Ni rahisi kamba kupenya kwenye tundu la sindano kuliko tajiri kuingia mbinguni

renamaizo

JF-Expert Member
Oct 17, 2014
2,118
3,003
Habari wadau leo tudiscuss hii kauli

Nadhani kuna ushahidi wa kutosha sasa kwamba kwenye ule mstari camel hakuwa ngamia bali ni kamba na viongozi wamekuwa wabishi kutengua io kauli wakihofia kuonekana vilaza, wamekazania eti ni rahisi ngamia kupenya kwenye tundu la si ndano kuliko tajiri kuingia mbinguni, by the way msiwashangae hapa wanatetea ugali wao. Tuje kwenye mada

Hapo kuna statement mbili
A= Kamba kupenya kwenye tundu la sindano

B=Tajiri kuuona ufalme wa mbinguni

Kwa lugha nyepesi au mathematically

Statement A is easy than B

A<B

Tukubaliane hapa statement A is easy km kamba na sindano vinawiana

Kwahiyo kwa lugha nyepesi ni rahisi sana kwa tajiri kuuona ufalme wa mbinguni
 
Kila Utajiri anaukafili Nyuma yake

Ndo maana huwezi kumkuta mtu mwenye kufata NJIA ZA MUNGU na sheria zake akawa nimwenyepesa nyingi

Sababu anajua utamsahau tu

So hizo AB sizani kama kunaukweli
 
Kamba inayotajwa hapo sio kamba hizi za kawaida, Bali hiyo "camel" ni kamba zile kubwa sana nene za kusokotwa zilizotumika hasa kufungia majahazi (dhow) bandarini,
 
Alikuwa ngamia mnyama, si kamba. Sindano lilikuwa lango dogo kwenye lango kubwa (eye of of a needle). Miji ya zamani, hususan Mashariki ya Kati, ilikuwa inazungukwa na ukuta na kuwa na lango moja kubwa la kutokea na kuingilia, kama ilivyo sasa nyumba zina kuta na milango ya kuingilia na kutokea (gates).

Lango kubwa likifungwa jioni, liliachwa wazi lango dodo (eye of a needle) ambalo ngamia alipita kwa taabu huku akiwa na mizigo mgongoni. Ililazimika apigishwe magoti, atue mzigo ndipo aingizwe ndani kwa shida sana. Mathayo 19:24, Marko 10:25 na Luka 18:25
Kila Utajili anaukafili Nyuma yake....
 
Kamba inayotajwa hapo sio kamba hizi za kawaida, Bali hiyo "camel" ni kamba zile kubwa sana nene za kusokotwa zilizotumika hasa kufungia majahazi (dhow) bandarini,
Siping hilo ni sawa lakini pia sindano iliotajwa hapo si hizi za kushonea nguo, ni zile kubwa zinazofungwa kwenye nanga za meli au bandari

Ndio maana nikasema ni rahisi kamba kupenya kwenye tundu la sindano kama zinawiana
 
Alikuwa ngamia mnyama, si kamba. Sindano lilikuwa lango dogo kwenye lango kubwa (eye of of a needle). Miji ya zamani, hususan Mashariki ya Kati, ilikuwa inazungukwa na ukuta na kuwa na lango moja kubwa la kutokea na kuingilia, kama ilivyo sasa nyumba zina kuta na milango ya kuingilia na kutokea (gates)..
Jamaa unatetea ugali
 
Hivi kuna mchawi kama tajili??? Au mwizi kama tajili anavyowanyonya wanyonge??

We unadhani kwanini Yesu alimwambia Yule tajili awagawie malizake zote maskini kisha amfate??
Ndugu usisikilize sana stpr za vijiwen piga kazi

Ni bora hata huyo tajiri hv kuna mwizi kama serikali biashara ufanye ww kod achukue yy ya kaisar mpen kaisar na ya Mungu mpen Mungu
 
Siping hilo ni sawa lkn pia sindano iliotajwa hapo si hz za kushonea nguo ni zile kubwa zinazofungwa kwenye nanga za meli au bandar

Ndio maana nikasema ni rahis kamba kupenya kwenye tundu la sindano km zinawiana
Ni kweli mkuu, Uko sahihi,
 
Mithali 30 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
⁷ Mambo haya mawili nimekuomba; Usininyime [matatu]


⁸ Uniondolee ubatili na uongo; Usinipe umaskini wala utajiri; Unilishe chakula kilicho kadiri yangu.
⁹ Nisije nikashiba nikakukana, Nikasema, Bwana ni nani? Wala nisiwe maskini sana nikaiba, Na kulitaja bure jina la Mungu wangu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom