Ni Serikali Ipi Isiyo na Jukumu la Kujenga Barabara, Hospitali na Shule?

eedoh05

JF-Expert Member
Apr 20, 2011
632
234
Kuna jambo nilisilo lielewa hasa ninapokutana na tambo kama hizi: "Tumejenga barabara...tumejenga shule...tumejenga hospitali...tumejenga vyuo vikuu nk nk" Ninajiuliza je hayo siyo majukumu ya kila serikali duniani? Kama ujenzi wa barabara katika nchi ni hisani? Je! Majukumu ya serikali ni yepi? Je, kodi inayokusanywa na serikali hiyo kazi yake ni nini? Au ni kufisidi kodi hizo?

Na iwapo ujenzi wa miundo-mbinu, hospitali,shule na vyuo sio jukumu la serikali, ni kwa nini basi kila nchi inakuwa na bunge la bajeti? Bunge hili kwa kila nchi hupanga bajeti za maendeleo na matumizi ya kawaida kwa taifa husika.

Imefika mahali unamsikia Waziri Mkuu akijinanga kwamba sisi tumejenga barabara ndefu na nyingi kuliko Burundi. Je, Burundi wana raslimali kiasi gani ni nyingi kuliko za Tanzania? Basi, ni bora Waziri Mkuu angeilinganisha serikali yake kiutendaji na zile za Botswana na Mauritius.

Serikali zote duniani hujenga miundombinu bora, hospitali na shule ili ziweze kuwa na jamii inayosonga mbele kimaendeleo.

Nawasihi wahusika wasijitokeze mbele ya watanzania na kutoa tambo kama hizo..vinginevyo watazomewa..watapopolewa mawe na kukimbiwa. Tambo kama hizo unaweza kuzisema kwa hadhira ya kukodishwa na kubebwa kwenye malori na kwenye coaster toka mji hadi mji mwingine ilkujaza watu mkutanoni.

Tatizo kubwa ni rushwa, eleza rushwa, chukua hatua kuikabili. Hapo utasikilizwa. Kwa sasa, hakuna mwananchi anayepata huduma yoyote pasipo rushwa. Imekuwa kawaida katika jamii huko vijijini na hata mijini, wanandugu wanachangishana fedha kwa ajili ya kutoa rushwa wanapokuwa wanadai haki ya mmoja wa ndugu yao akiwa anamashauri polisi, mahakamani, akitaka huduma hospitali, katika vituo vya afya, akitaka huduma kwa watendaji wa vijiji ama mitaa.

Rushwa ikianzia Ikulu usitarajie kuwa kuna mahali patakosa rushwa.Biblia inasema mfalme akiasi na kulaaniwa hadi taifa lake na watu wake huingia kwenye matatizo ya yanayotokana na laana hiyo. Aliweza kuishi bila laana hiyo, mwl. Nyerere, aliweza W/Mkuu. Moringe Sokoine. Waliweza kwa kuwa hawakupata madaraka kwa rushwa na ufisadi. CCM ya leo haina jipya, wameshika dola kwa rushwa, wanaishi kwa ufisadi kuanzia mabalozi wao wa nyumba kumi hadi wenyeviti wa jumuiya za chama; makatibu, wakuu wa wilaya, mikoa, wabunge, mawaziri, hadi huko ikulu.
 
Mbona bado hueleweki mkuu.

Hivi umeshawahi kusikia ilani ya uchaguzi, yenye kuweka kipaumbele matakwa ya wananchi?
Serikali haitekelezi majukumu yake kama ndege iliyo katika auto-pilot.
Serikali inaelekezwa nini cha kufanya.

Hilo ni somo la civics darasa la nne au tano.
 
Yoootr uliyoyataja Ni majukumu ya serikali ndo maana viongozi wanaeleza wananchi ni namna gani wametimiza majukumu yao.

Huna hoja ya msingi, kajipange kwanza.
 
Ndo matatizo ya kuwa na rais mwenye mediocre thinking..anakuwa na urguments za kitoto kama hizo za mambo ya barabara mara maji..ujinga mtupu
 
Kuna jambo nilisilo lielewa hasa ninapokutana na tambo kama hizi: "Tumejenga barabara...tumejenga shule...tumejenga hospitali...tumejenga vyuo vikuu nk nk" Ninajiuliza je hayo siyo majukumu ya kila serikali duniani? Kama ujenzi wa barabara katika nchi ni hisani? Je! Majukumu ya serikali ni yepi? Je, kodi inayokusanywa na serikali hiyo kazi yake ni nini? Au ni kufisidi kodi hizo?

Na iwapo ujenzi wa miundo-mbinu, hospitali,shule na vyuo sio jukumu la serikali, ni kwa nini basi kila nchi inakuwa na bunge la bajeti? Bunge hili kwa kila nchi hupanga bajeti za maendeleo na matumizi ya kawaida kwa taifa husika.

Imefika mahali unamsikia Waziri Mkuu akijinanga kwamba sisi tumejenga barabara ndefu na nyingi kuliko Burundi. Je, Burundi wana raslimali kiasi gani ni nyingi kuliko za Tanzania? Basi, ni bora Waziri Mkuu angeilinganisha serikali yake kiutendaji na zile za Botswana na Mauritius.

Serikali zote duniani hujenga miundombinu bora, hospitali na shule ili ziweze kuwa na jamii inayosonga mbele kimaendeleo.

Nawasihi wahusika wasijitokeze mbele ya watanzania na kutoa tambo kama hizo..vinginevyo watazomewa..watapopolewa mawe na kukimbiwa. Tambo kama hizo unaweza kuzisema kwa hadhira ya kukodishwa na kubebwa kwenye malori na kwenye coaster toka mji hadi mji mwingine ilkujaza watu mkutanoni.

Tatizo kubwa ni rushwa, eleza rushwa, chukua hatua kuikabili. Hapo utasikilizwa. Kwa sasa, hakuna mwananchi anayepata huduma yoyote pasipo rushwa. Imekuwa kawaida katika jamii huko vijijini na hata mijini, wanandugu wanachangishana fedha kwa ajili ya kutoa rushwa wanapokuwa wanadai haki ya mmoja wa ndugu yao akiwa anamashauri polisi, mahakamani, akitaka huduma hospitali, katika vituo vya afya, akitaka huduma kwa watendaji wa vijiji ama mitaa.

Rushwa ikianzia Ikulu usitarajie kuwa kuna mahali patakosa rushwa.Biblia inasema mfalme akiasi na kulaaniwa hadi taifa lake na watu wake huingia kwenye matatizo ya yanayotokana na laana hiyo. Aliweza kuishi bila laana hiyo, mwl. Nyerere, aliweza W/Mkuu. Moringe Sokoine. Waliweza kwa kuwa hawakupata madaraka kwa rushwa na ufisadi. CCM ya leo haina jipya, wameshika dola kwa rushwa, wanaishi kwa ufisadi kuanzia mabalozi wao wa nyumba kumi hadi wenyeviti wa jumuiya za chama; makatibu, wakuu wa wilaya, mikoa, wabunge, mawaziri, hadi huko ikulu.

Umeuliza swali la msingi sana. Serikali haipaswi kutamba kwa kufanya shuguli zake za msingi. Imagine shule hazina madawati wala taa viongozi wanapambana na tambo. Its disgusting.
 
Yoootr uliyoyataja Ni majukumu ya serikali ndo maana viongozi wanaeleza wananchi ni namna gani wametimiza majukumu yao.

Huna hoja ya msingi, kajipange kwanza.

Kisheria na katika somo la uraia darasa la 4, 5, na 6 watoto wanafundishwa kwamba, kusomeshwa, kununuliwa nguo, kupendwa ni miongoni mwa haki zao. Wanafundishwa kuwa mzazi kumsomesha na kumlea mtoto ni wajibu wake. Sio kuwa anafanya hisani. Kwa mujibu wa maelezo yako, naona somo la uraia linakosea kuonesha kuwa wajibu ni sawa na hisani.

Baba mpumbavu ni yule anayegeuza wajibu wake na kuufanya hisani. Labda kama baba huyo ni wa mbao, kama Pinokio.
 

Kisheria na katika somo la uraia darasa la 4, 5, na 6 watoto wanafundishwa kwamba, kusomeshwa, kununuliwa nguo, kupendwa ni miongoni mwa haki zao. Wanafundishwa kuwa mzazi kumsomesha na kumlea mtoto ni wajibu wake. Sio kuwa anafanya hisani. Kwa mujibu wa maelezo yako, naona somo la uraia linakosea kuonesha kuwa wajibu ni sawa na hisani.

Baba mpumbavu ni yule anayegeuza wajibu wake na kuufanya hisani. Labda kama baba huyo ni wa mbao, kama Pinokio.
Hata nchi zilzoendelea kama Marekani hazina uwezo unaofikiria.
Na ndio maana kunakuwepo planning ya hizo meagre resources ili kuoptimize matumizi ya kodi.
Na hapo ndio vyama vya siasa vinaingia katika kupanga na kuchagua nini cha kufanya.

Wajibu na utekelezaji ni vitu viwili tofauti sawa na mbingu na dunia.
 
Hata nchi zilzoendelea kama Marekani hazina uwezo unaofikiria.
Na ndio maana kunakuwepo planning ya hizo meagre resources ili kuoptimize matumizi ya kodi.
Na hapo ndio vyama vya siasa vinaingia katika kupanga na kuchagua nini cha kufanya.

