Ni rais yupi kati ya hawa anakubalika zaidi?

No admission

JF-Expert Member
Nov 26, 2011
215
68
JK Nyerere: Alishindwa kujenga hata nyumba yake ya kuishi lakini chanzo cha umaskini kilianzia kwake kwa kuanzisha azimio la Arusha

A. Mwinyi: Free rain leadership: Nchi ilijilimbikizia madeni kibao mpaka leo hii hayajamalizwa kulipwa
B. Mkapa: Utandawazi na soko huria: Kajilimbikizia mali nyingi na kawa chanzo cha rushwa Tanzania
JK aka baba Mwanaasha: Hapa sichangii

Naomba maoni yenu
 
kati ya hao wote best alkua ni nyerere coz kwtupa uhuru,hat mwanamke humkumbuka sana mwanaume aliyemtoa usichana wake kuliko wengne..
 
Ba Mwanaasha anafaa kwani ameshirikisha familia yake ipasavyo kuuza sura, ukianzia riz1, mdogo wake riz1 sijui nani,
1st ledi mwenyewe-mfilisi mkuu wa mali ya Taifa la Tanzania, Ba mwanaasha mwenyewe aka wa kuchekacheka.
Inshort ameshirikisha familia yake ipasavyo kuifilisi Taifa hili. Ikitokea ni kushtakiwa ni wote, labda "mwanaasha tutamwekea mdhamana".
 
Rais wa Tanzania aliyeleta mabadiliko ya kweli ni Kikwete peke yake. Nimebahatika kuwepo awamu zote nne.

Nyerere = huyu hafai kabisa.
Mwinyi = alijitahidi sana lakini alikuta uozo ulioachwa na Nyerere.
Mkapa = Huyu hana lolote zaidi ya ubabe na kujilimbikizia mali. EPA, KAGODA, RADAR, NDEGE, UMEME, yote madudu yake.

Kikwete= shule, zahanati, uchumi, barabara, umeme, utalii, demokrasia, maji, viwanja vya ndege, mahusiano ya kimataifa, mikutano ya kimataifa Tanzania. Karibu kila nyanja kawapita hao wote vibaya sana.

Chukua vya wote hao, utakuta Kikwete kawashinda katika vyote kwa idadi na ubora. Hakuna hata kimoja ambacho hajafanya zaidi yao, tena jumlisha vya wote si mmoja mmoja. Na ndio bado hajamaliza muda wake kwa miaka zaidi ya mitatu. Huyu Mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete anasatahili kila dua njema.
 
minaona mkapa na nyerere cause ukiangalia mkapa uongozi wake uligubikwa na rushwa lakini alifanya mambo mengi kama kujenga misingi mizuri ya uchumi wa nchi na kupambana na mfumuko wa bei.

ya nyerere obviously siwezi kuyasema nimengi sana japo nae alichemka na azimio la arusha.
 
Japo kila mtu ana mapungufu yake lakini Nyerere is the best,alijenga umoja na mshikamano miongoni mwa watanzania bila kujali dini wala kabila,hiki ni kitu cha msingi
 
Rais wa Tanzania aliyeleta mabadiliko ya kweli ni Kikwete peke yake. Nimebahatika kuwepo awamu zote nne.

Nyerere = huyu hafai kabisa.
Mwinyi = alijitahidi sana lakini alikuta uozo ulioachwa na Nyerere.
Mkapa = Huyu hana lolote zaidi ya ubabe na kujilimbikizia mali. EPA, KAGODA, RADAR, NDEGE, UMEME, yote madudu yake.

Kikwete= shule, zahanati, uchumi, barabara, umeme, utalii, demokrasia, maji, viwanja vya ndege, mahusiano ya kimataifa, mikutano ya kimataifa Tanzania. Karibu kila nyanja kawapita hao wote vibaya sana.

Chukua vya wote hao, utakuta Kikwete kawashinda katika vyote kwa idadi na ubora. Hakuna hata kimoja ambacho hajafanya zaidi yao, tena jumlisha vya wote si mmoja mmoja. Na ndio bado hajamaliza muda wake kwa miaka zaidi ya mitatu. Huyu Mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete anasatahili kila dua njema.

ila umesahau kuwa ni muumin mwenzetu.:lol:
 
Nyerere:-
  1. Kwanza alituletea uhuru, tukumbuke alikubali kuacha kazi yenye kumlipa mshahara mzuri ili tu afanye siasa na kisha kuleta uhuru, usisahau kuwa ali risk kwasababu wakoloni wangeweza hata kumuua so mama maria angeweza kubaki mjane na akina madaraka wasingekuwepo.
  2. Nchi ikiwa haina rasilimali za kutosha aliweza kusomesha Watanzania bure kuanzia msingi hadi ngazi ya Uprofesor tena ikibidi hata kuwapeleka nje ya nchi.
  3. Aliweza kunyang'anya shule zilizokuwa zikimilikiwa na taasisi zisizo za kiserikali hasa makanisa, (wakatoliki wakiwa ndio waathirika zaidi) ili hata watoto wasiokuwa na dini, au waislam nao wasome tena bure, chakula na nauri ya kwenda na kurudi shule daftari N.K vikiwa ni bure.
  4. Matibabu yalikuwa bure kabisa, kuanzia dispesari hadi Muhimbiri.
  5. Ndiye aliyeweka karibu vyanzo vyote vya umeme tunavyo vitumia leo bila ufisadi.
Mwinyi:-
  1. Huyu alianza vizuri kwa kurudisha uwajibikaji maofisini miaka yake ya mwanzo kwa kitu alicho kiita fagio la chuma, nakumbuka hadi akina Maalimu Ghurumo waliwahi kupata kazi za tempo kwa kuanzisha bend ya all Tanzania stars.
  2. Chanzo cha ufisadi kama tukiwa wakweli kilianzia kwake, kumbuka Mrema na neno "Vigogo na dhahabu ya uwanja wa ndege"
  3. Alitetea sna mawaziri wa dini yake hata kama wame underperform vibaya, remember Kighoma Alli Malima, rushwa wizara ya fedha ilitawala kwa ajabu sana, wahindi walikuwa hawatoi kabisa kodi, kila kitu waziri wa fedha ameruhusu, nchi ilikuwa haina pesa lakini watu wana mihela ajabu, nakumbuka vijana wengi enzi hizo waliacha hata kwenda shule (Chuo kikuu) kwa vile hali za wafanyakazi wa serikalini zilikuwa taabani while wazee wa mision town walikuwanazo za kutosha, kwenye mabar wakati huo uliweza kusikia mtu anasema, "Nitakupiga na hela za matibabu nitakupa" pia mtu aliweza kuingia bar na kuagiza crate za bia, sio kabia kamoja kamoja, au letet kama tulivyo, yote haya yalianzia kwa mzee ruksa.
  4. Yeye ndiye aliyeanzisha mageuzi ya kiuchumi, kijamii na kisias, vyama vingi vilianzia kwake, japo kulikuwa na mkono wa Nyerere pia, vyombo vingi vya habari kama TV, Redio (redio 1 na ITV also CTN)
  5. Mashule mengi yalibadilishwa kuwa Day badala ya Boarding school, faida yake ni kuwa watoto waliokuwa karibu na shule hizo ndo walikwa wakisoma, watu kuijua nchi yao kupia kutemebea kutoka mkoa 1 kwenda mwingine kufuata shule uliishia hapo.
  6. Mauaji ya ajabu pia yalianzia hapo, remember Francis Katabaro wa Mfanyakazi news paper.
MKAPA:-
  1. Alijenga barabara nyingi kwa pesa zetu
  2. Heshima ya wafanyakazi wa serikali ilianza kurudi enzi zake.
  3. Alibana sana demokrasia ya vyama vingi pamoja na uhuru wa kujieleza, mkumbuke mzee Jenerali Ulimwengu.
  4. Namsifu, hakuwa mdini kama Mwinyi na ******.
  5. Ufisadi mkubwa hapa ndo ulipoendelezwa, EPA, IPTL japo hii ilirithiwa toka kwa Mwinyi (kwenye utawala wake ndo tuliposhindwa kesi na kujikuta tunawalipa hadili 2015)
  6. Aliiacha nchi ikiwa na akiba ya kutosha ya fedha za ndani na za kigeni na madeni machache sana.
******:-
  1. Akiona anaelemewa tu, anasingizia kuwa wanamomwonea kwakua yeye ni mwislam (huwa hasemi yeye, hutumia watu), pia akishindwa jambo tu, anakimbilia nje ya nchi kujipumzisha.
  2. Mengine malizieni, maana huyu wote tunamwona.
 
