Ni nini tofauti kati ya mtoza ushuru asiye mwaminifu na jambazi mwizi wa pikipiki?

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,633
697,782
Case study ya Mfanyabiashara Khamis Ntunzwe... Mtu aliyepitia madhila mengi mabaya na ya kuhuzunisha sana kisa tu aligoma kutoa hongo ya milioni 2 kwa watoza ushuru

Watoza ushuru hata misahafu inawatambua.. Ni wachafu ni wadhambi, si watu wa haki ama haki zao zina makengeza.. Ni watu katili na waliokosa utu...

Watoza ushuru wana utatu wao.. Utatu wao huu ni mtakatifu kama ule wa wakristo.. Utatu wao ni haramu kwa ajili ya kukamilisha upigaji?
1. Mtoza ushuru
2. Askari polisi
3. Dalali
Ogopa sana hiyo chemistry combination ya huo utatu.. Uki temper nao.. Umekwisha...

Nitamcheka na kumdhihaki yeyote atakayesimama kifua mbele ya kadamnasi na kujitapa kuwa Tanzania ni taifa linalosimamia haki na kuzigatia utawala wa sheria pamoja na kuheshimu haki za binadamu.. Wakati kuna madudu ya kutisha kwenye kesi moja tu kama hii ya Ntunzwe ukiacha ile ya yule kijana wa Moshi aliyedhulumiwa gari yake... Kesi zote mbili zinaihusu mamlaka yetu ya mapato na watendaji wake...

Juzi tumetoka kumzika kijana dereva wa boda. Alinyongwa na kupokonywa pikipiki yake isiyozidi thamani ya milioni 3.. Kwa hesabu za haraka wauaji watauza kwa milioni moja na kugawana laki 5 kila mmoja.. Ntunzwe kapoteza dada yake kwa kugoma kutoa hongo ya milioni 2.. Yani kama hao maofisa watoza ushuru wanne wangefanikiwa kupata hicho kiasi pengine wangegawana laki 5 kila mmoja

Hawa wana tofauti gani na wauaji wa boda boda!? Tofauti yao ni
Elimu
Mavazi
Dhamana yao kwenye jamii
Kipato
Ajira

Lakini linapokuja suala la pesa za haramu hawana tofauti kabisa... Wote ni wauaji wakubwa

Ntunzwe kajitoa mhanga.. Madhila yamekuwa mengi mpaka kaamua liwale naliwe... Kakoswakoswa kuhitimishwa uhai.. Je ni wangapi wamesalimika kama yeye baada ya kuingia kwenye mikono inukayo damu ya mumiani?

Walimwaga ugali, sasa yeye kamwaga kitoweo... Habari iko full episode YouTube.. The soonest itanaswa na wambea wa dunia BBC, DW nk.. Uozo na uvundo wa Mamlaka yetu ya mapato inayojivunia kukidhi viwango vya ISO vitaanikwa mchana kweupee.. Watendaji wake majangili wezi na wachumia tumbo... Kwa majina dunia itawafahamu..

Ogopa sana mtu anayejiamini, aliyeumizwa sana na mwishoni kukata tamaa.. Muogope sana.. Ntunzwe kafanya kilichowashinda wengi... Lakini ni baada ya kikomo cha uvumilivu kumfika pomoni...

Sasa kila kitu hadharani... Tutasimama na raia mmoja aitwaye Ntunzwe? Na serikali yote iabike kwa kushindwa na seven leaver.. Ama tutayavaa mabomu na kunyorosha rula ili ili dhana ya uwajibikaji ichukue nafasi yake na kila mmoja kubeba mzigo wake?

Ya kwamba Mamlaka ya mapato kwa adhabu tofauti tofauti iwawajibishe watendaji wake wajuu kabisa, wa kati na wa chini kabisa wasiopungua 15?

Ya kwamba jeshi la polisi liwawajibishe askari wake na viongozi wao waliokalia jalada la uchunguzi kwa miaka mitatu bila Maendeleo yoyote?

Ya kwamba chama cha wafanyabiashara Tanzania kimwajibishe Katibu wake kwa kutaka KUJARIBU kufanya patano haramu.. Hapa kukiwa na wafanyabiashara wakihusishwa na mmoja kutajwa kwa jina kabisa?

