Komeo Lachuma
JF-Expert Member
- Oct 31, 2014
- 5,321
- 11,410
Wanasiasa kwa asilimia kubwa wengi wao wataenda motoni ikiwa una imani ya motoni na mbinguni.
Hawa huenda makanisani na misikitini kwa unafiki mkubwa sana wakitaka kuombewa na kubarikiwa ilhali ndani wamejawa uovu mkubwa wa kutisha.
Miaka yote wanasiasa wanasema wanapigania wanyonge. Wanyonge wapi? Wanyonge wanabaki kuwa wa kunyongwa miaka yote. Wananchi maskini wanaouliwa na wanasiasa kwa sababu mbalimbali ni wengi kuliko wanaouawa kwa malaria na magonjwa mengine.
Ni wanasiasa hawa hutoa amri ndugu zetu wateswe, wafungwe, wadhuriwe, wapotezwe na kupatwa na madhila mbalimbali. Ni hawa hawa na kesho na keshokutwa utawakuta nyumba za ibada wakimtaja Mungu. Ni dhahiri Mungu wao ni shetani.
Hawa huenda makanisani na misikitini kwa unafiki mkubwa sana wakitaka kuombewa na kubarikiwa ilhali ndani wamejawa uovu mkubwa wa kutisha.
Miaka yote wanasiasa wanasema wanapigania wanyonge. Wanyonge wapi? Wanyonge wanabaki kuwa wa kunyongwa miaka yote. Wananchi maskini wanaouliwa na wanasiasa kwa sababu mbalimbali ni wengi kuliko wanaouawa kwa malaria na magonjwa mengine.
Ni wanasiasa hawa hutoa amri ndugu zetu wateswe, wafungwe, wadhuriwe, wapotezwe na kupatwa na madhila mbalimbali. Ni hawa hawa na kesho na keshokutwa utawakuta nyumba za ibada wakimtaja Mungu. Ni dhahiri Mungu wao ni shetani.