JK Raisi wa kwanza kudhibiti malaria kwa vitendo.
Raisi wa kwanza kuruhusu mawaziri wapelekwe mahakamani bila dhamana!
Raisi wa kwanza kukutana na upinzani mzito lakini akavuka salama!
Raisi wa kwanza kutoa uhuru wa vyombo vya habari!
Raisi wa kwanza aliezungukwa na wajanja (Mawaziri, plus na na na)

JK huwezi mfanananisha na Mwinyi au Mkapa!

Japo anamapungufu yake but sii sawa na hao waliopita!!

God bless him
 
download
 
Rais wa Tanzania aliyeleta mabadiliko ya kweli ni Kikwete peke yake. Nimebahatika kuwepo awamu zote nne.

Nyerere = huyu hafai kabisa.
Mwinyi = alijitahidi sana lakini alikuta uozo ulioachwa na Nyerere.
Mkapa = Huyu hana lolote zaidi ya ubabe na kujilimbikizia mali. EPA, KAGODA, RADAR, NDEGE, UMEME, yote madudu yake.

Kikwete= shule, zahanati, uchumi, barabara, umeme, utalii, demokrasia, maji, viwanja vya ndege, mahusiano ya kimataifa, mikutano ya kimataifa Tanzania. Karibu kila nyanja kawapita hao wote vibaya sana.

Chukua vya wote hao, utakuta Kikwete kawashinda katika vyote kwa idadi na ubora. Hakuna hata kimoja ambacho hajafanya zaidi yao, tena jumlisha vya wote si mmoja mmoja. Na ndio bado hajamaliza muda wake kwa miaka zaidi ya mitatu. Huyu Mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete anasatahili kila dua njema.

akili zako zipo kwenye masaburi....unamfananisha kikwete na mkapa? mkapa ni mwizi ndio ila baba mwanaisha hawezi kumfikia mkapa
 
JK Raisi wa kwanza kudhibiti malaria kwa vitendo.
Raisi wa kwanza kuruhusu mawaziri wapelekwe mahakamani bila dhamana!
Raisi wa kwanza kukutana na upinzani mzito lakini akavuka salama!
Raisi wa kwanza kutoa uhuru wa vyombo vya habari!
Raisi wa kwanza aliezungukwa na wajanja (Mawaziri, plus na na na)

JK huwezi mfanananisha na Mwinyi au Mkapa!


Japo anamapungufu yake but sii sawa na hao waliopita!!

God bless him
direct wewe untakuwa na mtu wa karibu sana wa JK hilo halina ubishi..ordinary Tanzanian ambaye hana direct contact na hawa marais au hakuwa na direct contact hawez kuweka comment ya aina huu
 
JK Nyerere: Alishindwa kujenga hata nyumba yake ya kuishi lakini chanzo cha umaskini kilianzia kwake kwa kuanzisha azimio la Arusha

A. Mwinyi: Free rain leadership: Nchi ilijilimbikizia madeni kibao mpaka leo hii hayajamalizwa kulipwa
B. Mkapa: Utandawazi na soko huria: Kajilimbikizia mali nyingi na kawa chanzo cha rushwa Tanzania
JK aka baba Mwanaasha: Hapa sichangii

Naomba maoni yenu

Jibu kwang ni rahisi tu ni William Mkapa pamoja na mapungufu yake lakini kazi yake inaonekana.Thereb was no big inflation rate,no price inrease in consumable goods,infrustrusture were well networked and many more.
 
Rais wa Tanzania aliyeleta mabadiliko ya kweli ni Kikwete peke yake. Nimebahatika kuwepo awamu zote nne.

Nyerere = huyu hafai kabisa.
Mwinyi = alijitahidi sana lakini alikuta uozo ulioachwa na Nyerere.
Mkapa = Huyu hana lolote zaidi ya ubabe na kujilimbikizia mali. EPA, KAGODA, RADAR, NDEGE, UMEME, yote madudu yake.

Kikwete= shule, zahanati, uchumi, barabara, umeme, utalii, demokrasia, maji, viwanja vya ndege, mahusiano ya kimataifa, mikutano ya kimataifa Tanzania. Karibu kila nyanja kawapita hao wote vibaya sana.

Chukua vya wote hao, utakuta Kikwete kawashinda katika vyote kwa idadi na ubora. Hakuna hata kimoja ambacho hajafanya zaidi yao, tena jumlisha vya wote si mmoja mmoja. Na ndio bado hajamaliza muda wake kwa miaka zaidi ya mitatu. Huyu Mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete anasatahili kila dua njema.

