Ni tukio gani umefanya la kutunza mazingira au kuokoa viumbe hai?

MIGUGO

JF-Expert Member
Dec 3, 2011
2,131
3,911
Mtaani mahali napoishi weekend huwa naokota plastic zote na kuzikusanya kwenye mifuko.

Huwa na waokoa mbwa na paka wanaopigwa mawe mtaani.

Shambani kwangu nimeweka mizinga nyuki minne na nitaongeza.

Nikimuona nyoka,kenge naondoka au nitamuamisha kwa kumfukuza aende simuui. Ambapo zamani nilikuwa ninaua tu hawa viumbe.

Nimepanda miti mingi sana mwaka huu ya matunda.

20210528_144910.jpg
 
Jokes kidogo
"Nimekamata Kuku wa jirani yangu Nimemwosha kwa maji moto saivi nimemuweka kwenye friji alale nitamuamsha kesho

Ili kupunguza kero ya kuku wachafu"
Binafsi nahakikisha matumizi ya gas asilia na umeme katika kupika kuepuka matumizi ya mkaa
 
Uzi wa maana kama huu, huwezi kuona wachangiaji. Lakin ungeandika "Afumaniwa na mke wa mtu, atembezwa uchi barabarani" ungeshangaa kungekuwa na viewers milioni. People are just stupid!
Mimi bwana nimeshiriki kupanda miti zaidi ya 100
Safi sana matukio ya upandaji miti yale ya umati wa watu mazuri sana.
 
Nimekamata Kuku wa jirani yangu Nimemwosha kwa maji moto saivi nimemuweka kwenye friji alale nitamuamsha kesho

Ili kupunguza kero ya kuku wachafu
Punguza matumizi ya friji washa usiku wakati wa kulala weka waji kwenye deep freezer hadi yagande. Asubuhi zima hamisha maji yaloganda(barafu) kwenye upande ambao haugandishi ili kusaidia kumaintain ubaridi through out the day.

Utasave umeme na kupunguza gesi ya ukaa (carbon monoxide)
 
Siachi tabia ya kutopanda miti hususani ya matunda....

Siwaui wadudu wasionifuata kuudhuru mwili wangu na watu wangu.....
 
Siachi tabia ya kutopanda miti hususani ya matunda....

Siwaui wadudu wasionifuata kuudhuru mwili wangu na watu wangu.....
Kuna documentary moja niliona jinsi gani taa za umeme tunazowasha usiku zinavyoathiri na kuua mamilioni ya aina wadudu (insects) kila siku.
 
Kuna documentary moja niliona jinsi gani taa za umeme tunazowasha usiku zinavyoathiri na kuua mamilioni ya aina wadudu (insects) kila siku.
🤣🤣
Nilikwenda maeneo fulani nikakuta WANA MAZINGIRA hawana umeme ilihali wenzao wanao......jibu wakaniambia kuwa WANATUNZA MAZINGIRA ,sikuwauliza sana kuhusu hilo...ndio leo umenipa MWANGA 🤣
 
Mimi napenda kuondoa kitu chchote vha kudhuru barabarani mfano chupa zilizovunjwa kuwakinga watoto na watu wengine zile chupa zisiwaumize
 
Punguza matumizi ya friji washa usiku wakati wa kulala weka waji kwenye deep freezer hadi yagande. Asubuhi zima hamisha maji yaloganda(barafu) kwenye upande ambao haugandishi ili kusaidia kumaintain ubaridi through out the day.

Utasave umeme na kupunguza gesi ya ukaa (carbon monoxide)
Sawaa mkuu shukran kwa elimu hii
 
Kuna kibindonkoi(siafu wakubwa) kimenipa Strike moja hataree kwa shingo leo mchana, nikakashika lakini sikukaadhibu ila nilikaachia kaende zake. Vipi hapo si niko freshi?
 
Back
Top Bottom