Rufiji dam
JF-Expert Member
- Feb 20, 2020
- 3,803
- 8,794
Hivi uwa mnawaza nini kusifia ujuha kwani Magufuli alikuwa SAU ama.Hii ni moja ya sababu iliyonifanya niipende Serikali ya Awamu ya Sita! Hawana kelele sana wala propaganda ni vitendo tu na matokeo yanaonekana.
Baada ya Serikali iliyopita kudharau Sera ya Mambo ya nje jambo lililopelekea Tanzania kutofaidika na Sera Bora ya Mambo ya Nje, Sasa Mabadiliko ya Sera ya Mambo ya Nje tunaanza kuona yanaanza kuzaa matunda.
Kufuata miongozo ya kimataifa juu ya Corona na kuzingatia upya mahusiano bora na mataifa mengine kunaanza tena kuifaidisha Tanzania Kiuchumi.
Leo Shirika la Ndege la Kimataifa la Uswisi limeanzisha Safari zake kuja Tanzania! Na kwa Leo tu wameshusha watalii 270 Uwanja wa ndege wa kia
Kwa msiojua kila Mtalii anapotua tu hapa Tanzania analipia dola 100 kama gharama ya visa. Hapo hujalala hotelini ambapo TRA wanaingiza Tourist tax, Hapo hajaenda mbugani ambapo analipia pia kama dola 100 kwa kuingia tu mbugani. Fedha zote hizi zinaenda kumuhudumia Mtanzania Kwa kumpatia Maendeleo.
Kusema kweli sina budi kumpenda Mama Samia! Ndo mana thamani ya Shilingi ya Tanzania inazidi kuimarika dhidi ya dola ya Marekani. Hongera Kwa Mabadiliko ya Kisera yanayozidi kulinufaisha TaifaView attachment 1969580View attachment 1969581View attachment 1969582