Ni unafiki mkubwa wabunge wa CCM kumbana Waziri wa Sheria na katiba Prof Kabudi kuhusu Katiba Mpya

Hivi punde

JF-Expert Member
Apr 1, 2017
2,554
8,552
Unafiki unaendelea kututafuna sisi waTanzania.Wabunge wa CCM ndiyo wenye dola, wakisema NDIYO imepita hiyo. Mchakato wa kuipata Katiba Mpya ya Wananchi umetugharimu fedha nyingi sana za sisi walalahoi tunaolipa kodi kila kitu tunachonunua.

Na waliochangia Katiba Mpya kuyumba n wanachama na wabunge wa CCM.Kila kitu wakawa wanasema ndiyo.

Sasa hivi wanajidai et kuidai Katiba Mpya.Nimemsikia Mbunge wa Bahi CCM Mh Badwel et anaidai Katiba Mpya.Mlikuwa wapi kipindi kile imefinyangwa?

Mnampa Rais majaribu sana.Juzi tu hapa, Waziri wetu wa Sheria na Katiba ameapishwa Ikulu ya Dsm, leo hii wabunge wanakomaa kumuuliza maswala ambayo wao walishindwa kuyabeba kipindi cha nyuma.Afanyeje sasa?Tuache ushabiki.

Bahi kuna matatizo mengi sana ya wagogo.Nakushauri Mh Badwel ujikite kutetea kura zako Bahi na si kuanza kumshambulia Waziri mgeni,au kwa vile nae n mgogo mwenzio?
 
Unafiki unaendelea kututafuna sisi waTanzania.Wabunge wa CCM ndiyo wenye dola, wakisema NDIYO imepita hiyo. Mchakato wa kuipata Katiba Mpya ya Wananchi umetugharimu fedha nyingi sana za sisi walalahoi tunaolipa kodi kila kitu tunachonunua.

Na waliochangia Katiba Mpya kuyumba n wanachama na wabunge wa CCM.Kila kitu wakawa wanasema ndiyo.

Sasa hivi wanajidai et kuidai Katiba Mpya.Nimemsikia Mbunge wa Bahi CCM Mh Badwel et anaidai Katiba Mpya.Mlikuwa wapi kipindi kile imefinyangwa?

Mnampa Rais majaribu sana.Juzi tu hapa, Waziri wetu wa Sheria na Katiba ameapishwa Ikulu ya Dsm, leo hii wabunge wanakomaa kumuuliza maswala ambayo wao walishindwa kuyabeba kipindi cha nyuma.Afanyeje sasa?Tuache ushabiki.

Bahi kuna matatizo mengi sana ya wagogo.Nakushauri Mh Badwel ujikite kutetea kura zako Bahi na si kuanza kumshambulia Waziri mgeni,au kwa vile nae n mgogo mwenzio?

Napendekeza Mh Palamagamba Kabudi amshauri rais akubali marekebisho ya sheria ya mapendekezo ya katiba ili bunge hili liijadili na kurudisha zile ibara muhimu zilizoondolewa hasa ile ya serikali tatu, wabunge kutokuwa mawaziri nk. Kwa kuwa waziri huyu ndiye aliyeandika ile rasimu ya jaji Warioba atakuwa na nafasi nzuri ya kuitetea bungeni. Halafu iletwe tuipigie kura. Wabunge wa CCM waache unafiki na woga sasa kwani walikuwa wanawaogopa wahafidhina wa chama chao ambao sasa hawapo baada marekebisho ya katiba ya chama chao.
 
Waziri kama ni kweli kaamua kuendeleza katiba ya wananchi aendelee kufanya hivyo wananchi wataziona juhudi zake na wakwamishaji wa katiba ya wananchi nao wanaonekana kwa wananchi watavuna wanachokipanda.
 
Unafiki unaendelea kututafuna sisi waTanzania.Wabunge wa CCM ndiyo wenye dola, wakisema NDIYO imepita hiyo. Mchakato wa kuipata Katiba Mpya ya Wananchi umetugharimu fedha nyingi sana za sisi walalahoi tunaolipa kodi kila kitu tunachonunua.

Na waliochangia Katiba Mpya kuyumba n wanachama na wabunge wa CCM.Kila kitu wakawa wanasema ndiyo.

Sasa hivi wanajidai et kuidai Katiba Mpya.Nimemsikia Mbunge wa Bahi CCM Mh Badwel et anaidai Katiba Mpya.Mlikuwa wapi kipindi kile imefinyangwa?

Mnampa Rais majaribu sana.Juzi tu hapa, Waziri wetu wa Sheria na Katiba ameapishwa Ikulu ya Dsm, leo hii wabunge wanakomaa kumuuliza maswala ambayo wao walishindwa kuyabeba kipindi cha nyuma.Afanyeje sasa?Tuache ushabiki.

Bahi kuna matatizo mengi sana ya wagogo.Nakushauri Mh Badwel ujikite kutetea kura zako Bahi na si kuanza kumshambulia Waziri mgeni,au kwa vile nae n mgogo mwenzio?

Kifupi tu hiyo katiba anayoiulizia huyo mheshimiwa ni ile iliyopitishwa na CCM, sio unayoijua wewe, jukwaa la katiba wala sio aliyoshiriki Kabudi mwenyewe kuirasimu
Anataka tu tupoteze pesa nyingine huyo na ukawa watoke bungeni.
Wacha tunywe supu sie tujiandae kesho kazi
 
Katiba ipi inayozungumzwa ili original ya jaji Warioba au ili iliyochakachuliwa Samweli Sita!!!
 
Ndugu yangu, kuna tofauti ya mtazamo kati ya wana-CCM na Upinzani linapokuja suala la Katiba Mpya!!!

Upinzani wakisema Katiba Mpya wanamaanisha irudishwe rasimu ya Jaji Warioba ifanyiwe kazi!!!

Ukiwasikia CCM wanazungumza kuhusu Katiba Mpya wanamaanisha katiba ile ile ambayo waliipitisha pasipo na UKAWA!! Kwahiyo, si kwamba wanataka mchakato uanze upya bali wanataka ile katiba yao ipelekwe kwa wananchi ikapigiwe kura!!!

So, hakuna cha:
Unafiki unaendelea kututafuna sisi waTanzania.Wabunge wa CCM ndiyo wenye dola, wakisema NDIYO imepita hiyo.
Manake tayari wameshasema NDIYO kitambo!!!!!
 
Ukiwa na uelewa kidogo utafikiri n wazalendo ila ukifikiria kwa mapana utagundua n chuki wanaona donge kwa nn mtu asie mbunge wa kuchaguliwa kapewa wizara
 
Unafiki unaendelea kututafuna sisi waTanzania.Wabunge wa CCM ndiyo wenye dola, wakisema NDIYO imepita hiyo. Mchakato wa kuipata Katiba Mpya ya Wananchi umetugharimu fedha nyingi sana za sisi walalahoi tunaolipa kodi kila kitu tunachonunua.

Na waliochangia Katiba Mpya kuyumba n wanachama na wabunge wa CCM.Kila kitu wakawa wanasema ndiyo.

Sasa hivi wanajidai et kuidai Katiba Mpya.Nimemsikia Mbunge wa Bahi CCM Mh Badwel et anaidai Katiba Mpya.Mlikuwa wapi kipindi kile imefinyangwa?

Mnampa Rais majaribu sana.Juzi tu hapa, Waziri wetu wa Sheria na Katiba ameapishwa Ikulu ya Dsm, leo hii wabunge wanakomaa kumuuliza maswala ambayo wao walishindwa kuyabeba kipindi cha nyuma.Afanyeje sasa?Tuache ushabiki.

Bahi kuna matatizo mengi sana ya wagogo.Nakushauri Mh Badwel ujikite kutetea kura zako Bahi na si kuanza kumshambulia Waziri mgeni,au kwa vile nae n mgogo mwenzio?
In short hatuna Bunge. Angalia hoja zinazotolewa kuna hata moja makini ya kulete maendeleo?
 
#ng'adi lawi
umeandika vzur xana lakin hapo kweny ishu ya kwamb [HASHTAG]#wahafidhina[/HASHTAG] wa chama hawapo siyo kwer.
 
povu linawatoka nini sasa..kwan mlikua hamjui ccm ni wanafiki wakubwa? wamejaa kujipendekeza kwa serekal kisa ugali. Mungu anawaona
 
Samahani natoka nje ya mada kidogo..Huyu Badweli si yule Mbunge aliyewahi kushtakiwa kwa rushwa ? Au nachanganya majina?
 
Ni katiba ipi inayo daiwa na wabunge hawa?
Ni ile iliyo finyangwa na wao wenyewe ama ni rasumu ya Walioba?
Maana kama ni hii iliyo finyangwa sioni umhimu wa kuidai.
 
Wanataka wapige hela za bure halafu mwisho wa siku wao ndio wanaovuruga mchakato mzima.
 
Back
Top Bottom