Ni Rais Magufuli pekee ndiye anayeweza kurudisha Imani kwa watanzania ili waende kujiandikisha kupiga kura

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,480
30,152
Kama kichwa changu cha habari kinavyosema ni Rais Magufuli peke yake anayeweza kuwahakikishia na kuwarudishia imani watanzania ili waende kwenye vituo vya kuandikisha wapiga kura wa serikali za mitaa

Unaweza kujiuliza je atawahakikishaje watanzania?

Swali hili jibu lake ni hili, ni Rais Magufuli ndiye aliyewavunja moyo wapiga kura wa nchi hii hadi wamekata tamaa ya kuona zoezi zima la kupiga kura kama kichekesho, kwa kuona hata kama utapiga kura, lakini matokeo yake yanajulikana, ni "lazima" atangazwe mwanaCCM kuwa ameshinda uchaguzi huo.

Kauli na mienendo ya Rais Magufuli ndiyo ambayo imewafanya watanzania wakate tamaa kabisa na zoezi la kupiga kura nchini Tanzania

Tujiulize nchi ambayo imekuwa ikipiga hatua kidemokrasia hadi mwaka 2015 wakati anaingia madarakani Rais huyu ambaye kwa kauli zake na vitendo vyake vinaonyesha dhahiri kuwa ana nia ya kuua upinzani nchini na nchi irejee kwenye mfumo wa chama kimoja

Tunajionea namna mtawala huyu anavyojitahidi kuwajaza makada kindakindaki wa CCM kwenye Tume ya uchaguzi ya Taifa, akiwemo Mkurugenzi wake Dkt Wilson Mahera, licha ya mhimili wa mahakama kuwapiga marufuku wanachama waandamizi wa vyama vya siasa kutoteuliwa kwenye chombo hiko kinachosimamia uchaguzi.

Ni yeye Rais ambaye akinukuliwa huko siku za nyuma akiwaambia wateule wake kuwa nimekuteua na kukupa gari ya kifahari ya kutembelea, nyumba nzuri ya kuishi na mshahara mnono, halafu nisikie unamtangaza mpinzani kashinda katika eneo lako! Utakuwa umejifukuzisha kazi!

Kwa hiyo anatakiwa Rais Magufuli alihutubie Taifa na kuwahakikishia watanzania kuwa uchaguzi ujao wa serikali za mitaa utakuwa huru na haki na atubu kwa watanzania kuwa yale maneno na matendo yake aliyokuwa anayatoa alikuwa amekosea na ni uvunjifu wa Katiba wa waziwazi kabisa

Kwa kuyasema hayo na awasihi watanzania wamiminike kwa wingi kwenye vituo vya kujiandikisha, nina hakika baada ya tamko hilo watanzania watafurika kwenye vituo vya kupigia kura.

Lakini kinyume cha hapo, ikiwa Rais hatapenda kujishusha na kujisahihisha na kuona kuwa maneno yake na vitendo vyake ndivyo vilivyosababisha watanzania wavunjike sana moyo wa kujiandikisha basi itakuwa sawasawa na kutwanga kwenye kinu kilichojaa maji!
 
Kwake hiyo hali ni nafuu. Anajua vizuri 2015 alipata % ngapi. Na ndiyo maana nguvu nyingi imetumika kuviua vyama vingine hasa Cuf & Cdm . Huu ni mkakati maalum.
Lakini Inakuwaje aone hiyo ndiyo nafuu kwao CCM, wakati huo huo wanatumia nguvu kubwa "kuwalazimisha" wapiga kura wakajiandikishe kwenye vituo vya kupigia kura??
 
Kitendo cha wananchi kugomea kujiandikisha kupiga kura watawala mkichukulie kama ‘a wake up call’. Mdharau mwiba miguu huota tende.

Wananchi wameonyesha kuwa wamechoka na wako tayari kwa lolote ili kupata demokrasia.

Mnawategemea polisi! Polisi ni wangapi kulinganisha na idadi ya raia?
 
Kitendo cha wananchi kugomea kujiandikisha kupiga kura watawala mkichukulie kama ‘a wake up call’. Mdharau mwiba miguu huota twende.

Wananch wameonyesha kuwa wamechoka na wako tayari kwa lolote ili kupata demokrasia.

