Ni sehemu gani maeneo ya kijijini ndani ya Tanzania uliyowahi kufika ukayafurahia maisha ya hapo?

Vinci Dayot Upamecano

JF-Expert Member
Nov 11, 2020
522
1,272
Shikamoni Shimba ya Buyenze , Mshana Jr na Bujibuji Simba Nyamaume wengine wote hamjamboni?

Tofauti kidogo na Uzi wa mtaalam Kyambamasimbi hapa tutaangalia vijiji vizuri vyenye Amani, maziwa na asali.

Katika harakati za Maisha, suala la kutembea na kubadilisha makazi iwe ni kwa muda mfupi au kwa muda mrefu ni jambo lisiloepukika. Ndomaana hata mtu mzima mpwayungu village Juzi alikuwa Rwanda keshokutwa tutamkuta USA kisha atarudi tena kijijini kwao Mpwayungu.

Binafsi kwa sehemu yoyote ntakayoazimia kwenda iwe kikazi/kibiashara, kusalimia, mapumzikoni n.k Kipaumbele changu Cha kwanza kukiangalia ni Chakula na Maji mengine naweza kuvumilia hapa watoto wa kishua kina Bill Lugano wakae kwa kutulia kwanza.

Binafsi nimeshawahi kufika vijiji mbalimbali ndani na nje ya Tanzania na kwakweli zipo baadhi ya sehemu zimebarikiwa inshallah ukifika hutamani kutoka haraka na miongoni mwa vijiji ambavyo nilishawahi kukaa na angalau nikalamba asali ni pamoja na;

Malela - Karatu - Arusha. Mnamo mwaka wa 2019 nilikwenda huko kulangua Mbaazi na Ngano, aisee kule kumebarikiwa bwana maana Kuna Chakula Cha kutosha achilia mbali watoto weupe wa kimbulu. Maziwa fresh au mtindi 1ltr nilikuwa nanunua kwa Tshs 800 wakati mayai ya kienyeji naletewa kwa 200Tshs, hali ya hewa nzuri sanaa nilirudi nyumbani nmetakata, wanawake wa kule sio wachoyo, sijui kwa wanaume lkn pia ardhi yao ina rutuba sana.

Kyomu - Moshi (v) Kilimanjaro. Kama ilivyoada nilimsindikiza rafiki yangu Ukweni, bwana wee! Jua sio kali sana, msosi sio suala maana wanafanya kilimo cha umwagiliaji hususani mbogamboga na matunda. Mayai kienyeji 200, nyanya za 500 unapikia siku tatu Maziwa unaamua unywe ndo ukamue au ukamue ndo unywe. Msosi sio shida mabinti wa kushika mkono tu tena kama ndo mgeni hupati tabu ardhi imebarikiwa Ila tu Kuna vumbi kimtindo Na watu wake ni wakarimu sana.

Mto wa Mbu (kijiji nimekisahau jina) - Monduli - Arusha. Pazuri kuanzia ardhi, Hali ya hewa, huduma za kijamii, mzunguko wa hela upo Chakula sio tabu, Watu wake wakarimu na Mabinti pia wamo si mchanganyiko wa Wairaq na masai.

Bukuru - Kondoa - Dodoma. Huku bwana nilifanya kama kupita tu lkn baadae niliamua kurudi nipaone vizuri. Kuna amani ya Hali ya juu unaweza kulala hata nje maana warangi sio watu wa hila. Chakula, Hali ya hewa, ardhi na watoto wa kirangi ndiyo haswa walinishawishi nirudi kupaona vizuri nikanunua na eneo kabisa
Vipo vijiji vitatu ambavyo sitaviorodhesha lakini vilinikosha sana pia ila tu hivyo hapo juu vilinikosha zaidi.

Je na wewe ni Kijiji gani ulichowahi kufika na kukaa kwa muda wowote ule pakakukosha kwa namna moja ama nyingine? karibuni wapenzi.
 
Wewe bado hujatembea Tanzania umetaja sehemu ambazo ni ukanda mmoja tu ambako naamini 98% ya wanajamvi tunakujua.

Kwa taarifa yako Kondoa hamna sehemu nzuri kama Haubi kisha Mnenia!
Hujazuiwa kutowa experience yako, na yeye hiyo ni experience yake.

Na Mimi napigia mstari vijiji vya uchagani vina raha yake, mandhari, vyakula na hali ya hewa.
 
Wewe bado hujatembea Tanzania umetaja sehemu ambazo ni ukanda mmoja tu ambako naamini 98% ya wanajamvi tunakujua.

Kwa taarifa yako Kondoa hamna sehemu nzuri kama Haubi kisha Mnenia!
Nimesikia sifa nyingi za haubi, natamani sana kufika huko, mnenia nimefika pia ni pazuri kwa wastani.

Leta uzoefu wako katika vijiji ulivyowahi kufika na kukakuvutia.
 
