Ni sahihi kuvaa kandambili au kobazi kwenye public?

Mkuu unapata hadi muda wa kuangalia fulani kavaa hivi usawa huu wa Anko Gangachuma?
 
Mimi nafikiri hasara za kuvaa kandambili zinaweza kua kubwa kuliko faida. Nitatoa mifano:

1. Kama huna usafiri, jiandae kung'oka kucha kwa kujikwaa, au kukanyagwa kwenye daladala.
2. Kama una usafiri, ukikamatwa unaendesha gari huku umevaa ndala ni msala 30k inakuhusu
3. Ukipanda bodaboda ni rahisi ndala kuchomoka na kudondoka kitendo ambacho kinaweza sababisha ajali. Aidha, dole gumba linaweza ingia kwenye injini ya pikipiki na kuungua
4. Kwavile ndala ni laini, tegemea kwamba ukikanyaga kitu chenye ncha kali mfano msumari ni ishu
5. Mvua ikinyesha au kama kuna matope, wewe unakua huna tofauti na mtu anaetembea peku.
6. Ni ngumu kumkimbiza mwizi aliekwapua sim yako ukiwa umevaa kandambili
7. Kuna sehemu hawaruhusu kuingia na kandambili
8. Watoto wakikurushia mpira na wewe ukaupiga, kandambili utaikuta juu ya bati



Sababu dhaifu sana hizi. Ninadhani aliyezitoa hajui kanuni za mavazi. Yani, hajui mtu uvae nini na wakati gani. Hivyo, tunaposema tunavaa ndala, haimaanishi kila mahali au wakati wote. Kama ilivyo viatu vya kudumbukiza,si wakati wote ama kila mahali vinafaa. Mvaaji anapaswa kujitambua anafanya nini na kivipi. Hata ndala tunazosema hapa siyo ndala zako za kwa Mangi, ni ndala zimeenda chuo kikuu kiasi cha kuvutia machoni. Mfano, kuna hizo zipo pale Mr. Price, Mlimani City, binafsi, ninazihusudu sana, bahati mbaya saizi kubwa sijawahi kuzibahatisha.

Lakini, ukiacha kanuni, suala la hisia ni muhimu sana katika uvaaji, hivyo sisi tunashauri tu mengi hubaki kwenye maamuzi ya mtu binafsi.
 
Sababu dhaifu sana hizi. Ninadhani aliyezitoa hajui kanuni za mavazi. Yani, hajui mtu uvae nini na wakati gani. Hivyo, tunaposema tunavaa ndala, haimaanishi kila mahali au wakati wote. Kama ilivyo viatu vya kudumbukiza,si wakati wote ama kila mahali vinafaa. Mvaaji anapaswa kujitambua anafanya nini na kivipi. Hata ndala tunazosema hapa siyo ndala zako za kwa Mangi, ni ndala zimeenda chuo kikuu kiasi cha kuvutia machoni. Mfano, kuna hizo zipo pale Mr. Price, Mlimani City, binafsi, ninazihusudu sana, bahati mbaya saizi kubwa sijawahi kuzibahatisha.

Lakini, ukiacha kanuni, suala la hisia ni muhimu sana katika uvaaji, hivyo sisi tunashauri tu mengi hubaki kwenye maamuzi ya mtu binafsi.

Mkuu kwani wewe unaishi wapi? Ndala hizi hizi za kwa Mangi watu wanazunguka nazo mjini kila mahali we unaongea nini? Hapa hatuongelei sandals tunaongelea ndala za bafuni!
Na mimi sijasema mtu asivae, nimejaribu tu kuonyesha hasara za kuvaa ndala mjini. Still uamuzi wa kuvaa au kutovaa ni wako
 
Mkuu kwani wewe unaishi wapi? Ndala hizi hizi za kwa Mangi watu wanazunguka nazo mjini kila mahali we unaongea nini? Hapa hatuongelei sandals tunaongelea ndala za bafuni!
Na mimi sijasema mtu asivae, nimejaribu tu kuonyesha hasara za kuvaa ndala mjini. Still uamuzi wa kuvaa au kutovaa ni wako

Ninaishi hapahapa tz , tena ninaishi huku kwa watanzania wa kawaida tu.Ipo hivi,mimi kusema ndala za kwa Mangi ulikuwa ni mtazamo wangu kwa maana mchokoza mada hakusema ndala zipi.Sasa tupo wale tunaovaa ndala na kutembea nazo mjini,lakini ndala zinakuwa na mvuto,hata ukiwa nazo nyumbani pia baadhi hazijakaa kibafuni.

