Ni vigumu sana kwa Marekani kuifikia China kwenye mahusiano na nchi za Afrika

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,034
VCG31N1369803557.jpg

Fadhili Mpunji

Ni zaidi ya miezi sita sasa tangu Marekani itangaze pendekezo lake la ujenzi wa miundo mbinu wa Build Back Better World ( B3W), ambao ilisema lengo lake ni kukabiliana na vitendo visivyofaa vya kugharamia miradi ya miundo mbinu vya China, vinavyoziingiza kwenye changamoto kubwa nchi zinazopokea fedha za ujenzi wa miundo mbinu kutoka kwa China. Wakati Marekani ilipotangaza mpango huo, wapo walioupokea kwa furaha, wakiuita utachangia juhudi za China katika kuhimiza maendeleo ya miundo mbinu, lakini wengine walionyesha kuutilia shaka.

Kiuhalisi pendekezo la Build Back Better World lililotangazwa kwenye mkutano wa kundi la G7 huko Glasgow, Scotland, sio kama lilitolewa ili kuboresha hali ya miundo mbinu duniani, kimsingi lilitolewa kuleta changamoto kwa pendekezo la ‘Ukanda mmoja, Njia moja” (BRI) la China, ambalo limepokelewa vizuri na nchi nyingi duniani. Kwa nchi za Afrika, baadhi ya watu waliona kuwa, bila kujali kama ni changamoto kwa China au ni nia njema ya Marekani kwa Afrika, pendekezo hilo lilionekana ni zuri. Lakini katika miezi hii sita hakuna kubwa lilioonekana, na mwelekeo wake bado hauko wazi.

Sababu ya kwanza inayofanya pendekezo la Marekani lionekane kutokuwa na mwelekeo, ni msingi wake kutokuwa madhubuti kama ilivyo kwa pendekezo la “Ukanda mmoja, njia moja”. Msingi wa pendekezo la ukanda mmoja, njia moja ni kujenga jumuiya ya binadamu kwenye mustakabali wa pamoja, yaani pande zote zinanufaika. Hii ina maana kuwa kupitia pendekezo la ukanda mmoja njia moja, makampuni ya China yanashiriki kwenye ujenzi wa miundo mbinu Afrika na kupata faida, na nchi za Afrika zinapata miundo mbinu ya kisasa iliyojengwa kwa gharama nafuu, ambayo imekuwa katika hali mbaya kwa muda mrefu. Kuna ushahidi karibu katika kila nchi ya Afrika, iwe ni kwenye barabara kuu, barabara za mijini, viwanja vya ndege au bandari zilizojengwa au kuboreshwa chini ya mpango huo. Lakini pendekezo la Marekani msingi wake ni kukabiliana na China.

Sababu ya pili ni kuwa msingi wa pendekezo la “ukanda mmoja, njia moja” ni majadiliano kati ya pande mbili. Majadiliano hayo yanazingatia mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na mahitaji ya nchi, gharama za miradi, uwezo wa kulipa na njia za kulipa. Pande mbili yaani China na Afrika zinakaa pamoja. Kupitia pendekezo hilo kuna miradi ya msaada, kuna miradi ya ushirikiano na miradi ya kibiashara, lakini mwisho wa siku miradi inajengwa. Lakini bado haiko wazi kwa pendekezo la Build Back Better World la Marekani, kama mahitaji na sio sababu za kisiasa (yaani kuilenga China) ndio itakuwa msingi wa majadiliano ya ujenzi wa miradi.

Sababu ya tatu, ni kwamba licha ya kuwa pendekezo la Build Back Better World linatajwa kuwa ni la Marekani, uhalisi wake ni tofauti kiasi. Ikumbukwe kuwa pendekezo hilo lilitangazwa kwenye mkutano wa kundi la G7, na lilitajwa kuunganisha wadau mbalimbali wa kundi la nchi hizo saba kwenye utekelezaji wa miradi hiyo. Itakuwa ni jambo zuri kama nchi nyingine za kundi hilo zitasaidia utekelezaji wa miradi ya pendekezo la Build Back Better World, lakini ni vigumu kwa nchi hizo kuburuzwa kutekeleza miradi ambayo Marekani inataka ili kukabiliana na China barani Afrika wakati hazina nia hiyo.

Jambo la nne ni kuwa masharti ya kisiasa mara nyingi huambatana na uwekezaji au misaada inayotoka Marekani kwenda kwa nchi nyingine hasa za Afrika. Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Bw. Anthony Blinken alijaribu kugusia kidogo jambo hilo akisema sio nia ya Marekani kuweka masharti ya ajabu. Lakini uhalisi ni kuwa tayari kuna masharti kadhaa ambayo kama sio kikwazo kwenye utekelezaji wa pendekezo hilo la Marekani, ni msingi wa ubaguzi au kuzigawa nchi za Afrika.

Kwa sasa kuna pengo kubwa sana kati ya China na Marekani kwenye uwekezaji kwenye miundombinu barani Afrika. Takwimu zilizotolewa na ripoti ya IJ Global kuhusu mabadiliko ya mwelekeo wa uwekezaji kwenye miundombinu barani Afrika [New Dynamics: Shifting Patterns in Africa’s Infrastructure Funding], inaonesha kuwa kati ya mwaka 2008 hadi mwaka 2021 Marekani imewekeza dola za kimarekani bilioni 8.3 kwenye miundo mbinu, wakati katika kipindi hicho hicho China imewekeza dola za kimarekani bilioni 29. Katika mazingira kama ya sasa, na kwa pengo kubwa namna hii, ni vigumu sana kwa Marekani kufikia China.
 
Tuipe Africa miaka mingapi kabla haijageuzwa koloni la china linalonuka madeni???????
Kila nikitizama ya zambia na Uganda sina hamu na wachina barani Africa. Tuwe nao makini hawa wachina.
China anakushikia bunduki ili usaini hiyo mikataba feki?

Kama ile bandari ya Bagamoyo si unaelewa kabisa athari zake, sasa hapo mwenye kosa ni nani kama si kumsingizia tu China lawama za kipumbavu?
 
China anakushikia bunduki ili usaini hiyo mikataba feki?

Kama ile bandari ya Bagamoyo si unaelewa kabisa athari zake, sasa hapo mwenye kosa ni nani kama si kumsingizia tu China lawama za kipumbavu?
Unahakika china kwenye huo mradi wa Bagamoyo hakumshikia mtu Bunduki???? Emu fanya kama vile unafikiria kwa kutumia MULTIPLE DIMENSIONAL ANALYSIS na sio single dimensional analysis ulionayo sasa hivi.
 
Bora mmarekani kuliko mchina..mchina mnyonyaji pia mnyanysaji sana kwa wafanyakazi.

Marekani ni mnyonyaji wa uchumi wa nchi ila wafanyakazi wake wanaenjoy sana.

#MaendeleoHayanaChama
 
Mchina anaiingiza Afrika kwenye ulimwengu wa kisasa kwa bei nafuu iwe smart phone,tv vifaa vya umeme 'vya ujenzi 'mavazi 'vyombo vya nyumbani jioni nk

Marekani na Ulaya huwezi gusa bei vitu vyao hata uwe middle class Afrika

Mchina kusaidia Afrika kuingia modern world
 
Ila na hao wamarekani na nduguze walijisahau wao wanawaza vita tu mara osama bin laden,,mullah,,saadam hussein,,gadaff,,uku wakimchungulia kiduku mara iran bado palestine,,wakati wenzake wanapiga show achane na mchina ni ndugu yetu huku kwa sasa
 
Back
Top Bottom