Sky Eclat
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 57,597
- 215,272
Rafiki yangu kipenzi amefiwa na aunty yake. Gharama za kumsafisha marehemu mpaka kijijini alikozaliwa zilikuwa kubwa na familia haijiwezi sana. Huyu rafiki yangu alikwenda msibani na aliuliza michango iliyopatikana aliambiwa imepungua milioni 2 kukodi gari la kupelekea msiba kijijini.
Huyu rafiki alijitahidi na kupata milioni tatu. Aliwakabidhi akiwaambia hiyo moja isaidie kuendeshea msiba.
Alinieleza kuwa hii pesa na mwenyewe aliikopa lakini haijalishi mradi tatizo limepata usuluhishi. Alinieleza marehemu alikuwa jirani yao wakiwa wadogo. Alifiwa na mumewe muda mrefu na maisha yake siku za mwisho hayakuwa mazuri sana. Alikuja mjini kuishi na mdogo wake mpaka mauti yanamkuta.
Alinieleza jinsi marehemu alivyokuwa mkarinu wakiwa wadogo. Kuna siku alitoka boarding school kufika nyumbani mama yake amekwenda kwenye msiba kijijini kwao. Marehemu alimwambia awe anakwenda kula nyumbani kwake mpaka mama yake akirudi. Anasema aliona aibu, muda ukipopita yule mama alimfungia chakula na kipande cha mkate. Anasema alifanya hivyo kwa wiki nzima mpaka mama yake anarudi. Alimpa mkate wa kifungua kinywa kwa kesho asubuhi na chakula cha moto cha kula jioni.
Kwa kipindi chote yule mama akiwa kwa mdogo wake, weekend rafiki yangu huyu aliwapelekea kitweo na kila Christmas alimnunulia vitenge na khanga za sikukuu.
Yule mama hakujua kuwa mwanafunzi aliyempa chakula atakuja kumfaa sana mbele ya safari.
Huyu rafiki alijitahidi na kupata milioni tatu. Aliwakabidhi akiwaambia hiyo moja isaidie kuendeshea msiba.
Alinieleza kuwa hii pesa na mwenyewe aliikopa lakini haijalishi mradi tatizo limepata usuluhishi. Alinieleza marehemu alikuwa jirani yao wakiwa wadogo. Alifiwa na mumewe muda mrefu na maisha yake siku za mwisho hayakuwa mazuri sana. Alikuja mjini kuishi na mdogo wake mpaka mauti yanamkuta.
Alinieleza jinsi marehemu alivyokuwa mkarinu wakiwa wadogo. Kuna siku alitoka boarding school kufika nyumbani mama yake amekwenda kwenye msiba kijijini kwao. Marehemu alimwambia awe anakwenda kula nyumbani kwake mpaka mama yake akirudi. Anasema aliona aibu, muda ukipopita yule mama alimfungia chakula na kipande cha mkate. Anasema alifanya hivyo kwa wiki nzima mpaka mama yake anarudi. Alimpa mkate wa kifungua kinywa kwa kesho asubuhi na chakula cha moto cha kula jioni.
Kwa kipindi chote yule mama akiwa kwa mdogo wake, weekend rafiki yangu huyu aliwapelekea kitweo na kila Christmas alimnunulia vitenge na khanga za sikukuu.
Yule mama hakujua kuwa mwanafunzi aliyempa chakula atakuja kumfaa sana mbele ya safari.