Kipeperushi
Senior Member
- Aug 17, 2011
- 168
- 33
Habari zenu wanaJF.
Eti jamani hii issue kwanini inakuwaga hivi? Mwanadada akikushika makalio bwana aaaa.., yani inakuwa shwaari, lakini dume lenzio likikugusa hata ikiwa ni kwa bahati mbaya tu ee.. ee.. ee.. eeeee....!! Hii issue imemkuta jirani yangu jana, mimi naamini ilikuwa ni bahati mbaya tu (kwa jinsi ninavyo mjua jirani yangu naamini hakuwa na nia mbaya kabisa). Katika pitapita yake mitaa ya Tandika sokoni, ikawa ka-mgusa baba mmoja mtu wa makamo kiasi. Inaelekea alimgusa kunako makalio yake, na ilikuwa ni kwa sababu ya msongamano tu, kama unavyojua tena maeneo ya sokoni. Inasemekana baada ya tukio hilo jamaa alipokea matusi ya kufa mtu na kuwaacha wapitao jirani wakiwa wamepigwa butwaa bila kujua kulikoni.
Sasa jamani hata kama ni bahati mbaya ndio iwe matusi hivyo...!? Tatizo hili tuliite ni la kisaikolojia au? Maana naamini hata ingekuwa mimi japo nisingeweza kuporomosha matusi hadharani lakini mmmh...! Hebu nipe habari ndugu yangu ingekuwaje hapo kama ni wewe..? Na kama inatokea ni mdada kakushika hata kama ni kwa makusudi inakuwa pooooa...!
Eti jamani hii issue kwanini inakuwaga hivi? Mwanadada akikushika makalio bwana aaaa.., yani inakuwa shwaari, lakini dume lenzio likikugusa hata ikiwa ni kwa bahati mbaya tu ee.. ee.. ee.. eeeee....!! Hii issue imemkuta jirani yangu jana, mimi naamini ilikuwa ni bahati mbaya tu (kwa jinsi ninavyo mjua jirani yangu naamini hakuwa na nia mbaya kabisa). Katika pitapita yake mitaa ya Tandika sokoni, ikawa ka-mgusa baba mmoja mtu wa makamo kiasi. Inaelekea alimgusa kunako makalio yake, na ilikuwa ni kwa sababu ya msongamano tu, kama unavyojua tena maeneo ya sokoni. Inasemekana baada ya tukio hilo jamaa alipokea matusi ya kufa mtu na kuwaacha wapitao jirani wakiwa wamepigwa butwaa bila kujua kulikoni.
Sasa jamani hata kama ni bahati mbaya ndio iwe matusi hivyo...!? Tatizo hili tuliite ni la kisaikolojia au? Maana naamini hata ingekuwa mimi japo nisingeweza kuporomosha matusi hadharani lakini mmmh...! Hebu nipe habari ndugu yangu ingekuwaje hapo kama ni wewe..? Na kama inatokea ni mdada kakushika hata kama ni kwa makusudi inakuwa pooooa...!