mwizi, mimi sipaswi kukuambia ww ni mwizi mpaka nitafute lugha ya staha ambayo itakufarahusha ww? Au najua kabisa we ni muuaji nitasubiri nitengeneze lugha za kiungwana kukuambia ww ni muuaji, eti kisa nitatengeneza ugomvi!?

Ninaposema mahubiri namaanisha kuwa ni kama muongozo usio na shuruti bali ushawishi wa kukufanya ufuate kwa utashi wako. Mara nyingi mahubiri huwa yanaelekezwa kwa kundi la watu, ambao utakuta hata hayo yanayohubiriwa hakuna aliye kinyume chake.
 
Aziz mengi ya mabandiko yako yana hoja za msingi, lakini sehemu kubwa kutokana na uhalisia uliopo huwa inageuka kuwa kama kiongozi wa kidini
mengine uliyosema kwenye hili nakubaliana na wewe, ila umekuwa ukinipa shida kidogo kwenye hili kwa muda kidogo sasa.

Kwa ni ni unadhani kama wanaopaswa kukemea maovu na kuhamashisha mabaya wanapaswa kuwa viongozi wa dini peke yao?,hivyo anayefanya hivyo ni kiongozi wa dini? Lakini unachonishangaza zaidi, kwa ni ni unadhani kuwa au ku- behave kama kiongozi wa dini kwenye kukemea jambo baya au kuhamasisha jambo zuri si sawa?

Au kama unaamini ni sawa na ni muhimu, sasa concept yako ya dini unai conect vipi kwenye mijadala hii?

Kusema kweli sijawahi kukuelewa vyema kwenye kipengele hiki
 
Back
Top Bottom