Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Mmoja wa mawaziri wa muda mrefu hapa nchini Profesa Kapuya hayumo kwenye baraza la mawaziri na maswali ninayojiuliza ni uswahiba wake na Manji ndiyo umemgharimu..................Ni katika himaya ya Kapuya ambapo mwekezaji wa ndani Bw. Manji ameweza kufanya dili kubwa na NSSF na hivyo kujiongozea kipato chake kwenye mazingira tatanishi...................Je yawezekana hii ndiyo sababu JK na Pinda wake wakam'mwaga?
Au ni jinsi alivyoshughulikia migogoro ya wavuja jasho na kuacha taifa lina mpasuko mkubwa kati ya TUCTA na serikali ndivyo vimemponza mwanasiasa huyu mkongwe?
Lakini kule kwenye jimbo lake yamekuwepo malalamiko ya kuwajibu hovyo wapigakura kwa maswali mazito juu ya utendaji wa serikali na kauli zake za majibu ambazo hazikuwa zinalingana na umri wake au hata nyadhifa alizowahi kuzishika serikalini..........Je huenda nazo pia zimechangia au la.......................kama zipo sababu nyingine tuzichambue................
Au ni jinsi alivyoshughulikia migogoro ya wavuja jasho na kuacha taifa lina mpasuko mkubwa kati ya TUCTA na serikali ndivyo vimemponza mwanasiasa huyu mkongwe?
Lakini kule kwenye jimbo lake yamekuwepo malalamiko ya kuwajibu hovyo wapigakura kwa maswali mazito juu ya utendaji wa serikali na kauli zake za majibu ambazo hazikuwa zinalingana na umri wake au hata nyadhifa alizowahi kuzishika serikalini..........Je huenda nazo pia zimechangia au la.......................kama zipo sababu nyingine tuzichambue................