Ni nini Utamaduni wa Mtanzania?

Gamba la Nyoka

JF-Expert Member
May 1, 2007
7,022
9,285
Siku nyingi nimekuwa nikisikia kauli kadha wa kadha, mathalani "mavazi haya ni kinyume cha maadili ya mtanzania", au kitendo alichokifanya juma cha ni "kinyume cha utamaduni wa Mtanzania". lakini sijapata kusikia kauli ya "wizi wa pesa ya umma ni kinyume cha Utamaduni wa mtanzania", au kusaini mikataba mibovu ni "kinyume cha utamaduni wa mtanzania" sasa mimi najiuliza je utamaduni wetu kama tunao ni upi?. je sisi watanzania values zetu ni zipi?. kama tunazo hizo values je Tunazikuza(kuziongeza) kadri muda unavypita au bado tunaendeleza stutus quo?.
je wakati wa mkoloni tulikuwa na values zipi na miaka 47 baada ya uhuru tunazo zipi?.

mimi ninadhani values za jamii ni kioo ambacho maendeleo yoyote tunayoyataka na kuyatafuta kwa udi na uvumba lazima ya reflect, kama hatuna values za maana ni vipi tutaendelea?
mjadala uko wazi
 
Kwa kinachote kilichowahi kufikiwa ili kujua true value za Mtanzania...jibu lilikuja moja... Ni UTU!

Nafikiri kazi kubwa iko kwenye kutafsiri maana ya utu!

Lakini wataalamu wa "elimu ya utu" dhidi ya "elimu ya akili" wanadai kuwa kila binaadamu alizaliwa na thamani inayoitwa UTU na utu unaweza kukuwa (To grow) au kufifia mtu anavyoendelea kuutumia, kuishi na umri kuongezeka. Lakini ukweli ni kuwa ingawa kila mtu anazaliwa na UTU ni wachache wanaulinda, kuukuza, na kuupenda hata kufa nao. Ni Wachache wanakufa wakiwa na UTU. Wengi wanakufa wanyama au karibu na hapo.

Tumbili anaweza kuuliza utu ni nini, lakini sio mtu. Mwanadamu ataulizaje asili yake? Tumbili hakuumbwa kuwa na utu, hivyo anaweza kuushangaa, kuulizia na kutaka kuujua. Mtu anayeuliza maana ya UTU ina maana amesha upoteza..yaani amesha upoteza Utanzania.

Mtanzania ni mtu mwenye utu!

Utu ni character au zaidi unaweza kuwa ni Utamaduni!

Asiye na utu ..ameupoteza Utanzania.

Ni kweli kuna wakati Kiwango cha UTU WA TAIFA LA TANZANIA kilikuwa juu!Hakijawahi kutokea afrika.

Utu Kwenye UONGOZI

Utu kwenye Familia.

Utu kwenye kilimo.

utu kwenye elimu

Utu kwenye mavazi

Utu kwnye muziki

Utu kwenye vyakula

Utu kwenye Biashara

Utu kwenye siasa ya nchi

Utu kwenye mifumo ya kiuchumi ya taifa..azimio la arusha? etc

Utu kwenye mahusiano na nchi nyingine

Utu kwenye kuweka mikataba muhimu ya Taifa

Utu ndani ya bunge na wabunge wenyewe!

Utu kwenye sehemu za kazi..(Walikuwa hata na msemo .. KAZI NDIO KIPIMO CHA UTU)

Utu kwenye muungano kati ya Tanganyika na Zanziber

Utu kwenye baraza la Mawaziri

Utu kwenye chaguzi mbalimbali za kitaifa.

Utu kwnye kuwajali wananchi wote kwa pamoja..bila kuwepo kwa matabaka.

Utu kwenye VIONGOZI WASTAAFU WA NGAZI ZA JUU KITAIFA

Utu kwenye kila kitu ilikuwa ndio utamaduni wa Mtanzania. Na Alama za kitaifa zilidhihirisha hivyo. Kauli mbiu mbalimbali zilidhibitisha hivyo..etc

Kujibu swali kuwa UTAMADUNI HUU WA UTU/UTANZANIA unadevelope au ume kwama....Kasi ya kudidimia kwa Utanzania kama utu ni kubwa na inatisha.

Maendeleo bila Utu..? wapi yalishawahi kuonekana hayo? Siasa na uchumi kuwa mikononi mwa viongozi wasio na utu/mafisadi...iyatawezekana vipi?

Kiogozi asiye Mtanzania/asiye na utu anaweza kufanya unyama na kuudhihirisha zadi ya tumbili.

Anaweza kudiriki kuweka saini upande wa kuliangamiza Taifa....badala ya kuweka saini pale pa Kulinda na kutetea Taifa na Maendeleo ya wanachi wake.

