iNine9
JF-Expert Member
- Mar 1, 2017
- 4,230
- 7,814
Pole sana mkuu..Dah sitaki hata kukumbuka hilo tulio ila nililipa kwa kumpa kilema cha maisha
Kuna jambo miaka kadhaa imepita nilisingiziwa na mke wa baba yangu mdogo, aisee bamdogo yule anilipiga sana kama vile anapiga jambazi sugu lililoisumbua serikali miaka mingi (bamdogo ni inspector jeshi la polisi moja ya jiji hapa nchini). Nilipata kipigo ambacho sitakuja kusahau maisha yangu yote ni Mungu alinitetea make nadhani angekuaga na mguu wa kuku ndichi angenipoteza kwenye uso wa dunia..
Ninavyosema Mungu alinitetea na alikua upande wangu ni kwamba baada ya kipigo cha umbwa koko kitu nilichosingiziwa na yule shetani mwanamke wa kichaga kwamba nimekichukua bamdogo alikuja kukiona kipo ndani chumbani mwake kwenye moja ya library zake za picha daah aliona aibu na mkewe. Ila niliapa mbele yake mimi na yeye undugu ufe tu hakuna hasara atakayopata wala mimi sipati hasara, navyoandika hapa tuna miaka 7-8 hatuna ukaribu wa aina yoyote ile na huyo jamaa wala kizazi chake..
Alinidharirisha sana mbele ya jamii inayonizunguka mpaka utupu wangu ulikua kama maonesho kwa wananzengo kwa maneno ya kuambiwa na yule mkewe bila kufanya uchunguzi wa kina kwanza kabla ya kunipa adhabu. Pia nakumbuka aliwahi toa kauli chafu kwamba mimi ntakuja kua jambazi ambae ni most wanted na jeshi lake na sitafaulu shule ngazi zote asilani. Vyote Mungu alitengua na navyoskia yule jamaa kila matokeo yalipokua yakitoka ya academic alikua anaulizia akiambiwa nimefaulu basi aibu inamjaa tu.
Bladfakeni kabisa popote ulipo.