Zekidon
JF-Expert Member
- May 29, 2013
- 1,903
- 566
Yamemkuta Rafiki yangu anahitaji ushauri.
Ipo hivi!!!!
Alikuwa na mwanamke wake kwa kipindi cha miaka mitatu. Akawa akimpa huduma zote.
Kwa kiburi chake, mwanamke akamuacha rafiki yangu, akakimbia kuolewa na mwanaume wake wa zamani.
Baada ya miezi mitatu tu ya ndoa, huko alikokuwa ndoa ikamshinda. Wakawa wamerudi katika mahusiano tena ( yule mwanamke aliyeachika na rafiki yangu) hapo kumbuka bado alikuwa hajaachika. Wameendelea katika mahusiano kipindi chote mpaka wakati wanatengana yule mwanamke na mumewe.
Sasa tatizo lipo kwa rafiki yangu kuwa, anaona sio sahihi kumuoa huyo mwanamke kwani alichomtenda awali haikuwa sahihi.
Mwanamke alimdhalilisha sana jamaa kwa kuolewa na mtu mwingine, ila huko nako akashindwa .
Je ni sahihi kurudiana na hatimaye kuoana na mtu ambaye hapo awali alikutendea mabaya??
Tumsaidieni huyu ndugu yetu.
Ipo hivi!!!!
Alikuwa na mwanamke wake kwa kipindi cha miaka mitatu. Akawa akimpa huduma zote.
Kwa kiburi chake, mwanamke akamuacha rafiki yangu, akakimbia kuolewa na mwanaume wake wa zamani.
Baada ya miezi mitatu tu ya ndoa, huko alikokuwa ndoa ikamshinda. Wakawa wamerudi katika mahusiano tena ( yule mwanamke aliyeachika na rafiki yangu) hapo kumbuka bado alikuwa hajaachika. Wameendelea katika mahusiano kipindi chote mpaka wakati wanatengana yule mwanamke na mumewe.
Sasa tatizo lipo kwa rafiki yangu kuwa, anaona sio sahihi kumuoa huyo mwanamke kwani alichomtenda awali haikuwa sahihi.
Mwanamke alimdhalilisha sana jamaa kwa kuolewa na mtu mwingine, ila huko nako akashindwa .
Je ni sahihi kurudiana na hatimaye kuoana na mtu ambaye hapo awali alikutendea mabaya??
Tumsaidieni huyu ndugu yetu.