Ya kwamba huyu dalali Yono naye aachwe tu? Kesi hii ni mfano mmoja kati ya maelfu ya kesi wanazokumbana nazo wafanyabiashara Tanzania.. Na wengi huishia kukata tamaa kutokana na formalities nyingi na kutishwa.... Ntunzwe kapiga PABAYA mno.... Na kabamiza hasa.. Ana rundo la USHAHIDI wa nyaraka mpaka na sauti zilizorekodiwa...

Macho na masikio yote sasa ni Mamlaka za juu za nchi.... Je utatumika uzi kunyoosha mstari ama itatumika rula? Ntunzwe anastahili pongezi, pole na hongera... Hata akikoma kuwa leo kila kitu keshaweka hadharani....

Good morning Tanganyika!




Jr
 
Case study ya Mfanyabiashara Khamis Ntunzwe... Mtu aliyepitia madhila mengi mabaya na ya kuhuzunisha sana kisa tu aligoma kutoa hongo ya milioni 2 kwa watoza ushuru

Watoza ushuru hata misahafu inawatambua.. Ni wachafu ni wadhambi, si watu wa haki ama haki zao zina makengeza.. Ni watu katili na waliokosa utu...
Watoza ushuru wana utatu wao.. Utatu wao huu ni mtakatifu kama ule wa wakristo.. Utatu wao ni haramu kwa ajili ya kukamilisha upigaji?
1. Mtoza ushuru
2. Askari polisi
3. Dalali
Ogopa sana hiyo chemistry combination ya huo utatu.. Uki temper nao.. Umekwisha...

Nitamcheka na kumdhihaki yeyote atakayesimama kifua mbele ya kadamnasi na kujitapa kuwa Tanzania ni taifa linalosimamia haki na kuzigatia utawala wa sheria pamoja na kuheshimu haki za binadamu.. Wakati kuna madudu ya kutisha kwenye kesi moja tu kama hii ya Ntunzwe ukiacha ile ya yule kijana wa Moshi aliyedhulumiwa gari yake... Kesi zote mbili zinaihusu mamlaka yetu ya mapato na watendaji wake...

Juzi tumetoka kumzika kijana dereva wa boda. Alinyongwa na kupokonywa pikipiki yake isiyozidi thamani ya milioni 3.. Kwa hesabu za haraka wauaji watauza kwa milioni moja na kugawana laki 5 kila mmoja.. Ntunzwe kapoteza dada yake kwa kugoma kutoa hongo ya milioni 2.. Yani kama hao maofisa watoza ushuru wanne wangefanikiwa kupata hicho kiasi pengine wangegawana laki 5 kila mmoja

Hawa wana tofauti gani na wauaji wa boda boda!? Tofauti yao ni
Elimu
Mavazi
Dhamana yao kwenye jamii
Kipato
Ajira
Lakini linapokuja suala la pesa za haramu hawana tofauti kabisa... Wote ni wauaji wakubwa

Ntunzwe kajitoa mhanga.. Madhila yamekuwa mengi mpaka kaamua liwale naliwe... Kakoswakoswa kuhitimishwa uhai.. Je ni wangapi wamesalimika kama yeye baada ya kuingia kwenye mikono inukayo damu ya mumiani?
Walimwaga ugali, sasa yeye kamwaga kitoweo... Habari iko full episode YouTube.. The soonest itanaswa na wambea wa dunia BBC, DW nk.. Uozo na uvundo wa Mamlaka yetu ya mapato inayojivunia kukidhi viwango vya ISO vitaanikwa mchana kweupee.. Watendaji wake majangili wezi na wachumia tumbo... Kwa majina dunia itawafahamu..

Ogopa sana mtu anayejiamini, aliyeumizwa sana na mwishoni kukata tamaa.. Muogope sana.. Ntunzwe kafanya kilichowashinda wengi... Lakini ni baada ya kikomo cha uvumilivu kumfika pomoni...

