Ni njia zipi za kukuza GPA kama ikitokea umemaliza Chuo na GPA ndogo

sychellis

Senior Member
Oct 16, 2018
132
107
Wakuu naomba mwenye ujuzi anijuze njia zipi unaweza kutumia kukuza GPA kama ukimaliza na GPA ndogo. na pia nataka nijue ukimaliza chuo na GPA chini ya 3 unaweza kupata kazi
 
Hakuna njia ya kukuza GPA mkuu. Labda kama uko mwaka wa pili hivi unaweza kupambana mwaka wa tatu ukapata A nyingi na kuiinua lakini kama umeshamaliza chuo/shule sidhani kama kuna lolote unaweza kufanya kubadilisha GPA yako.

Labda kama una pesa za kutosha unaweza kutafuta mtu wa IT mroho anayefanya kazi huko kwenye ofisi inayohusika na matokeo akaingia kwenye system akakubadilishia matokeo na kukupandishia GPA unayotaka. Ila napo mtakamatwa tu.

Umeondoka na GPA ya ngapi na unataka uikuze ifikie ngapi?

Kazi nyingi zinatolewa kwa kujuana hapa Bongo hata kama una GPA mbovu kama una connections kazi unapata tu...
 
Hakuna njia ya kukuza GPA mkuu. Labda kama uko mwaka wa pili hivi unaweza kupambana mwaka wa tatu ukapata A nyingi na kuiinua lakini kama umeshamaliza chuo/shule sidhani kama kuna lolote unaweza kufanya kubadilisha GPA yako.

Umeondoka na GPA ya ngapi na unataka uikuze ifikie ngapi?

Kazi nyingi zinatolewa kwa kujuana hapa Bongo hata kama una GPA mbovu kama una connections kazi unapata tu...
Thread closed
 
Mkuu huo mdaa wa kuanza kufikiria kupandisha GPA ni bora upambanie maisha kufanikiwa kivingine bongo hii hata kama GPA ni nzuri na huna connection ni kupoteza mdaa wengine vyeti vipo kabatini mdaa sana tunafanya kazi ambazo hata hatukusomea na maisha yanaendelea vyema
 
jamaa inaweza kuwa bonge la idea hii wizara ya elimu ikaichukua na kuifanyia kazi kwa ajili ya kuwawezesha wenye GPA ndogo
ila kiongozi itakua amepasuka sana kichwa aiseeee mpaka kuwaza kupandisha GPA wakati umemaliza chuo hahahaaaa
 
jamaa inaweza kuwa bonge la idea hii wizara ya elimu ikaichukua na kuifanyia kazi kwa ajili ya kuwawezesha wenye GPA ndogo
ila kiongozi itakua amepasuka sana kichwa aiseeee mpaka kuwaza kupandisha GPA wakati umemaliza chuo hahahaaaa
yes wanatakiwa wafanyie kazi ili swala mkuu. unajua unavyoanza chuo pale kuna mambo mengi unakutana nayo mwisho wa siku yanasababisha unapata GPA ndogo
 
yes wanatakiwa wafanyie kazi ili swala mkuu. unajua unavyoanza chuo pale kuna mambo mengi unakutana nayo mwisho wa siku yanasababisha unapata GPA ndogo
kweli jomba chuoni mambo mengi unashtuka chuo kimeisha umebahatisha kumaliza unaki gpa 2.0001:p:p:p:p
unabahatika tena kuitwa kwenye interview wanataka angalau uwe na 2.5 hapo sasa ndo kazi inaanza na kuanza kuwaza kama kijana wetu
 
Bro gpa isiwe kigezo cha wew kukata tamaa maisha ya chuo yana vikwazo vingi sana sometymz ukiwa na damu mbaya dhid ya malecturer lazma uzingue tu ila jarbu kuomba kazi ukiitwa kwny interview uwa wanaangalia sana personality yako,,kama umegraduate wote tunajua unajua vitu ila personality yako ukoje??la pili jifunze sana kuhusu taaluma yako sasa ujijengee theoretical experience hii nayo itakujenga nna jamaa angu tulimaliza chuo na gpa ndogo sana 2.8 ila sasa hv yy yupo TBS hapo anakula maisha katokea kwao huko kijijin mwanza huko ila jamaa akiwa anakuelekeza kitu yupo competent balaa na ndo maana ma prof walikuwa wanampiga vita ana good personality ana kila kitu mkuu

Jifunze
 
Bro gpa isiwe kigezo cha wew kukata tamaa maisha ya chuo yana vikwazo vingi sana sometymz ukiwa na damu mbaya dhid ya malecturer lazma uzingue tu ila jarbu kuomba kazi ukiitwa kwny interview uwa wanaangalia sana personality yako,,kama umegraduate wote tunajua unajua vitu ila personality yako ukoje??la pili jifunze sana kuhusu taaluma yako sasa ujijengee theoretical experience hii nayo itakujenga nna jamaa angu tulimaliza chuo na gpa ndogo sana 2.8 ila sasa hv yy yupo TBS hapo anakula maisha katokea kwao huko kijijin mwanza huko ila jamaa akiwa anakuelekeza kitu yupo competent balaa na ndo maana ma prof walikuwa wanampiga vita ana good personality ana kila kitu mkuu

Jifunze
asante sana mkuu. ubarikwe sana
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom