Anko Sam
JF-Expert Member
- Jun 30, 2010
- 3,200
- 820
<br />
<br />
Wana Jf alichokisema Shyrose si jambo la Kubeza,mimi Binafsi Ni Mwana CCM JK anaendasha Nchi kwa Matukio Toka ameingia madarakani nchi yetu imekua ikiendeshwa si kwa kuangalia matatizo yanayokabili Taifa wananchi wake Jamaa huyu ametumia style ya Kutufanya busy tukijadili na Kulumbana juu ya mambo yasiyokuwa na TIJA.
Toka mwaka 2008 nitaorodhesha chini hapa Matukio ambayo kama Taifa tumetumia muda mwingi huku yeye akienda kutembea ulaya na kutupatia ahadi na kauli mbiu ambazo hazitusaidii.
2005 aliingia na MOVIE inaitwa Maisha Bora kwa Kila Mtanzania na Kuleta mabilioni ya JK.No impact to the economy and Common Wananchi.
2007/2008.Akaleta sinema inaitwa Kupambana na Rushwa na Matumizi Mabaya ya Madaraka Tukasikia EPA ambayo ilimuingiza yeye madarakani,Tukasikia kina Mramba,Kina Mgonja,Kina LIUMBA wakifunguliwa kesi mpaka leo zinaendelea na liumba yupo jela.
Tukaletewa Movie ingine RICHMOND na ili aendelee kupatta Umaarufu akamtosa waziri Mkuu wake akidai hajui RICHMOND wakati ilikuwa CABINET decission.
Tumeimba Richmond,Lowasa weeeeeeee yeye anaendelea kupeta wananchi tukasahau kuhoji mambo ya msingi ya nchi yetu tukawa Bar,Majumbani,ktk Madaldala,Mashuleni,Hospitalini,Na kila sehemu mjadala ni huo huo.
Akatutengenezea Sinema Inaitwa TINDI KALI la KUBENEA katumia Idara yake ya Usalama wakachukua Tindikali wakchakachua kamwagiwa Kubenea Nchi nzima tukahamia hiyo sinema kesi akamuuzia Lowasa tukawa busy na hilo hamna kujadili maendeleo.
2010 ukawa mwaka wa uchaguzi hapo kavuka Term ya kwanza salama kwa kutugawa kama Taifa na ndani ya Chama chake akawagawa wananchama wake wakawa Makundi yakipambana yeye anakula kuku Ikulu leo Serengeti kesho marekani.
2011,Zikaanza movie zingine BABU WA KIKOMBE loliondo,tukawa busy na babu nchi nzima hatuhoji maendeleo.
Mara Movie Ingine GAMBA limetuchukua muda Muda Mrefu tukaletewa Stering anaitwa Nape hapa nchi nzima ikawa Sinema ya magamba weeeeeeeee hatujadili maendeleo.
Ikawepo pia Muda tunajadili DOWANS ilipwe isilipwe nchi nzima mjadala ni huo hakuna kujadili maendeleo.
Mnaweza kuongezea matukio,Nchi ikageuka Nchi ya matukio na kujadili matukio kila kukicha jamaa anatengeneza tukio kumsaidia kusogeza siku bila kujali wananchi maisha yao yako vipi uchumi unahali gani.
Matokeo yake.
Leo Shilingi Inaporomoka.
Bei ya Sukari kwetu Bkb ni 2900
Chumvi aloacha Mkapa Tsh 50kifuko kidogo leo Tsh 500.
Umeme Haupatikani
Mafuta shida Tupo kumbe CCM ina share OILCOM
Bei ya Vyakula imepanda kwa asilimia 100
Uchumi wa Nchi unayumba
Dola leo 1640
Mafuta ya Taa leo 2000
Mpaka ameacha Reserve za kutosha leo hatuna Reserve hata ya kutumia miezi Mitatu.
Mkapa ameacha makusanyo ya Ndani ni bn 250 na dola ikiwa Tsh 1100 leo makusanyo ni bn 400 wakati Dola ni 1600.
Mfumuko wa Bei umeongezeka mpaka wamebadili Formula.
Wana Jf jamaa ametuendesha kisanii Tazama lack of Seriousness Mramba na Mgonja wapo mahakamani kutokana na makosa yaliyotokana na sheria mbovu ambayo inampa mamlaka waziri kusamehe kodi yoyte yule kosa ambalo leo anaweza kulifanya mkulo hatujasikia sheria hiyo ikibadilishwa.
Richmond hatuna sheria inayo simamia swala la Dharura na kutokana na makosa hayo leo tunaweza kurudia kosa lile lile.
Tazama usanii leo wameleta Mitambo ya Megawati zaidi ya 200 inatumia Mafuta kama IPTL wakati huo huo IPTL wanashindwa kuzalisha megawati 100 kwa ukosefu wa mafuna na mwaka 2008 waliweka mitambo ya Megawati 60 kule mwanza ya Mafuta wakashindwa kupeleka mafuta tukalipa Capacity charge kwa Alstrom kipindi chote cha Mkataba mpaka jamaa walipoondoka,leo Tena Aggreco kapewa Tenda hiyo hiyo apeleke Mtambo wa Mafuta mwanza sijui kipi kimebadilika leo tuweze kupeleka Mafuta hayo mwz ambapo mwanzo tulishindwa.
Sasahivi nchi inaongozwa kwa Msingi wa Majungu ole wako ugombane na Ridhwani waulize Bashe na Masauni watakueleza,leo mtoto anafanya Dili zote kuanzia kusafisha Vyoo Mpaka kusafirisha Madini,
Usipomuona Rizy ktk Dili utamuona 2nd First lady Alkhuroos Rahma kaibuka hapa mara Pale ,Kampeni za CCM zilitengwa Bilioni 6 kwa ajili ya Familia Ccm kina makamba wakawa wanapiga kelele hapa hapa Dar,chama kimekufa Nchi iko HOI jamaa anaongea Ngonjera Mara nitajenga viwanja vya Ndege,Mara Meli,Mara mnataka Ngeleja abebe Maji kwenye ndo apeleke Mtera?mara matatizo mwl Nyerere alishindwa hata mm siyawezi.
Katufanya watu wa Matukio kuanzia ktk chama mpaka serekalini 2015 ifike aondoke sana Tupo anajisifia shule za kata wazee wetu waliuza kuku,mbuzi,mazao kila kitu wao wameshindwa kuleta waalimu inaudhi basi tu.
Ongezeeni matukio mengine.Kila jambo Inaundwa tume ,ichunguze sasa wanataka kuchukua na UDA yetu .
Umemaliza kila kitu, sina cha kuongeza nasubiri nionyeshwe Taharir square ya Tanzania ikowapi nilianzishe.