KIBURUDISHO
JF-Expert Member
- Mar 28, 2011
- 1,002
- 274
WanaJF wenzangu napata shida kidogo juu ya tafsri ya hili neno maombolezo.Hivi inaingia akilini taifa kusitisha shughuli zake muhimu kama Bunge na kutangaza kuwa taifa linaomboleza juu ya msiba mkubwa uliowakumba wenzetu wa Zanzibar hali wenzetu wa vyombo vya redio na televisheni wakiwa na vipindi vya kawaida na nyimbo zinazopigwa sii za maomboleza!.Ilitakiwa vipindi vingine viendelee kama kawaida ila vile vipindi vya muziki viwe vinapigwa nyimbo za maombolezo kwa siku hizo zilizopangwa za kuomboleza tukiwa tunawafariji ndugu jamaa na marafiki waliofikwa na msiba huo mkubwa.Nawapongeza Capital redio wamekuwa wakifanya hivyo toka asubuhi.