Ni taifa gani kati ya haya ambalo limekuwa na mchango mkubwa zaidi Duniani katika maendeleo ya Sayansi na Teknolojia kwa muda wote na kwanini?

FRANC THE GREAT

JF-Expert Member
May 27, 2016
5,416
7,828
Habari!

Taifa ni watu na tunapozungumzia mchango wa taifa katika maendeleo ya Sayansi na Teknolojia tunamaanisha jitihada za watu katika taifa husika katika kulitekeleza hilo.

Katika historia kuna watu wengi maarufu kutokana na vipaji pamoja na maarifa waliyokuwa nayo hapo zamani yaliyokuwa chanzo kikubwa cha mabadiliko mbalimbali ya kimaisha katika dunia yetu ambao wengi huyaita 'maendeleo'.

Watu kama vile Isaac Newton, Albert Einstein, Galileo Galilei, Aristotle, Leonardo da Vinci, Johannes Kepler, Marie Curie, Michael Faraday, Archimedes, Nikola Tesla, Alexander Graham Bell, Thomas Edison, James Watt ni baadhi tu.

Kuna mataifa mengi ambayo kwa umoja wake yamechangia katika maendeleo ya Sayansi na Teknolojia lakini kwa sasa tuzungumzie mataifa haya manne ya barani Ulaya yenye historia ndefu sana.

1) BRITAIN (Uingereza)
2) FRANCE (Ufaransa)
3) GERMANY (Ujerumani)
4) ITALY (Italia)

Kwa maoni yako, ni taifa lipi kati ya hayo ambalo kwa muda wote limekuwa na mchango mkubwa katika maendeleo ya Kisayansi na Teknolojia tuzitumiazo hivi sasa na kwa sababu zipi?


Karibu!
 
• WAGIRIKI / WAYUNANI

√ Elimu hasa ya darasani kwa dunia hii na Mifumo yake tangu utotoni mpaka Uzeeni (Elementary Education) kuhusu Saikolojia ya Binadamu, Falsafa ya ndani kabisa, na Matibabu

• WAISRAEL

√ Kilimo, Ubunifu na Ugunduzi wa Viwanda mbalimbali vikubwa duniani kote pamoja na silaha za kivita

• WALATINI YAANI WARUMI na nchi zake hasa ITALY, SPAIN & FRANCE

√ Uendelezaji na Uekezaji wa Elimu ya Wagiriki wa kale (Ancient Greeks) pamoja na Mapinduzi ya Uhandisi wa Majengo, hasa Makanisa, Shule, Barabara, Madaraja na Nyumba Imara na bora za kuishi

• WAMISRI WA KALE /ANCIENT EGYPTIANS

√ Uhandisi wa makaburi ya mapiramidi ya kudumu, Matibabu na Utawala


• WACHINA WA KALE / ANCIENT CHINESE

√ Matibabu na Madawa


• WAINGEREZA YAANI GREAT BRITAIN (GB) & OTHER GERMANIC NATIONS KAMA GERMANY YENYEWE

√ Kwa Modern world Baadae around karne ya 16 mpaka leo hii hawa wali take Over, wakaasisi Mapinduzi ya Viwanda vikubwa sana na Ugunduzi wa Umeme. Viwanda vya Magari, Meli, Treni, Vifaa vya Umeme, Drillers, Millers na Uongozi bora pamoja na Sheria hasa ile Magna Carta

• USA, JAPAN, KOREA, RUSSIA & TURKEY

√ Waliendeleza zaidi walichoanzisha Waisrael, Waingereza na Wajerumani ila USA na RUSSIA wakaenda mbali zaidi kugundua usafiri wa Anga (Aircrafts), Internet na Silaha kali za kivita


• ISRAEL, HOLLAND

√ Kilimo cha kisasa na Ufugaji

Ahsante kubwa zaidi kwa Waingereza na Wamarekani kwani Sayansi, Elimu, Utawala, Sheria na teknolojia yao ndio tunayoiishi hata sasa, ambapo China na India nazo zinasambaza.

.........XXX.........XXX.........XXX.........XXX......
 
• WAGIRIKI / WAYUNANI

√ Elimu hasa ya darasani kwa dunia hii na Mifumo yake tangu utotoni mpaka Uzeeni (Elementary Education) kuhusu Saikolojia ya Binadamu, Falsafa ya ndani kabisa, na Matibabu

• WAISRAEL

√ Kilimo, Ubunifu na Ugunduzi wa Viwanda mbalimbali vikubwa duniani kote pamoja na silaha za kivita

• WALATINI YAANI WARUMI na nchi zake hasa ITALY, SPAIN & FRANCE

√ Uendelezaji na Uekezaji wa Elimu ya Wagiriki wa kale (Ancient Greeks) pamoja na Mapinduzi ya Uhandisi wa Majengo, hasa Makanisa, Shule, Barabara, Madaraja na Nyumba Imara na bora za kuishi

• WAMISRI WA KALE /ANCIENT EGYPTIANS

√ Uhandisi wa makaburi ya mapiramidi ya kudumu, Matibabu na Utawala


• WACHINA WA KALE / ANCIENT CHINESE

√ Matibabu na Madawa


• WAINGEREZA YAANI GREAT BRITAIN (GB) & OTHER GERMANIC NATIONS KAMA GERMANY YENYEWE

√ Kwa Modern world Baadae around karne ya 16 mpaka leo hii hawa wali take Over, wakaasisi Mapinduzi ya Viwanda vikubwa sana na Ugunduzi wa Umeme. Viwanda vya Magari, Meli, Treni, Vifaa vya Umeme, Drillers, Millers na Uongozi bora pamoja na Sheria hasa ile Magna Carta

• USA, JAPAN, KOREA, RUSSIA & TURKEY

√ Waliendeleza zaidi walichoanzisha Waisrael, Waingereza na Wajerumani ila USA na RUSSIA wakaenda zaidi kugundua usafiri wa Anga (Aircrafts), Internet na Silaha kali za kivita


• ISRAEL, HOLLAND

√ Kilimo cha kisasa na Ufugaji

Ahsante kubwa zaidi kwa Waingereza na Wamarekani kwani Sayansi, Elimu, Utawala, Sheria na teknolojia yao ndio tunayoiishi hata sasa, ambapo China na India nazo zinasambaza.

.........XXX.........XXX.........XXX.........XXX......
Mkuu umeshusha vitu, safi. Yaani Africa tumeingiza Egypt tu? Hakuna weusi?
 
1) BRITAIN (Uingereza)
Huyu mtu mwingereza hakuwa wa kawaida; hata akina Einstein walimu-amidre kwa kiwango kikubwa sana
Ukimwangalia vizuri mtu huyu, unaona kabisa kuwa pengine Mwingereza alikuwa na haki ya kuutawala ulimwengu na ndiyo maana alifanya hivyo; haikuwa kwa bahati mbaya.

 
Back
Top Bottom