Wajibu na utekelezaji ni vitu viwili tofauti sawa na mbingu na dunia.


Nina wasiwasi kama tunajua tunachokibishia.
 
Hata nchi zilzoendelea kama Marekani hazina uwezo unaofikiria.
Na ndio maana kunakuwepo planning ya hizo meagre resources ili kuoptimize matumizi ya kodi.
Na hapo ndio vyama vya siasa vinaingia katika kupanga na kuchagua nini cha kufanya.

Wajibu na utekelezaji ni vitu viwili tofauti sawa na mbingu na dunia.

Ni uwendawazimu kujilinganisha na marekani kila tunapotaka kutetea ujinga, ufisadi na ushetani wetu uliopea. Kama kila jambo tuangalie marekani wanafanyaje, basi jambo la kwanza kuliiga lingelikuwa ushoga.

Kwa nini hatuigi Rwanda...sababu zilizowafikisha kwenye machinjano? Kwa nini tusiige Rwanda katika kupambana na ufisadi na kupanga bajeti yao.

Nadhani ilitupasa kuiga Sweden, Finland kwa walioweza kupanga bajeti zao zikafana.

Mwaka jana, viongozi wa dini wanaripoti kwamba kwa mara ya kwanza wameshangaa wanawake wanashiriki midahalo ya kisiasa; kuonesha kukerwa kwao na mfum
o wa utawala uliopo. Hadithi za hata Kenya au Marekani iko hivyo...kutetea ubovu na uozo zilikuwa enzi hizo.
 
Ni uwendawazimu kujilinganisha na marekani kila tunapotaka kutetea ujinga, ufisadi na ushetani wetu uliopea. Kama kila jambo tuangalie marekani wanafanyaje, basi jambo la kwanza kuliiga lingelikuwa ushoga.

Kwa nini hatuigi Rwanda...sababu zilizowafikisha kwenye machinjano? Kwa nini tusiige Rwanda katika kupambana na ufisadi na kupanga bajeti yao.

Nadhani ilitupasa kuiga Sweden, Finland kwa walioweza kupanga bajeti zao zikafana.

Mwaka jana, viongozi wa dini wanaripoti kwamba kwa mara ya kwanza wameshangaa wanawake wanashiriki midahalo ya kisiasa; kuonesha kukerwa kwao na mfum
o wa utawala uliopo. Hadithi za hata Kenya au Marekani iko hivyo...kutetea ubovu na uozo zilikuwa enzi hizo.
You are a poor debator.
Mtu asiye na hazina ya uelewa daima hukimbilia matusi. Na aina ya matusi huonekana katika thinking ya mtu.

Nimetoa mfano wa marekani kama ulinganishi ya the richest nation on earth ambayo hata hiyo haina uwezo wa kutekeleza majukumu kwa raia wake WOTE.

Sasa kama ulinganishi huo unaamsha mawazo ya kishoga kwa mtu kama huyu mtoa hoja, its unfortunate indeed.

With such an uncivilised line of thought do we need to say more?
I leave the scenario for like feathers.
Cheerio.
 
Mkuu hoja hapa kwa mtazamo wangu ni kuwa mbali na kuwa ni wajibu wa serikali kubeba majukumu hayo ila ukweli ni kwamba barabara nyingi zinazojengwa sasa na mambo mengine yote ni mambo yaliyostahili kuwa yamefanywa miaka mingi iliyopita.

Ni aibu kwa serikali hii kujinadi na ujenzi wa barabara.Kibaya zaidi ni kuwa tukiwa ndani ya miaka zaidi ya hamsini ya uhuru bado tunazungumzia kujenga barabara za kuunganisha mikoa.Hii ni aibu na fedheha kwa nchi yenye rasilimali nyingi kama yetu.Na kinachotia kichefuchefu ni kuwa kuna zingine zinajengwa ktk kiwango ambacho zitakuwa bara bara za vumbi.

Kwa kifup,i tungekuwa na serikali makini, saa hizi tungekuwa tumeanza kujenga fly over,kupanua bara bara hizo za kuunganisha mikoa n.k.
 
Kazi ya Serikali yoyote duniani ni kufanikisha huduma za jamii ziwebora kwa wanainchi wote, tena siyo hiyari nilazima (hospitali, mashule, njia za usafirishaji, chakula, usalama wa raia nk). Nafikiri serikali ingejisifu kwa, Je imefanikiwa kuongeza ajira kwakiasi gani?(not wamachinga), kutafuta masoko kwa mazao ya wakulima wetu, Kufanikisha au kujenga viwanda, Kukusanya kodi kwa 100%, kulinda ajira za wazawa, kupambana na rushwa.
 
Back
Top Bottom