Subiri nkusanye data kwa ajili ya utalii wa ndani. Maana vijiji nlivkenda mimi vyooote sikutamani kurudi
 
Tunaomba ushuhuda wake tafadhali
images (18).jpeg
images (19).jpeg
images (23).jpeg
 
Sehemu nilpowai kufika na nimepapenda ni lushoto tu ,kuanzia ukarimu wa wenyeji, wanawake wazuri weupe, maji safi Tena ya baridi nyumba iko mlimani ila Kuna maji ,Kuna viwanja vya mpira ,hali ya hewa usiseme yaani raha kinoma matunda kibao ...siku ya jumapili Kuna soko town kule duh wacha tu!!!! Maparachichi Bei ya kutupa ,ndizi ,matunda damu, maapple

Nitarudi Tena watu wakarimu nakumbuka nilikuwa nakaa karibu na msikiti pale stendi unaitwa Irshad kama sijakosea maana nilikuwa naswali pale ...kuna waarabu Kuna uwanja wa mpira safi sema mdogo ...watu wako poa nilienda kweny msiba ya mshkaji baba ake wale wafiwa wametulia tu pale but majirani ndo wanaleta vyakula na Kuni mpaka kupika yaani pamefiwa utasema wanevuna wanaletewa kama zawadi hawajatoa gharama hata gari tulichangia...kila mtu analeta wengine wanaleta mpaka kuku.

Wasambaa shikamooni...
 
Shikamoni Shimba ya Buyenze , Mshana Jr na Bujibuji Simba Nyamaume wengine wote hamjamboni?

Tofauti kidogo na Uzi wa mtaalam Kyambamasimbi hapa tutaangalia vijiji vizuri vyenye Amani, maziwa na asali.

Katika harakati za Maisha, suala la kutembea na kubadilisha makazi iwe ni kwa muda mfupi au kwa muda mrefu ni jambo lisiloepukika. Ndomaana hata mtu mzima mpwayungu village Juzi alikuwa Rwanda keshokutwa tutamkuta USA kisha atarudi tena kijijini kwao Mpwayungu.

Binafsi kwa sehemu yoyote ntakayoazimia kwenda iwe kikazi/kibiashara, kusalimia, mapumzikoni n.k Kipaumbele changu Cha kwanza kukiangalia ni Chakula na Maji mengine naweza kuvumilia hapa watoto wa kishua kina Bill Lugano wakae kwa kutulia kwanza.

Binafsi nimeshawahi kufika vijiji mbalimbali ndani na nje ya Tanzania na kwakweli zipo baadhi ya sehemu zimebarikiwa inshallah ukifika hutamani kutoka haraka na miongoni mwa vijiji ambavyo nilishawahi kukaa na angalau nikalamba asali ni pamoja na;

Malela - Karatu - Arusha. Mnamo mwaka wa 2019 nilikwenda huko kulangua Mbaazi na Ngano, aisee kule kumebarikiwa bwana maana Kuna Chakula Cha kutosha achilia mbali watoto weupe wa kimbulu. Maziwa fresh au mtindi 1ltr nilikuwa nanunua kwa Tshs 800 wakati mayai ya kienyeji naletewa kwa 200Tshs, hali ya hewa nzuri sanaa nilirudi nyumbani nmetakata, wanawake wa kule sio wachoyo, sijui kwa wanaume lkn pia ardhi yao ina rutuba sana.

Kyomu - Moshi (v) Kilimanjaro. Kama ilivyoada nilimsindikiza rafiki yangu Ukweni, bwana wee! Jua sio kali sana, msosi sio suala maana wanafanya kilimo cha umwagiliaji hususani mbogamboga na matunda. Mayai kienyeji 200, nyanya za 500 unapikia siku tatu Maziwa unaamua unywe ndo ukamue au ukamue ndo unywe. Msosi sio shida mabinti wa kushika mkono tu tena kama ndo mgeni hupati tabu ardhi imebarikiwa Ila tu Kuna vumbi kimtindo Na watu wake ni wakarimu sana.

Mto wa Mbu (kijiji nimekisahau jina) - Monduli - Arusha. Pazuri kuanzia ardhi, Hali ya hewa, huduma za kijamii, mzunguko wa hela upo Chakula sio tabu, Watu wake wakarimu na Mabinti pia wamo si mchanganyiko wa Wairaq na masai.

Bukuru - Kondoa - Dodoma. Huku bwana nilifanya kama kupita tu lkn baadae niliamua kurudi nipaone vizuri. Kuna amani ya Hali ya juu unaweza kulala hata nje maana warangi sio watu wa hila. Chakula, Hali ya hewa, ardhi na watoto wa kirangi ndiyo haswa walinishawishi nirudi kupaona vizuri nikanunua na eneo kabisa
Vipo vijiji vitatu ambavyo sitaviorodhesha lakini vilinikosha sana pia ila tu hivyo hapo juu vilinikosha zaidi.

Je na wewe ni Kijiji gani ulichowahi kufika na kukaa kwa muda wowote ule pakakukosha kwa namna moja ama nyingine? karibuni wapenzi.
Mto wa Mbu (kijiji nimekisahau jina) - Monduli - Arusha. Pazuri kuanzia ardhi, Hali ya hewa, huduma za kijamii, mzunguko wa hela upo Chakula sio tabu, Watu wake wakarimu na Mabinti pia wamo si mchanganyiko wa Wairaq na masai.
Umenikumbusha mbai sana
 
Mto wa Mbu (kijiji nimekisahau jina) - Monduli - Arusha. Pazuri kuanzia ardhi, Hali ya hewa, huduma za kijamii, mzunguko wa hela upo Chakula sio tabu, Watu wake wakarimu na Mabinti pia wamo si mchanganyiko wa Wairaq na masai.
Umenikumbusha mbai sana
Ongea lolote tupate kitu alwatan Jr.
 
Back
Top Bottom