Ni upi mchango wa azam katika ukuaji wa uchumi wa tanzania?

Fpam

JF-Expert Member
Apr 28, 2011
290
115
Habari ya kwenu wanajukwaa

Naamini kila mtu pasipo na shaka anatambua na Azamu alivyotapanya biashara zake hapa nchini na nchi za jirani hasa zile zinazohusiana na vyakula na chamsingi zaidi kwa biashara hizo zinagusa moja kwa moja maisha ya watu na hivyo zinatumika sana.

Hivi karibuni TRA wametoa orodha ya makampuni yanayolipa kodi (10 best) lakini cha kushangaza kampuni ya AZAM haijatokea hicho ni kitu cha kushangaza kiasi kwamba hata baadhi ya hotel zinatoa kodi kuliko AZAM.

Mategemeo yangu ilikuwa nikiona AZAM ikiwa namba za juu kabisa kwa naman ilivyo monopolize biashara hiyo, katika nchi nyingine makampuni makubwa ndiyo yanayosaidia kuendesha uchumi na kuendesha serikali kupitia kodi, mfano SUMSUNG inachangia 20% ya budget ya South Korea kupitia kodi inazotoa. ikumbukwe tu kuwa AZAM inaathiri sana biashara nchini hasa kuzinyima Small and Medium Enterprises kuanzisha biashara na kushindana katika quality na price na AZAM.

Hizi SME's zingeweza kutoa kodi na ajira nyingi sana hasa katika kipindi hiki ambacho vijana wengi wapo mtaani bila kazi. serikali imekuwa ikihimiza vijana kuanzisha vikundi vidogo vidogo na kufungua biashara je hivyo vikundi vitaweza kushindana na hawa AZAM na makampuni makubwa ambayo yanafaidika na kukwepa kodi? tulitegemea haya makampuni yacompliment kupitia kodi sasa ni umuhimu wa AZAM?

Nakaribisha michango yenu
 
Nchi zingine wanasema "LIPA KODI UJENGE TAIFA LAKO".
Tanzania tunasema.."LIPA KODI UEPUKANE NA USUMBUFU"

Unategemea nini kamaishu ni Kuepukana na Usumbufu!...Mtu anaweza akafanya option nyingine ambayo si kulipa kodi ili Kuepukana na Usumbufu!...Ni rahisi tu!...Ukimjengea nyumba ya Mil 200 Bwana Kiti*lya, kwanini ulipe kodi ya Mil 700? serikalini?
 
Maswali ya kujiuliza ni kwamba Je AZAM wanaingiza shilingi ngapi kwa mwaka? na kodi inayotakiwa kulipwa ni shilingi ngapi kwa mwaka? Na amekwepa shilingi ngapi? hapo unaweza ukaanza kuijadili vinginevyo ni kupoteza muda
 
Pia kuna suala la kusajili kampuni ndogo ndogo ndani ya kampuni kubwa ya Bakhresa, kwa hiyo ulipaji kodi kila kampuni ndogo inalipa kivyake sio kama kampuni moja
 
Nchi zingine wanasema "LIPA KODI UJENGE TAIFA LAKO".
Tanzania tunasema.."LIPA KODI UEPUKANE NA USUMBUFU"

Unategemea nini kamaishu ni Kuepukana na Usumbufu!...Mtu anaweza akafanya option nyingine ambayo si kulipa kodi ili Kuepukana na Usumbufu!...Ni rahisi tu!...Ukimjengea nyumba ya Mil 200 Bwana Kiti*lya, kwanini ulipe kodi ya Mil 700? serikalini?
Kwa hiyo takrima kwa mkuu inahusika sana
nashukuru mkuu
 
Back
Top Bottom