Ni vigezo vipi vilivyoipa Star TVushindi wa zabuni ya kuonesha Ligi ya VodaCom?

Balantanda

JF-Expert Member
Jul 13, 2008
12,476
4,752
Salama wakuu?...Kwa muda mrefu nimekuwa nikiwaza na kuwazua na kujiuliza maswali kibao juu ya vigezo vilivyoipa Star TV mkataba wa kuonesha moja kwa moja michezo ya VPL....Pamoja na kushinda zabuni hiyo Star TV wameshindwa kuoneshwa michezo ya VP iliyochezwa nje ya jiji la Mwanza kwa madai kwamba gari lao la kurushia matangazo haliwezi kusafiri umbali mrefu(kwamba linaenda mwendo wa 20km/h)....Hii ina maana kwamba hawataonesha mechi zinazochezwa nje ya Mwanza,kwamba mechi za Morogoro,Dodoma n.k hazitaoneshwa kwa sababu ya hilo gari la matangazo...

Ina maana TFF(ama waliopewa jukumu la kupitia zabuni) hawakuliona hili wakati wakipitia zabuni hizi?,ni bora wangepewa TBC ama ITV kuliko hawa wababaishaji wa Star TV......
 
Mkuu kibonbo bongo unategemea station gani inaweza kurusha mechi zote live tz nzima.
mechi zenyewe zinachezwa wakati mmoja
 
Mkuu kibonbo bongo unategemea station gani inaweza kurusha mechi zote live tz nzima.
mechi zenyewe zinachezwa wakati mmoja

Tatizo sio kuonesha mechi nchi nzima kwa wakati mmoja...Swali hapa ni ilikuwaje wakapewa mkataba wa kuonesha VPL(ambayo inachezwa mikoa tofauti tofauti) ilhali hawana uwezo wa kuonesha katika maeneo hayo tofauti na wana uwezo wa kuonesha mechi za Mwanza tu???...

Mara nyingi wameulizwa kwa nini wasiende hata Morogoro(kituo kilichokuwa mna timu nyingi za Yanga,African Lyon,JKT Ruvu,Ruvu Shooting na Mtibwa waliokuwa Manungu) na kuweka kambi hapo kuonesha mechiza VPL...Jibu walilolitoa ni kwamba hawawezi kusafiri kwenda sehemu yoyote nje ya Mwanza kwa wakati kwani gari lao linatembea 20km/h.........Kama sio ubabaishaji ni nini hii
 
Tunaweza kulalamika hapa bila kujua pengine wao ndio walioonekana bora kuliko wengine,
pengine wao ndio pekee walioomba.
Lakini kikubwa kuliko yote ni kuwa hii ni biashara, kufunga makamera na mitambo ya kurusha live matangazo ni gharama sana kwahiyo wao wanaangalia pia biashara yao
 
Tunaweza kulalamika hapa bila kujua pengine wao ndio walioonekana bora kuliko wengine,
pengine wao ndio pekee walioomba.
Lakini kikubwa kuliko yote ni kuwa hii ni biashara, kufunga makamera na mitambo ya kurusha live matangazo ni gharama sana kwahiyo wao wanaangalia pia biashara yao

Hapana mkuu....Waliomba ITV,Star TV na TBC1.........Hata kama ni biashara,sababu wanayoitoa Star TV si gharama za makamera mengi....Wao wanasema kwamba gari lao la matangazo(OB Van)haliwezi kufika(let say Morogoro) kwa wakati.....Hii ina maana hawakujiandaa kuonesha mechi hizi kwa Tanzania nzima bali walijiandaa kuonesha mechi zitakazochezwa Mwanza tu(kama Simba wasingeenda Mwanza ina wangeonesha mechi za Toto Africans tu).....Huu ni ubabaishaji babaake
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom