Ni rahisi kutumia cheo na madaraka kuzima ndoto za wengine, ndoto yako itazimwa pia

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
May 18, 2019
762
6,980
Wapo watu wamejitwalia mamlaka za kuwafanya walio chini yao kama wanyama. Mtu anapigwa na dola Hadharani then dola inasema alikua mgonjwa na anayetamka hayo yupo mbele ya TV na hakuna anakemea.

Tunadhulumu watu haki ya ajira na hakuna wa kutuambia kwamba Taifa ni letu sote. Hakuna anayewakumbusha viongozi kwamba mishahara inalipwa na waajiri ambao ni wananchi.

Tunalazimisha watu watusikilize ila tunasahau kwamba hata wao wana upeo mkubwa kuliko sisi na tunachowazidi ni mamlaka tu.

Waliotangulia kuongoza walitupotosha kwa kisingizio cha uzalendo na ulinzi wetu, wanaotutawala pia wanatufundisha uzalendo bila kujua kwamba uzalendo haufundishwi. Wapo walioitwa wazalendo leo hii ni watuhumowa, ni suala la wakati.

Tusikilizane, tusimamie Hali, tuwaadhibu wanaokwamisha ndoto zetu
 
Bado najiuliza kosa la yule daktari anaetakiwa kukamatwa kwa amri ya Rais bado sijalijua, ndio maana mfalme Suleiman alimuomba Mungu ampe hekima, haya madaraka bila hekima unageuka adui kwa unaowaongoza bila kujua.

Tuendelee kumuombea kwa Mungu bila kuchoka apewe hekima angalau nusu ya kijiko cha chai.
 
Kuna watu waliaajiriwa kama walim

Lkn baada ya kuona ajira hiyo haiondoi ktk ukwamo wa maishaz wameamua kuachaa.

Wanafanya mambo yao, na Mkopo wanaulipa kama kawaida.

Et leo hii, anatokea mmojaz kwa mamlaka yake na kisingizio cha uzalendo, anawataka watu waendelee kubakia palepale walipo bila kujalisha hatima za maisha yao.

Ni wangapi wako nyuma ya Huyo Daktar, wakimtegemea ,ndugu rafiki jamaa?

Et kwakua ulsomeshwa kwa mkopo wenye Riba ya kishenzi, Basi uwe mzalendo wakutumika bila kunufaika.

NCHI HII CHIN YA UTAWALA WAHUYU MPUUZI,WOTE TUTAISHIA KUA MASIKIN.
 
Kauli ya Rais leo akiwa Tabora kuhusu Daktari alieondoka Hospitali ya serikali na kuhamia Hospitali ya private imeniacha na maswali mengi sana,

1) Kauli ya Rais kwamba Daktari yule akamatwe kisa mkopo.

Je, kama hakuchukua mkopo na alisoma kwa pesa zake mwenyewe? Hana haki ya kuhama kutafuta maslahi kwenye ajira? Na hata kama alichukua mkopo, huko alipo kama anakatwa hela kwenye mshahara wake ili alipe?

2) Kauli ya Rais kwamba hio Hospitali ya private aliohamia huyo daktari inyang'anywe leseni.

Hospital hio inakosa gani kama walitoa nafasi za ajira, na huyo Daktari akafanya application ya kuomba kazi? Kuifungia hio hospital kutapoteza ajira ngapi? Kuifungia hio hospital kutapoteza mapato ya kodi n.k ngapi? Kuifungia hio hospital kutapoteza maisha ya raia wangapi wanaotibiwa?

KWANINI Rais asingetoa kauli ya kutatua tatizo la madaktari kuhama kutoka public hospital kwenda private hospital (Kuwaongezea mshahara madaktari wa public hospital ili wasihame kwenda private).
 
Magufuli anafahamu kuwa tangu enzi za Nyerere kuna madaktari wa Tanzania wanakwenda Botswana, Lesotho na Afrika ya Kusini na wanapata ajira na mishahara minono sana.
ANA AKILI SANA ---- Mfumo wa maamuzi kutisha. Uwezo wa mishahara na maslahi bora hana, unacho fanya ni kutengeneza mazingira ambayo wenye kutaka kuhama hospitali za umma wapate taabu kufikia maamuzi, na hospitali binafsi zisite kuchukua Madaktari kutoka serikalini..
 
Bado najiuliza kosa la yule daktari anaetakiwa kukamatwa kwa amri ya Rais bado sijalijua, ndio maana mfalme Suleiman alimuomba Mungu ampe hekima, haya madaraka bila hekima unageuka adui kwa unaowaongoza bila kujua.

Tuendelee kumuombea kwa Mungu bila kuchoka apewe hekima angalau nusu ya kijiko cha chai.
Siombei chizi mimi. Over and out.
 
Wapo watu wamejitwalia mamlaka za kuwafanya walio chini yao kama wanyama. Mtu anapigwa na dola Hadharani then dola inasema alikua mgonjwa na anayetamka hayo yupo mbele ya TV na hakuna anakemea....
IMG_20210130_123255.jpg
 
Bado najiuliza kosa la yule daktari anaetakiwa kukamatwa kwa amri ya Rais bado sijalijua, ndio maana mfalme Suleiman alimuomba Mungu ampe hekima, haya madaraka bila hekima unageuka adui kwa unaowaongoza bila kujua.

Tuendelee kumuombea kwa Mungu bila kuchoka apewe hekima angalau nusu ya kijiko cha chai.
Huyu anaomba Mungu ampe madaraja na wananchi wake waishi kama MASHETANI
 
Back
Top Bottom