Zingatia

Sandals ni kitu kingine, sizungumzii sandals, nazungumzia kandambili, yani, flip flops.Aidha, wewe kutaja hasara za ndala haimaanishi watu tusihoji,wewe umechangia,ni sawa na mimi nachangia kwa kukosoa ulichosema. Si lazima tukubaliane nawe hasa hata kama haupo sahihi.

Mfano,unasema eti nikiwa naendesha gari, kwani nimekwambia nitavaa ndala nikiwa naendesha? Wakati wote mtu makini katika kuvaa unajua wazi kuwa nivae nini wapi na wakati gani.
 
Ninaishi hapahapa tz , tena ninaishi huku kwa watanzania wa kawaida tu.Ipo hivi,mimi kusema ndala za kwa Mangi ulikuwa ni mtazamo wangu kwa maana mchokoza mada hakusema ndala zipi.Sasa tupo wale tunaovaa ndala na kutembea nazo mjini,lakini ndala zinakuwa na mvuto,hata ukiwa nazo nyumbani pia baadhi hazijakaa kibafuni.

Zingatia

Sandals ni kitu kingine, sizungumzii sandals, nazungumzia kandambili, yani, flip flops.Aidha, wewe kutaja hasara za ndala haimaanishi watu tusihoji,wewe umechangia,ni sawa na mimi nachangia kwa kukosoa ulichosema. Si lazima tukubaliane nawe hasa hata kama haupo sahihi.

Mfano,unasema eti nikiwa naendesha gari, kwani nimekwambia nitavaa ndala nikiwa naendesha? Wakati wote mtu makini katika kuvaa unajua wazi kuwa nivae nini wapi na wakati gani.

Kwahiyo mkuu hua unabeba ndala kwenye pochi ukifika mjini ndio unazivaa au vipi? Au ukiwa kwenye gari unavaa viatu then ukishuka unavaa ndala? Maana wengi naowaona mimi hua wanatoka nyumbani wamevaa ndala na wanazunguka nazo kila mahali.
 
Kwahiyo mkuu hua unabeba ndala kwenye pochi ukifika mjini ndio unazivaa au vipi? Au ukiwa kwenye gari unavaa viatu then ukishuka unavaa ndala? Maana wengi naowaona mimi hua wanatoka nyumbani wamevaa ndala na wanazunguka nazo kila mahali.


Kama kweli umemaliza darasa la saba, sentensi hii kutoka post yangu ya mwisho ilipaswa kumaliza mjadala huu:

"Wakati wote mtu makini katika kuvaa unajua wazi kuwa nivae nini wapi na wakati gani"

Sasa hapo kwa muelewa sitegemei tena uulize naweka kwenye pochi,kwenye bonet, tairi au la. Baadhi yetu hata safari za mbali kama hatuendeshi tunavaa ndala.Wewe unatoka dar mpaka Bukoba au Kigoma, unalala njiani, upo kwenye basi na kiatu cha kudumbukiza, kha! Kwani wewe mwanajeshi?
 
Joto watembee uchi hata sandles wasivae, maana joto sio mchezo.
Niliona mtu kavaa leather jacket kwa baridi la hapa kwetu nikafurahi mwenyewe.
Hupangiwi, ila kandambili vaeni kwenu, mkitoka vaeni viatu vya kufunika muguu jamani.
Mkuu HATA NG'AMBO kuna SUMMER TIME.....hukuti MTU kavaa MABUTI JUA KALI,,,,,usiwalaumu wengine pengine wewe ndy KITUKO,,,usiyoenda na SEASONS...SANDLES ni aina ya KIATU CHA MAJIRA YA JOTO..,.usimpangie MTU cha KUVAA,,mbona wewe UNAVAA KAUNDA SUIT. , unajiona upo sawa?

