Jumakidogo
R I P
- Jul 16, 2009
- 1,851
- 417
Nimekuwa nikisoma biblia na kukutana na neno Mungu likiandikwa ama kwa kuanza na herufi kubwa au herufi ndogo. Nimekuwa nikijiuliza kwa nini neno hili huandikwa hivyo. Yaani unaweza kukuta limeandikwa 'Mungu' katikati ya sentensi kwa kuanza na herufi kubwa au unaweza kukuta pia limeandikwa 'mungu' katikati ya sentensi kwa kuanza na herufi ndogo. Hii imetumika hivi ikiwa na maana gani? Au hii ninayotumia imechapwa ikiwa na makosa ya kibinadamu? Pia kuna neno 'Bwana' na 'bwana' Nadhani wengi wetu tunajua vizuri kuandika katika lugha yetu ya kiswahili. Lakini hili limenipa utata kidogo. Angalizo; sitarajii ubishi na ushabiki wa kidini katika hili. Nimeuliza tu kwa ufupi nategemea majibu kutoka kwa wajuaji na hasa wanaoijua biblia ipasavyo.