Kapicha basiKwenu enyi wajuzi wa mambo.
Naomba kujuzwa je ni sahihi kwa wanajeshi kuvuta bangi hadharani wakishirikiana na raia?
tangu pazuke kinachoitwa vita dhidi ya ugaidi hasa maeneo ya pwani humu nchini juhudi mbalimbali zimeanzishwa kukabiriana na mambo haya.moja wapo ni kuanzishwa kwa kanda maalumu huko pwani. vita hii ambayo kimkakati inalenga kuwatia adabu wote wenye kuleta fyoko dhidi ya serikali pendwa inawajumuisha wanajeshi wa JWTZ hawa wapo wengi sana huko pwani.
sote tunajua kazi za jeshi ni MIPAKA YA NCHI YETU ndio maana linaitwa jeshi la wananchi.
sasa mambo yamebadilika .
wanajeshi wanalinda raia dhidi ya watawala kwa kufanya hivyo wanafanya kazi ambazo sio zao kwakweli. miongoni mwa kazi wanazofanya ni pamoja na
1) kulinda hifadhi ya bahari yani mwajeshi anazuiaje uvuvi haramu kwa mfano.
2) kuzuia wanaoingia na wanaotoka maeneo hayo. mwanajeshi anamuuliza raia kitambulisho chake tena wakiwa bar usiku ? wengine wanatoa silaha hadharani , wengine wanapigana na raia na kujiita makomandoo basi ni visa na vituko vyao tu.
3) wanahariri mauzui ya mazungumzo ya watu hata kwenye vijiwe vya kahawa.
kubwa kuliko yote wanashirikiana na vijana wa maeneo hayo kuvuta BANGI Tena mchana kweupe hadharani kana kwamba wao wapo juu ya sheria?
Nawauliza wajuzi wa mambo ya jeshi je ni halali kwa mwanajeshi kuvuta BANGI Hadharani?