Sasa kila kitu hadharani... Tutasimama na raia mmoja aitwaye Ntunzwe? Na serikali yote iabike kwa kushindwa na seven leaver.. Ama tutayavaa mabomu na kunyorosha rula ili ili dhana ya uwajibikaji ichukue nafasi yake na kila mmoja kubeba mzigo wake?
Ya kwamba Mamlaka ya mapato kwa adhabu tofauti tofauti iwawajibishe watendaji wake wajuu kabisa, wa kati na wa chini kabisa wasiopungua 15?
Ya kwamba jeshi la polisi liwawajibishe askari wake na viongozi wao waliokalia jalada la uchunguzi kwa miaka mitatu bila Maendeleo yoyote?
Ya kwamba chama cha wafanyabiashara Tanzania kimwajibishe Katibu wake kwa kutaka KUJARIBU kufanya patano haramu.. Hapa kukiwa na wafanyabiashara wakihusishwa na mmoja kutajwa kwa jina kabisa?
Ya kwamba huyu dalali Yono naye aachwe tuu?
Kesi hii ni mfano mmoja kati ya maelfu ya kesi wanazokumbana nazo wafanyabiashara Tanzania.. Na wengi huishia kukata tamaa kutokana na formalities nyingi na kutishwa.... Ntunzwe kapiga PABAYA mno.... Na kabamiza hasa.. Ana rundo la USHAHIDI wa nyaraka mpaka na sauti zilizorekodiwa...

Macho na masikio yote sasa ni Mamlaka za juu za nchi.... Je utatumika uzi kunyoosha mstari ama itatumika rula? Ntunzwe anastahili pongezi, pole na hongera... Hata akikoma kuwa leo kila kitu keshaweka hadharani....

Good morning Tanganyika!




Jr

Hii sjaisikia! Ngoja niifuatilie what is all about!
 
.
hqdefault.jpeg


Jr
 
Ukisikia kumwaga mboga ndio hii.Ntuzwe kaongea ukweli na uhalisia toka moyoni, yupo makini, mbali ya imani yake thabiti, ana baraka za kutosha toka kwao." Nitakufa siku aliyonipangia Mungu na haki yangu nitakuwa nimeipata tayari..."

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ila pona yake ni 2020 maamuzi ya wengi yakiwa tofauti na sasa... La sivyo watamtafuta kila kona...
Ukisikia kumwaga mboga ndio hii.Ntuzwe kaongea ukweli na uhalisia toka moyoni, yupo makini, mbali ya imani yake thabiti, ana baraka za kutosha toka kwao." Nitakufa siku aliyonipangia Mungu na haki yangu nitakuwa nimeipata tayari..."

Sent using Jamii Forums mobile app

Jr
 
Nilikamatiwa gari yangu 2014 Toyota Hiace na madalali wa majembe kwa kesi ambayo tayari nilikuwa nimesharipoti TRA investigation unit. Hawa ndugu wakataka milioni 3 ili waniachie lakini wakashuka mpaka million moja... Sikuwapa chochote kwakuwa kwanza sikuwa na hiyo pesa pili hata kama ningekuwa nayo nikawapa bado nisingetatua tatizo na tatu tayari nilishatoa taarifa sehemu husika
Baada ya ishu kushindikana tukaelekea TRA tukisindikizwa na polisi.. Kufika TRA makao makuu maofisa walionikamata wakaingia ndani wakaongea na kiongozi wao kwa dakika kadhaa...
Nilikuja kujua baadae kuwa kumbe waliripoti tofauti wakisema niligoma kukamatwa mpaka wakaitwa polisi... Niandikapo haya leo hii gari iko pale W9 inaendelea kuoza licha ya mapambano ya miaka 3

Jr
 
Naomba nimshauri Mzalendo Ramadhani Ntuzwe, awe makini pale anapouza bidhaa dukani kwake ahakikishe anatoa risiti hata kama mteja kanunua bidhaa ya sh 50.00 kwani TRA inaelekea wapo "Rada" ili waweze kumfungilia kesi ya kutakatisha fedha.

Kwasababu kama alisema Mh Rais Magufuli akitekelezeki walipaswa kumjibu sio kwa kimya hicho, na ikiwezekana hata Waheshimiwa Wabunge walipeleke hilo suala Bungeni katika maswali ya papo kwa hapo kwa Mh Waziri Mkuu kila Alhamisi.
 
Hawa wezi wa bodaboda katili sana. Badala tu wachukue pikipiki wasepe wanaua kikatili. Kuna mijitu kwenye jamii sijui imezaliwaje hayana utu kabisa.
 
Back
Top Bottom