Shule mpaka chuo kikuu cha dodoma (By the way, ni chuo kikuu au primary. Chuo unsoma mpaka mwisho hufundishwi na mwalimu mwenye PhD.

Pamoja na ubabe wa Mkapa, by the way Tanzania tunahitaji dictator, uchumi uliimarika. Miaka kumi Daa nauli ni 150 Shs only

Nyerere wakati wake hela haikuwepo bwana.
 
Rais wa Tanzania aliyeleta mabadiliko ya kweli ni Kikwete peke yake. Nimebahatika kuwepo awamu zote nne.

Nyerere = huyu hafai kabisa.
Mwinyi = alijitahidi sana lakini alikuta uozo ulioachwa na Nyerere.
Mkapa = Huyu hana lolote zaidi ya ubabe na kujilimbikizia mali. EPA, KAGODA, RADAR, NDEGE, UMEME, yote madudu yake.

Kikwete= shule, zahanati, uchumi, barabara, umeme, utalii, demokrasia, maji, viwanja vya ndege, mahusiano ya kimataifa, mikutano ya kimataifa Tanzania. Karibu kila nyanja kawapita hao wote vibaya sana.

Chukua vya wote hao, utakuta Kikwete kawashinda katika vyote kwa idadi na ubora. Hakuna hata kimoja ambacho hajafanya zaidi yao, tena jumlisha vya wote si mmoja mmoja. Na ndio bado hajamaliza muda wake kwa miaka zaidi ya mitatu. Huyu Mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete anasatahili kila dua njema.


we nyau!
 
Kambarage asifananishwe na wengine kiutendaji,kiuadilifu.Kiongozi gani kati ya hawa Maraisi wa tatu angefanya yafuatayo wakati ule nchi imepewa uhuru na kipindi chote cha uongozi wake?

1.Kukubali kujipunguzia mshahara

2.Kutokuweka tofauti kati ya familia yake na mtanzania mwingine

3.Kutokuwa na nyumba ya kisasa

4.Kuishi maisha ya kawaida kama mkulima

5.Kujenga umoja wa kitaifa kwa kutumia Kiswahili

6.Kuongoza taifa la wajinga

Tumshukuru Mungu baada ya kutoka mwinyi alifwatia Mkapa vinginevyo kama angefwata Baba Ridhi mwaka 1995 sijui ingekuwaje nadhani tungekuwa na noti ya laki moja.

Siwezi kumtetea Mkapa kwa aliyoyafanya ila yale mazuri yalikuwa na msingi mkubwa kwa taifa na yale ya radda,epa,na mengine ndio kama yanavyoonekana


Wote wanamazuri na mabaya yao hata baba Ridhi naye
 
Shule mpaka chuo kikuu cha dodoma (By the way, ni chuo kikuu au primary. Chuo unsoma mpaka mwisho hufundishwi na mwalimu mwenye PhD.

Pamoja na ubabe wa Mkapa, by the way Tanzania tunahitaji dictator, uchumi uliimarika. Miaka kumi Daa nauli ni 150 Shs only

Nyerere wakati wake hela haikuwepo bwana.

1. Kuwa na PhD sio kujuwa kufundisha. Isitoshe tulimsikia "live" kwenye TV akimuomba Makamu wa Rais Dr. Mohamed Gharib Bilal kuwa aende akasaidie kufundisha pale.

2. Kuwa na nauli ya shilling 150 hakumaanishi uchumi umekuwa au umepunguwa. Pole sana. Muhimu kuwepo na usafiri.
 
Kwenye suala la uadilifu nyerere alikuwa juu ukimlinganisha na Mkapa au Kikwete maana hawa wawili ni wala rushwa tu.

Kwenye suala la uhuru wa kujieleza wote zero maana hata sasa hivi wanalialia JF ifungwe.

Kwenye ujengaji wa miundombinu Mkapa yuko juu maana hata Kikwete anatembelea kwenye yale aliyoyaanzisha Mkapa.

Kwenye kutoa maamuzi mwalimu Nyerere na Mkapa wako juu ukilinganisha na Kikwete maana hata kukemea hawezi.

Sijamzungumzia Mwinyi maana alikuwa mdini zaidi

Nilitaka kusahau raisi anayeongoza kuchekacheka aisee baba Mwanaasha
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom