Ihavagakwetu
Member
- Jul 26, 2019
- 5
- 6
Hong eraa sana ndugu mimi huwa najiuliza hivi ni lini watanzania wataonyesha na kuutumia utu wa na elimu? Yaani utakuta mtu na utu wake na Elimu yake anachoma nyumba ingawaje na yeye yu ndani ya nyumba hiyo.Siyo kila ukweli lazima uuanike kwa majirani. Siku zote mwenye hekima huficha aibu yake.
Hata kwenye ndoa zetu, tunapishana, lkn kwa mwenye hekima hutamuona akikimbizana na mkewe ili ampe kichapo eti kwa kuwa yeye huwa hafichi makosa na hataki unafiki. Utakuwa wa ajabu sana, maana hata nyumbani mkigombana na mkeo wakija wageni mnasema poo, ugonvi unasitishwa na hata kama mlinuna mnaahirisha, ili wageni wasigundue kitu, na hiyo si unafiki, bali ni hekima.
Aksante.