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hahaha nilikuwa mjini siku moja nilikuwa naangalia wapita njia, yani unakuta mtu mguu hautamaniki kwa vumbi lakini kavaa kandambili, mmoja alikuja nilipokuwa nimekaa kwa show shine akiwa kashikilia kandambili moja iliyokatika moja kavaa, miguu yote haitamaniki kwa uchafu wa vumbi lakini, bado anataka ashonewe kandambili nikashindwa kuelewa, kwa uchafu ule kandambili za nini, ata angetembea peku asingeshangaliwa na yeyote.
Mkuu unapata hadi muda wa kuangalia fulani kavaa hivi usawa huu wa Anko Gangachuma?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hahaha zote ndala tu hakuna cha sandles wala za mangi, wavae viatu vya kufunika muguu. Mtu mguu mchafu bado anavaa sandles, bora kupekua tu hutotimua vumbi au kurusha tope.
Mkuu kwani wewe unaishi wapi? Ndala hizi hizi za kwa Mangi watu wanazunguka nazo mjini kila mahali we unaongea nini? Hapa hatuongelei sandals tunaongelea ndala za bafuni!
Na mimi sijasema mtu asivae, nimejaribu tu kuonyesha hasara za kuvaa ndala mjini. Still uamuzi wa kuvaa au kutovaa ni wako

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hahaha vaeni viatu jamani, sandles na flipflop ni uchafu kuzunguka nazo mjini. Hizo vaenu ndani ya mageti yenu, ukienda nje vaa viatu kwa ustaarabu.
Hakuna kandambili inayovutia, miguu michafu kandambili inavutia nini?! Mtu anatoka ukonga hadi buguruni hadi pisya jandambili gani au sandles gani zina himili joto na vumbi hilo?! Hata tairi za gari zina pata joto na kuchanika.
Ninaishi hapahapa tz , tena ninaishi huku kwa watanzania wa kawaida tu.Ipo hivi,mimi kusema ndala za kwa Mangi ulikuwa ni mtazamo wangu kwa maana mchokoza mada hakusema ndala zipi.Sasa tupo wale tunaovaa ndala na kutembea nazo mjini,lakini ndala zinakuwa na mvuto,hata ukiwa nazo nyumbani pia baadhi hazijakaa kibafuni.

Zingatia

Sandals ni kitu kingine, sizungumzii sandals, nazungumzia kandambili, yani, flip flops.Aidha, wewe kutaja hasara za ndala haimaanishi watu tusihoji,wewe umechangia,ni sawa na mimi nachangia kwa kukosoa ulichosema. Si lazima tukubaliane nawe hasa hata kama haupo sahihi.

Mfano,unasema eti nikiwa naendesha gari, kwani nimekwambia nitavaa ndala nikiwa naendesha? Wakati wote mtu makini katika kuvaa unajua wazi kuwa nivae nini wapi na wakati gani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hahaha sasa waangalie miguu ilivyopigwa vumbi, unashindwa kuelewa anazuia nini.
Hawa ndio wanaosha kandambi anatembea kwa mguu zisichafuke.
Kwahiyo mkuu hua unabeba ndala kwenye pochi ukifika mjini ndio unazivaa au vipi? Au ukiwa kwenye gari unavaa viatu then ukishuka unavaa ndala? Maana wengi naowaona mimi hua wanatoka nyumbani wamevaa ndala na wanazunguka nazo kila mahali.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hahaha hata jama unatoka Dar hadi Brunei kiatu muhimu acheni uchafu, kandambili na sandles zenu vaeni ndani ya kuta za nyumba zenu, publicly vaeni viatu vya kufunika makanyagio yenu.
Kama kweli umemaliza darasa la saba, sentensi hii kutoka post yangu ya mwisho ilipaswa kumaliza mjadala huu:

"Wakati wote mtu makini katika kuvaa unajua wazi kuwa nivae nini wapi na wakati gani"

Sasa hapo kwa muelewa sitegemei tena uulize naweka kwenye pochi,kwenye bonet, tairi au la. Baadhi yetu hata safari za mbali kama hatuendeshi tunavaa ndala.Wewe unatoka dar mpaka Bukoba au Kigoma, unalala njiani, upo kwenye basi na kiatu cha kudumbukiza, kha! Kwani wewe mwanajeshi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom