Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 116,496
- 215,349
Hii ni kwa sababu kipindi wanachopitia raia wake kwa sasa ni cha dhiki kubwa mno , ukichunguza utagundua kwamba Ni vigumu kwa raia wa Tanzania kwa sasa kupata milo mitatu , wengi wanapata mlo mmoja tu , tena saa 10 jioni , na baada ya mlo huo duni , ambao unaweza kuwa mihogo na Chachandu hawali tena hadi siku inayofuata .
Kuendelea kujidanganya kwamba nchi yetu imekuwa kiuchumi huku raia wake wakinuka uvundo wa dhiki ni sawa na kujipiga kitanzi wenyewe , wekeni wazi hali halisi ili Dunia ielewe na iweze kuwasaidia hata viroba vya mtama na uwele ili raia wanusurike .
Nafuu kidogo iko kwa wafanyakazi , ambao hata wenyewe wanateseka kutokana na kutokuongezwa mshahara wala marupurupu yoyote kwa miaka 7 sasa , huku wengi wao wakihamishiwa Dodoma na familia zao zikibaki DSM au kwingine kokote walikokuwa kabla ya uhamisho huo, kwa hiyo mshahara ule ule ambao haukuongezwa hata senti tano sasa unagawanywa mara 2 kwa matumizi , aliyeko Dodoma apate na waliobaki alikokuwa awali nao wapate , Ikumbukwe kwamba Wafanyakazi wa serikali ya Tanzania hawazidi laki 6 , kati ya wananchi wake ambao idadi yao ni zaidi ya mil 60 .
Mficha maradhi mauti humuumbua
Kuendelea kujidanganya kwamba nchi yetu imekuwa kiuchumi huku raia wake wakinuka uvundo wa dhiki ni sawa na kujipiga kitanzi wenyewe , wekeni wazi hali halisi ili Dunia ielewe na iweze kuwasaidia hata viroba vya mtama na uwele ili raia wanusurike .
Nafuu kidogo iko kwa wafanyakazi , ambao hata wenyewe wanateseka kutokana na kutokuongezwa mshahara wala marupurupu yoyote kwa miaka 7 sasa , huku wengi wao wakihamishiwa Dodoma na familia zao zikibaki DSM au kwingine kokote walikokuwa kabla ya uhamisho huo, kwa hiyo mshahara ule ule ambao haukuongezwa hata senti tano sasa unagawanywa mara 2 kwa matumizi , aliyeko Dodoma apate na waliobaki alikokuwa awali nao wapate , Ikumbukwe kwamba Wafanyakazi wa serikali ya Tanzania hawazidi laki 6 , kati ya wananchi wake ambao idadi yao ni zaidi ya mil 60 .
Mficha maradhi mauti humuumbua