Ni tatizo la kisaikolojia au?

Kipeperushi

Senior Member
Aug 17, 2011
168
33
Habari zenu wanaJF.

Eti jamani hii issue kwanini inakuwaga hivi? Mwanadada akikushika makalio bwana aaaa.., yani inakuwa shwaari, lakini dume lenzio likikugusa hata ikiwa ni kwa bahati mbaya tu ee.. ee.. ee.. eeeee....!! Hii issue imemkuta jirani yangu jana, mimi naamini ilikuwa ni bahati mbaya tu (kwa jinsi ninavyo mjua jirani yangu naamini hakuwa na nia mbaya kabisa). Katika pitapita yake mitaa ya Tandika sokoni, ikawa ka-mgusa baba mmoja mtu wa makamo kiasi. Inaelekea alimgusa kunako makalio yake, na ilikuwa ni kwa sababu ya msongamano tu, kama unavyojua tena maeneo ya sokoni. Inasemekana baada ya tukio hilo jamaa alipokea matusi ya kufa mtu na kuwaacha wapitao jirani wakiwa wamepigwa butwaa bila kujua kulikoni.

Sasa jamani hata kama ni bahati mbaya ndio iwe matusi hivyo...!? Tatizo hili tuliite ni la kisaikolojia au? Maana naamini hata ingekuwa mimi japo nisingeweza kuporomosha matusi hadharani lakini mmmh...! Hebu nipe habari ndugu yangu ingekuwaje hapo kama ni wewe..? Na kama inatokea ni mdada kakushika hata kama ni kwa makusudi inakuwa pooooa...!
 
like charges repell, unlike charges attract each other. Ukishikwa makalio na mwanaume mwenzio ujue amekuona wewe ni sawa na boflo. Uko tayari jamii ikuone mtu wa aina hiyo. Tia akili mwenyewe.
 
like charges repell, unlike charges attract each other. Ukishikwa makalio na mwanaume mwenzio ujue amekuona wewe ni sawa na boflo. Uko tayari jamii ikuone mtu wa aina hiyo. Tia akili mwenyewe.[/Ila mdada akikushika..!? Sio boflo sio, au ndio mambo ya unlike charges..., asante mkuu.]
 
mmmh! tupo tofauti maana mm ht mwanamke spend anishike makalio, ili iweje tena mambo yakuchezewa makalio. ili ni suala la kisaikolojia tu, sababu wenzetu wazungu wanapongezana kwa kupigana kwenye makalio kwani tunashuhudia tunapoangalia mipira ya ulaya.

lkn ikiwa ni kwa bahati mbaya kwenye msongamano hapo sioni tabu na nafikiri km mtu ni muelewa awezi kureact negatively, unless otherwise!
 
Nadhani haya ni matokeo ya watu wengi kuwa na mawazo ya kingono ngono muda wao wote. Vingine sioni sababu ya kuwa na wazo la aina hiyo kila uguswapo bila hata kujali mazingira yaliyopelekea kuguswa kwako.
 
Makalio meng ya wanaume n makubwa ktokana na vyakula tofaut na wazungu. Kwa hiyo mtu anajhisi..
 
Teh teh teh!
Hebu msituchanganyie habari bana,watu tuko busy na uchaguzi igunga nyie mnaleta habari za boflo hapa!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom