Ni sahihi kisheria mtu kukatwa mkopo mara mbili kwa wakati mmoja kabla ya mshahara kuingia na baada ya mshahara kuingia?

Jalema

JF-Expert Member
Oct 26, 2013
593
856
Habari zenu wakuu bila kuzunguka acha niende moja kwa moja kwenye mada tajwa hapo juu.

Mimi ni muajiriwa katika taasisi moja hapa nchini.Miaka miwili iliyopita nilichukua mkopo katika benki moja maarufu tu.Baada tu ya mkopo kuingia kwenye account yangu mwezi uliofuta nilianza kukatwa mshahara.

Katika kukagua kiasi cha fedha ninayotakiwa kubaki nayo baada ya kukatwa kila kitu pamoja na deni ninalodaiwa niligundua kuna mapungufu ya fedha zaidi ya elfu 50 ambayo huwa inakatwa baada ya kukatwa makato yote ikiwa ni pamoja na deni la benki. Nikasema embu nisubiri baada miezi mitatu nione.

Bàada ya huo muda ilinibidi niende benki kwa afisa mikopo nkamuuliza inakuaje nnakatwa fedha ya kulipa deni lenu mara mbili? Akanitolea bank statement akakagua akuta ni kweli jibu alilonipa ni kwamba nisiwe na wasiwasi fedha yote ninayokatwa inaenda kulipa deni.

Wiki iliyopita nimejaribu kupiga calculation ya miezi yote niliyoliopa deni nikalinganisha na fedha ninayodaiwa ili kumaliza deni pamoja na jumla ya fedha ninayotakiwa kulipa yoote pamoja na riba kwa kile kiasi ninachokatwa mwanzo ambacho ni halali hesabu zinakubali

Shida inakuja kwamba nikijumuisha ile elfu hamsini naa inayo katwa mara ya pili baada ya kukatwa kila kitu hesabu zinakataa ambayo afsa mikopo ndio aliniambia inakwenda kufidia deni

Hivyo ninaomba ushauri na kujuzwa je ni sahihi kiutaratibu na kisheria mtu kukatwa mkopo mara mbili kwa wakati mmoja kabla ya mshahara kuingia na baada ya mshahara kuingia.Karibuni wadau kwa msaada
 
Sio sahihi.

Rejea makubaliono ya mkataba wako na CRDB.

Ilikupata ufumbuzi mfuate afisi utumishi wako mweleze.... Ikibidi watembelee takukuru waelezi uhuni wa wizi unaofanyiwa na benki kubwa nchini.

Ikubainika Ni kweli wako nje ya mkataba pesa yako itarudi na fidia pia.


Pole sana mkubwa
 
Sio sahihi.

Rejea makubaliono ya mkataba wako na CRDB.

Ilikupata ufumbuzi mfuate afisi utumishi wako mweleze.... Ikibidi watembelee takukuru waelezi uhuni wa wizi unaofanyiwa na benki kubwa nchini.

Ikubainika Ni kweli wako nje ya mkataba pesa yako itarudi na fidia pia.


Pole sana mkubwa
Shukran mkuu nnashkuru
 
Muache alete tu ujuaji mkuu.
Lingine ni hili la M Pawa ya hawa Vodacom ukikopa huko wanakata riba KABLA hujaweka pesa hiyo kwenye mikakati yao . Kinachokera sasa ukipata mkopo ule ni muda wa mwezi ufanye marejesho . Ooohhoo masaa 17 hadi 25 toka upokee mkopo utaambia mkopo wako wa78,900/= unatakiwa kuarudishwa kuanzia sasa . Jamani kawizi haka vipi jamani daaah
 
Naona kwa sasa thread za kulalamika kutoka kwa watumishi waliokopa benki hapa JF zimeshika kasi sana.
Nahisi akili za watumishi zimeanza kuwakaa sasa, vyuma vimekaza kote kote.
 
Habari zenu wakuu bila kuzunguka acha niende moja kwa moja kwenye mada tajwa hapo juu.

Mimi ni muajiriwa katika taasisi moja hapa nchini.Miaka miwili iliyopita nilichukua mkopo katika benki moja maarufu tu.Baada tu ya mkopo kuingia kwenye account yangu mwezi uliofuta nilianza kukatwa mshahara.

Katika kukagua kiasi cha fedha ninayotakiwa kubaki nayo baada ya kukatwa kila kitu pamoja na deni ninalodaiwa niligundua kuna mapungufu ya fedha zaidi ya elfu 50 ambayo huwa inakatwa baada ya kukatwa makato yote ikiwa ni pamoja na deni la benki. Nikasema embu nisubiri baada miezi mitatu nione.

Bàada ya huo muda ilinibidi niende benki kwa afisa mikopo nkamuuliza inakuaje nnakatwa fedha ya kulipa deni lenu mara mbili? Akanitolea bank statement akakagua akuta ni kweli jibu alilonipa ni kwamba nisiwe na wasiwasi fedha yote ninayokatwa inaenda kulipa deni.

Wiki iliyopita nimejaribu kupiga calculation ya miezi yote niliyoliopa deni nikalinganisha na fedha ninayodaiwa ili kumaliza deni pamoja na jumla ya fedha ninayotakiwa kulipa yoote pamoja na riba kwa kile kiasi ninachokatwa mwanzo ambacho ni halali hesabu zinakubali

Shida inakuja kwamba nikijumuisha ile elfu hamsini naa inayo katwa mara ya pili baada ya kukatwa kila kitu hesabu zinakataa ambayo afsa mikopo ndio aliniambia inakwenda kufidia deni

Hivyo ninaomba ushauri na kujuzwa je ni sahihi kiutaratibu na kisheria mtu kukatwa mkopo mara mbili kwa wakati mmoja kabla ya mshahara kuingia na baada ya mshahara kuingia.Karibuni wadau kwa msaada
Mkuu hiyo kitu sio sawa, nenda kamuone meneja wa bank pamoja na bank statement inayoonesha miezi yote waliyokukata mara mbili hela yako irudishwe haraka sana.


Ila siku hizi hii bank kubwa ..... ina makato ya ajabu ajabu sana. Ndiyo maana sisi wengine tunataka kuwakimbia pia.
 
Back
Top Bottom