Ni sheria ipi ilifuta fao la kujitoa?

Nssf wanatoa nina rafiki yangu amechukua mwezi mmoja uliopita
Kama nssf wanatoa basi ni kwa upendeleo mimi nimezungushwa mwaka mzima na last week wamenitolea nje eti sababu nilisitisha mkataba... Siupendi huu mfuko ni kalenda kila siku
 
"Waheshimiwa wabunge, huu mchakato ulianza muda mrefu na hata hapa bungeni sheria iliwahi kuletwa… sheria ilishatungwa. Na mpaka sasa tunapozungumza sheria ya mwisho kabisa iliyopitishwa na Bunge hili inakataza fao la kujitoa," Dk. Tulia alisema.

"Kwa hiyo, mchakato maana yake ni mazungumzo sasa ya kuangalia namna ya kubadilisha tulikotoka, lakini sheria iliyopo mpaka ninapozungumza inakataza fao la kujitoa."

Dk. Tulia aliongeza kuwa mifuko ya hifadhi za jamii imeweka utaratibu wa ziada ukiacha yale mafao ambayo yako kisheria.
Alisema utaratibu huo unaipa mifuko huo fursa ya kuamua kujitengenezea utaratibu, lakini sheria iliyopitishwa na bunge inakataza fao la kujitoa.


Hivi kuna sheria kweli inayokataza fao la kujitoa MOJA KWA MOJA? Ama mwandishi kamnukuu vibaya Naibu Spika? Sababu Bwana Kilambimkwidu ameelezea vema kule mwanzo kuwa mifuko kama NSSF iliachana na fao la kujitoa kwenye sheria yake baada ya kuona kuna loop-hole ya kutokulazimishwa na sheria mama kuwepo kwa fao la kujitoa.

Kwa ujumla "The Social Security Laws (Amendments) Act, 2012 (Act No. 5/2012)" - haizungumzii kabisa mambo ya withdrawal benefits.
 
Kama wanaondoa fao la kujitoa basi wawarudishie watumishi kodi yao waliolipa kipindi cha utumishi wao. .....kwa mfumo wa sasa mtu anaweza kulipa kodi kubwa zaidi ya makato anayopeleka kwa ajili ya mafao ya uzeeni
 
Kama wanaondoa fao la kujitoa basi wawarudishie watumishi kodi yao waliolipa kipindi cha utumishi wao. .....kwa mfumo wa sasa mtu anaweza kulipa kodi kubwa zaidi ya makato anayopeleka kwa ajili ya mafao ya uzeeni

Kama wanaondoa hilo fao sababu ya ukata wa serikali basi hawawezi kuwarudishia watumishi kodi waliyolipa kipindi cha utumishi wao. Unaona kabisa kuwa ni dhuluma ya makusudi. Sidhani kama nitakuja kuipenda CCM hata kwa dakika moja.
 
Ni uhuni tu. Eti kila mfuko una taratibu zake! Sasa maana yake nini? Yaani nchi moja halafu raia wake wanakuwa treated tofauti. Ukiwatakari sana hawa watu unaweza kupata kichaa. Mathalani, mtu aliyepoteza ajira kwa kufukuzwa hapewi mafao yake anaambiwa eti mpaka afikishe umri wa miaka 55 au 60, kwamba ukipoteza ajira ukiwa bado na umri mdogo, uwezekano wa kupata ajira nyingine ni mkubwa. Wakati huo huo, mtu aliyepoteza ajira kwa redundancy, yeye anapewa mafao yake, zingatia mtu huyo anayepewa mafao na aliyepoteza ajira kwa redundancy ni mtu ambaye umri wake ni sawa kabisa na yule aliyefukuzwa kazi. Sasa huu kama si uwendawazimu ni nini? Halafu kwa nini hii sheria haiwagusi watumishi wa umma kama vile wabunge? Unajua haya mambo tukiwa kama makondoo tutaangamizwa na hawa wanaojidai kuwa watetezi wa wanyonge! Jamani tupaze sauti, haiwezekani uzuie hela zangu wakati hujui maiisha yangu yapoje. Completely uhuni ambao haitakiwi tukaukubali, na nina amini kuna mazingira ya kuigomea sheria pale inapoonekana sheria hiyo si rafiki. Tuamke Watanzania.
 
tusilalamike sana...sisi wanasheria wetu wanajua tu kutafsiri maana ya neno jpm...lkn linapokuja suala lenye maslahi kwa umma...wanakaa kimya au wanpiga kelele halafu wakipewa pesa tu fresh wanaacha kelele
 
Mabadiliko ya sheria za Hifadhi ya Jamii (Social Security Laws Amendment), 2012 yaliondoa kipengele cha uwepo wa fao la kujitoa kwenye sheria ya kila mfuko (maana kila mfuko wa pensheni unayo sheria yake inayotaja mafao yanayotolewa na mfuko husika).

