BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,825
- 287,847
Swala linatumika sana Tanganyika ingawaje siku za karibuni nimeona matumizi ya suala badala ya swala yakiongezeka sana Bara. Wenzetu wa visiwani wanatumia suala.
Kuna maneno mengi yana tofauti kati ya kiswahili cha Tanganyika na kiswahili cha visiwani. Kwa mfano wenzetu wanatumia marikiti sisi tunaita soko, wao wanatumia skuli sisi tunaita shule, wao wanatumia buku sisi tunaita kitabu.
Je, katika maneno haya mawili suala na swala lipi ni sahihi? Je tunasema nataka kuuliza swali au suali?
Kuna maneno mengi yana tofauti kati ya kiswahili cha Tanganyika na kiswahili cha visiwani. Kwa mfano wenzetu wanatumia marikiti sisi tunaita soko, wao wanatumia skuli sisi tunaita shule, wao wanatumia buku sisi tunaita kitabu.
Je, katika maneno haya mawili suala na swala lipi ni sahihi? Je tunasema nataka kuuliza swali au suali?