Mnawategemea polisi! Polisi ni wangapi kulinganisha na idadi ya raia?
Ni kweli kabisa kuwa CCM imebaki na tegemeo lake pekee kuwa ni Jeshi la Polisi na kuligeuza Jeshi hilo kuwa miongoni ya vitengo vyake
 
Ukweli ni huu hata hayo magari ya matangazo waliyoyakodi kwa kodi zetu, kwa ajili ya kuhamasisha wapiga kura wakajiandikishe kwenye vituo, hayasaidii kitu

Hata hili tishio la Rais la kuwatumbua maRC ambao wapiga kura wao hawakujitokeza kwa wingi kujiandikisha kwenda kupiga kura hizi za serikali ya mitaa, naliona kama ni kichekesho kitupu!
 
hili neno.

while on that......

hivi upinzani hauwezi kupinga mahakamani teuzi za Rais ambazo zinaonekana dhahiri kuikanyaga katiba?

I mean.... kama ni illegal they'll definitely remain that - illegal!
and the court can surely determine that
that, can't it?

my point (as has always been on this forum) ni kwamba upinzani ujenge utamaduni wa kuhakikisha una formalize complaints mbalimbali kisheria ili kuwepo na traceable records hata kama court ruling kwa wakati husika itakuwa unfavourable. there's always a chance such a ruling being overturned at a higher level at some point afterwards.

please don't call me naive...lol!
 
Lakini Inakuwaje aone hiyo ndiyo nafuu kwao CCM, wakati huo huo wanatumia nguvu kubwa "kiwalazimisha" wapiga kura wakajiandikishe kwenye vituo vya kupigia kura??
Just show kwa wafadhili wao. Lakini kwa aina ya raia WaTz wamefanikiwa. % kubwa ya raia wa Tz wangelikuwa na misimamo kama wale Tarime & Kilimanjaro upuuzi usingelikuwa mwingi .
 
Lakini Inakuwaje aone hiyo ndiyo nafuu kwao CCM, wakati huo huo wanatumia nguvu kubwa "kiwalazimisha" wapiga kura wakajiandikishe kwenye vituo vya kupigia kura??
Hawa ni Mabingwa wa kupika Takwimu. Ni kiini macho tu ili kuihadaa Dunia kuwatazama waliojiandikisha na waliopiga kura ni wengi. Rejea hata kwenye mikutano yao wanavyowasomba watu kwa malori ili waonekane wanapendwa wakati wanafahamu fika kuwa hawategemei ushindi kupitia sanduku la kura.

Hivi sasa watu wameamua kumuacha afanye apendavyo kwani sio mtu wa kushaurika. Sio mtu wa kuona umuhimu wa kuwa na Katiba wala Sheria wala Mahakama wala Bunge katika Nchi kwani yeye Mwenyewe anaona mawazo yake ni bora kuliko wengine wote. Kama ameweza kuamua kuiweka Mahakama mfukoni na kuwaamuru Watuhumiwa dhidi ya uhujumu uchumi wakiriakisha kukubali kulipa fedha wanazotuhumiwa nazo unategemea nini kwa Bw Yule? Hakuna marefu yasiyo na ncha. Tuasubiri afike ukingoni tuanze kuijenga nchi upya.
 
hili neno.

while on that......

hivi upinzani hauwezi kupinga mahakamani teuzi za rais ambazo zinaonekana dhahiri kuikanyaga katiba?

I mean.... kama ni illegal they'll definitely remain that - illegal!
and the court can surely determine that
that, can't it?

my point (as has always been on this forum) ni kwamba upinzani ujenge utamaduni wa kuhakikisha una formalize complaints mbalimbali kisheria ili kuwepo na traceable records hata kama court ruling kwa wakati husika itakuwa unfavourable. there's always a chance such a ruling being overturned at a higher level at some point afterwards...

please don't call me naive...lol!
Mahakama zipi mkuu?!. Hizi zinazoogopa kugonganisha mihimili!
 
Unamzungumzia Magufuli huyu huyu tunayemjua au kuna mwingine,unasema ajishushe? naona ni kama unaongelea kuupiga mwezi na manati
 
Kwa hiyo anatakiwa Rais Magufuli alihutubie Taifa na kuwahakikishia watanzania kuwa uchaguzi ujao wa serikali za mitaa utakuwa huru na haki na atubu kwa watanzania kuwa yale maneno na matendo yake aliyokuwa anayatoa alikuwa amekosea na ni uvunjifu wa Katiba wa waziwazi kabisa

ntakuja jamani.
 
Back
Top Bottom