Hivo bas, wabunge walipitisha mabadiliko yale na hivyo automatically vipengele vilivyokua vinataja FAO LA KUJITOA (withdraw) viliondolewa.

Nasikitika kusema kwamba inawezekana kabisa kwamba mabadiliko yalipitishwa bila kujua haswa ni KITU KIPI HASA KINABADILISHWA na matokeo yake wakajikuta wame -repeal vifungu vilivyokua vinasema " mafao yanayotolewa na mfuko chini ya sheria hii ni......(FUTA -Withdraw)

Haikutungwa sheria kama sheria ya kusema FAO LA KUJITOA LISITOLEWE...bali kwa mabadiliko yale kurekebisha vipengele vya mafao na kutokutaja fao la kujitoa (withdraw) automatically mfuko hauwezi kulipa kwakua mfuko unalipa mafao YALIYOTAJWA TU na kila fao limewekewa utaratibu namna linavotolewa.

Sheria za mifuko yote pamoja na hao wasimamizi wa SSRA zilirekebishwa mwaka 2012 na copy ya sheria ambazo ziko embeded zinataja sheria kua ni [R.E 2015] ~maana yake ni kwamba shwria husika ni TOLEO LA 2015 (ambalo ndilo linayo hayo marekebisho ya 2012.

ONA VIELELEZO
1. Kitabu cha sheria za Hifadhi ya Jamii Toleo 2015.
8ead3388573a7af22e055aef7e13bf49.jpg


2. Sheria za mifuko mmojammoja zinajieleza (hii ni NSSF)
3ce3999e98099d69a55843c8045f6ab9.jpg


3. Mafao ya NSSF (angalia kwa hautaona WITHDRAWAL ikitajwa, iliondolewa)
280fba61dd9a9cfe4ba316c6c9967f48.jpg

Naenda Zim.
Ki ukweli ni kuwa wabunge wetu wametusaliti.
 
Halafu ukienda kufuatilia mafao wafanyakazi hasa wa Nssf wanakukata jicho baya, jicho la ugaidi, kisasi na chuki. Utasema unachukua pesa toka kwenye wallet zao
 
Kama Una Baba yako, Mama Yako, Bibi Babu, Dada Na Hata wewe Mwenyewe na Wanyonge Wote Serikali ya Awamu ya Tano Imekaribia kuleta Mkong'oto Huu Huu hapa (Kilio na kusaga Meno)

Kuna mswada unakuja na kwa Bunge letu la Wangapi wanakubali Waseme Ndiyooooo "Ndiyoooooo" waliosema ndiyo wameshinda "Utapita"

MSWADA HUO Unaenda kuua wastaafu Na sisi Tunao karibia kustafu

Ni hivi Mafao ya wastafuu yatakuwa hivi Tega sikio, utalazimika kulipwa 38% tu na 62% utakuwa unalipwa kila Mwezi (monthly) hapa ili unielewe nikupe mfano. kama ilikuwa ulipwe milioni 100 kama hela yako ya kustafia maana yake kwa mswada mpya utalipwa pension ya mkupuo 38 milioni halafu milioni 62 ulipwa kila mwezi.

Ukistafu na umri wa miaka 61 utakula hicho kiasi cha million 38 kigingine utalipwa kidogo kidogo kila mwezi

Ubaya wa hili siku ukifa tu kila kitu kimekufa malipo kila mwezi nayo yanakufa. Hivyo hela nyingi zitabaki kwenye mifuko maana rekodi inaonyesha wastaafu wengi hawaishi muda mrefu na hasa ukizingatia mafao yatapungua.

2. Mume akifa Mke na wategemezi watahudumiwa miaka 3 tu kisha huduma itakoma wakati ungepewa yote ungewaachia miradi familia wakaishi hata kama haupo

3. March 2018 mifuko itaunganishwa kubaki mifuko 2 tu. Yaani LPF, NSSF PPF sijui nani sijui nani itafungwa na kubaki mifuko miwili tu (Vibarua vinaenda kuota nyasi)

4. April 2018 sheria itaanza kutumika Yaani Mwakani Kuna kilio kikuu kwa watumishi wa mifugo na wastafuu

My Take

Kwa ufupi bila kupindisha muswada huu utaumiza watumishi wote ,Bunge Mkafanye kazi yenu, sasa Hiki ni kipimo chenu cha kudhibitisha Mpo huru na kwamba ni muhimili unajitegemea ,Wabunge wetu msipoliona hili kuwasemea watumishi basi Mtawasononesha watumishi

Yaani Ufanye kazi miaka 61 ukitumikia umma uzeeni uporwe haki itasikitisha

Alloyce Nyanda
Mtozi.
 
Kama Una Baba yako, Mama Yako, Bibi Babu, Dada Na Hata wewe Mwenyewe na Wanyonge Wote Serikali ya Awamu ya Tano Imekaribia kuleta Mkong'oto Huu Huu hapa (Kilio na kusaga Meno)

Kuna mswada unakuja na kwa Bunge letu la Wangapi wanakubali Waseme Ndiyooooo "Ndiyoooooo" waliosema ndiyo wameshinda "Utapita"

MSWADA HUO Unaenda kuua wastaafu Na sisi Tunao karibia kustafu

Ni hivi Mafao ya wastafuu yatakuwa hivi Tega sikio, utalazimika kulipwa 38% tu na 62% utakuwa unalipwa kila Mwezi (monthly) hapa ili unielewe nikupe mfano. kama ilikuwa ulipwe milioni 100 kama hela yako ya kustafia maana yake kwa mswada mpya utalipwa pension ya mkupuo 38 milioni halafu milioni 62 ulipwa kila mwezi.

Ukistafu na umri wa miaka 61 utakula hicho kiasi cha million 38 kigingine utalipwa kidogo kidogo kila mwezi

Ubaya wa hili siku ukifa tu kila kitu kimekufa malipo kila mwezi nayo yanakufa. Hivyo hela nyingi zitabaki kwenye mifuko maana rekodi inaonyesha wastaafu wengi hawaishi muda mrefu na hasa ukizingatia mafao yatapungua.

2. Mume akifa Mke na wategemezi watahudumiwa miaka 3 tu kisha huduma itakoma wakati ungepewa yote ungewaachia miradi familia wakaishi hata kama haupo

3. March 2018 mifuko itaunganishwa kubaki mifuko 2 tu. Yaani LPF, NSSF PPF sijui nani sijui nani itafungwa na kubaki mifuko miwili tu (Vibarua vinaenda kuota nyasi)

4. April 2018 sheria itaanza kutumika Yaani Mwakani Kuna kilio kikuu kwa watumishi wa mifugo na wastafuu

My Take

Kwa ufupi bila kupindisha muswada huu utaumiza watumishi wote ,Bunge Mkafanye kazi yenu, sasa Hiki ni kipimo chenu cha kudhibitisha Mpo huru na kwamba ni muhimili unajitegemea ,Wabunge wetu msipoliona hili kuwasemea watumishi basi Mtawasononesha watumishi

Yaani Ufanye kazi miaka 61 ukitumikia umma uzeeni uporwe haki itasikitisha

Alloyce Nyanda
Mtozi.
Kwa mwendo huu watumishi wengi wasioridhishwa na mazingira ya kazi watakuwa na ujasiri wa kuacha kazi kwani pensheni iliyokuwa inawabwetesha kuendelea na kazi haina maana tena.
 
JAMANI WANA JAMVI NAOMBA USHAURI KUHUSU FAO LA KUJITOA Mimi nililipwa fao lakujitoa PPF mwaka jana fao langu lilikua jumla mil,15 lkni nikalipwa mil,10 tano wakanimbia niandike barua ya punjo ili nilipwe iliyo baki nimepeleka barua mara nyingi hakuna jibu nikaingia kwa meneja anasema hiyo siwezi pata mpka ni staafu nilipwe kwa mwezi ukipiga simu custumer care wanasema niitume barua yapunjo lkni wao hajaniambia mpka nistaafu ushauri wanao jua utaratibu huu niingie office gani nipate haki yangu?
 
JAMANI WANA JAMVI NAOMBA USHAURI KUHUSU FAO LA KUJITOA Mimi nililipwa fao lakujitoa PPF mwaka jana fao langu lilikua jumla mil,15 lkni nikalipwa mil,10 tano wakanimbia niandike barua ya punjo ili nilipwe iliyo baki nimepeleka barua mara nyingi hakuna jibu nikaingia kwa meneja anasema hiyo siwezi pata mpka ni staafu nilipwe kwa mwezi ukipiga simu custumer care wanasema niitume barua yapunjo lkni wao hajaniambia mpka nistaafu ushauri wanao jua utaratibu huu niingie office gani nipate haki yangu?
Mkuu naomba maelekezo hapa, umewezaje kutoa hata hiyo 10 m wakati Fao la kujitoa limesitishwa au wameshalirudisha..??
 