Kiongozi asiye na Utu/Fisadi anaweza kuuza Migodi yote ya madili mali ya Taifa kwa robo kilo ya almasi.

Utanzania Ni Utu na Utu umetoweka Tanzania karibu kwenye kila nyanja.

Ndio Maana viongozi wengi waliopo kwenye uongozi wanakufa/watakufa bila UTU! Wanakufa na watakufa wamepoteza asili yao ya kibinaadamu na ya kitanzania.

Swali ..Walizaliwa na UTU Wameupotezea wapi? Ni sahihi kufa kama Mnyama au bila kuwa na heshima ya kiutu?

Ni ulize Swali..Watanzania na Viongozi waliopo IKULU..wanajua siri ya NEMBO YA SEREKALI..kwanini ina alama ya Mwenge wa UHURU? Wanajua hii ni alama ya nini? Wajiulize wanakalia viti na kupeperusha bendera ya serekaliya tanzania ..wanahakika wanajua wanapeperusha na kukalia nini? OLE WAO!!!

Wanajeshi wote..wakague mavazi yao..wanijibu kwanini alama ya Mwenge wa UHURU iko kwenye kila nembo ya mwanajeshi wa nchi hii?

Kama wanajua jibu sawa... huo ndio ya Utanzania... Na utanzania Hausalitiwi na msaliti akabaki salama..haijawahi kutokea...Waulize wasomi wazito wa elimu ya UTU.

Ni nani huyo aliitagulia hii nchi ..na kuijenga katika misingi ya kiutu na akaiwekea alma chungu nzima za kiutu kwa ajiliya vizazi vya kiutu vijavyo?

NCHI HII NI NINI NA INATOKA WAPI NA INKWENDA WAPI::::::

Mkuu nawakilisha mada!!!!

Mungu Ibariki Tanzania!!!!
 
Siku nyingi nimekuwa nikisikia kauli kadha wa kadha, mathalani "mavazi haya ni kinyume cha maadili ya mtanzania", au kitendo alichokifanya juma cha ni "kinyume cha utamaduni wa Mtanzania". lakini sijapata kusikia kauli ya "wizi wa pesa ya umma ni kinyume cha Utamaduni wa mtanzania", au kusaini mikataba mibovu ni "kinyume cha utamaduni wa mtanzania" sasa mimi najiuliza je utamaduni wetu kama tunao ni upi?. je sisi watanzania values zetu ni zipi?. kama tunazo hizo values je Tunazikuza(kuziongeza) kadri muda unavypita au bado tunaendeleza stutus quo?.
je wakati wa mkoloni tulikuwa na values zipi na miaka 47 baada ya uhuru tunazo zipi?.

mimi ninadhani values za jamii ni kioo ambacho maendeleo yoyote tunayoyataka na kuyatafuta kwa udi na uvumba lazima ya reflect, kama hatuna values za maana ni vipi tutaendelea?
mjadala uko wazi

Kabla ya yote toa tafadhali kwanza maana sanifu (au "definitions" kwa Kiingereza) za dhana za "utamaduni" na "Utanzania"/"Mtanzania" kama zinavyoeleweka katika lugha ya Kiswahili.
 
Tunapozungumzia utamaduni wa Tanzania ni muhimu tukumbuke kuwa Tanzania ina miaka 44 na siyo 47 kama mwandishi alivyoandika.

Kuanzia nchi ilipozaliwa hatujawa na utamaduni mmoja kama Taifa ila tuna tamaduni tofauti katika jamii mbalimbali ndani ya taifa moja.

Utamaduni wa kutia mikataba yenye hasara kwa taifa ni kitu ambacho tumekirithi toka kwa mababu zetu.wao ndio walianzisha kutia mikataba iliyotufanya tuwe watumwa. Hivi sasa waandishi wa historia wameamua kuiita mikataba hiyo ni ya kilaghai, katika jitihada za kuwatupia lawama wageni walionufaika na mikataba hiyo huku machief waliokumbatia mikataba hiyo wakipata easy ride. Historia inalaani walionunua watumwa huku ikiwapa easy ride machief waliouza watumwa!

Sijui kizazi kijacho kikiandika historia ya mikataba inayotiwa saini sasa hivi wataiitaje!

Ni muhimu kwa kizazi chetu kutambua kuwa sio kila tamaduni iliyotekelezwa na mababu zetu inafaa, na tuchague tamaduni zenye manufaa.
 
wat about the fact that mtu ukipata ajali kituchakwanza kinachotokea ni watu kukuibia hela, simu na kingine chochote wanachoweza kuchukua alafu ndio uisaidiwe... Wanakijiji wengine have been known to rob even funeral processions..... sasa huu ndio utanzania.. Tanzania is a creation ya wazungu... including over 130 cultures... sasa there are some things which overlap and maybe that is what we can call "utamaduni wakitanzania"
 
Back
Top Bottom