Ni Kweli NSSF wanatoa kweli? mbona habari hizi zinachanganya sana maana nimesoma watu wakisema hawatoi. Ama ni mambo ya upendeleo? Kwamba wanatoa kwa watu fulani tu?
Liliwahi kufutwa 2012 na mie wakati huo nilikuwa ni muhanga ambapo John Mnyika na Selemani Jafo walitoa hoja binafsi ambapo ilipelekea tena mwaka 2012 mwezi Novemba ambapo bunge ilirudisha na ndipo tulipooanza tena kuchukua hilo fao mpaka mwanzoni wa mwaka 2018 na waliacha kulitoa mwanzoni mwa 2018 baada ya Rais kusaini sheria mpya ambapo wakaja na fao la kukosa ajira ambalo kimsingi hakuna mfumo ambao umewekwa.

Ila kwa kuwa Rais amefutilia mbali mambo ya pensheni kwa sheria hii mpya nadhani pia fao la kujitoa litakuwa limerudi automatically maana alizungumzia pia hakuna logic kwa mtu amefanya kazi miaka 4 alafu baadae umwambie achukue hela baada ya miaka 60 akatolea mfano mtu kapata kazi kwenye ujenzi wa madaraja ama kwenye migodi
 
JAMANI WANA JAMVI NAOMBA USHAURI KUHUSU FAO LA KUJITOA Mimi nililipwa fao lakujitoa PPF mwaka jana fao langu lilikua jumla mil,15 lkni nikalipwa mil,10 tano wakanimbia niandike barua ya punjo ili nilipwe iliyo baki nimepeleka barua mara nyingi hakuna jibu nikaingia kwa meneja anasema hiyo siwezi pata mpka ni staafu nilipwe kwa mwezi ukipiga simu custumer care wanasema niitume barua yapunjo lkni wao hajaniambia mpka nistaafu ushauri wanao jua utaratibu huu niingie office gani nipate haki yangu?
Mkuu nenda ofisi yyte ya psssf au waibukie ssra wakakupe mwongozo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Liliwahi kufutwa 2012 na mie wakati huo nilikuwa ni muhanga ambapo John Mnyika na Selemani Jafo walitoa hoja binafsi ambapo ilipelekea tena mwaka 2012 mwezi Novemba ambapo bunge ilirudisha na ndipo tulipooanza tena kuchukua hilo fao mpaka mwanzoni wa mwaka 2018 na waliacha kulitoa mwanzoni mwa 2018 baada ya Rais kusaini sheria mpya ambapo wakaja na fao la kukosa ajira ambalo kimsingi hakuna mfumo ambao umewekwa.

Ila kwa kuwa Rais amefutilia mbali mambo ya pensheni kwa sheria hii mpya nadhani pia fao la kujitoa litakuwa limerudi automatically maana alizungumzia pia hakuna logic kwa mtu amefanya kazi miaka 4 alafu baadae umwambie achukue hela baada ya miaka 60 akatolea mfano mtu kapata kazi kwenye ujenzi wa madaraja ama kwenye migodi

Irudi tu hii kitu
 
MH.RAISI KESHASEMA TUNARUDI KWENYE UTARATIBU WA ZAMANI HADI 2023.
HAJASEMA WAFANYAKAZI WASIPEWE FAO LA KUJITOA.
WATU WAPEWE HELA ZAO KAMA ZAMANI PAMOJA NA VIKOKOTOZI VYA ZAMANI ANAYEPINGA ATAKUWA ANAPINGANA NA MANENO YA RAISI.
 
Liliwahi kufutwa 2012 na mie wakati huo nilikuwa ni muhanga ambapo John Mnyika na Selemani Jafo walitoa hoja binafsi ambapo ilipelekea tena mwaka 2012 mwezi Novemba ambapo bunge ilirudisha na ndipo tulipooanza tena kuchukua hilo fao mpaka mwanzoni wa mwaka 2018 na waliacha kulitoa mwanzoni mwa 2018 baada ya Rais kusaini sheria mpya ambapo wakaja na fao la kukosa ajira ambalo kimsingi hakuna mfumo ambao umewekwa.

Ila kwa kuwa Rais amefutilia mbali mambo ya pensheni kwa sheria hii mpya nadhani pia fao la kujitoa litakuwa limerudi automatically maana alizungumzia pia hakuna logic kwa mtu amefanya kazi miaka 4 alafu baadae umwambie achukue hela baada ya miaka 60 akatolea mfano mtu kapata kazi kwenye ujenzi wa madaraja ama kwenye migodi

KUTOKANA NA KAULI YA RAISI NI KWELI AUTOMATICALLY FAO LA KUJITOA LIMERUDI LABDA NSSF WAMBISHIE RAISI!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom