Ni nini maana ya huku kususia chaguzi ya vyama vya siasa hususani CHADEMA?

RNA

JF-Expert Member
Mar 27, 2013
1,584
2,683
Habari JF

Kumekuwa na Tabia ya kususia Chaguzi kwa baadhi ya Vyama hususani CHADEMA, kwa namna navyoelewa kususa haijawahi kuwa suluhu ya tatizo labda kipindi cha utoto tu napo wazazi walikuwa wanaweza kukupotezea tu.

Hivyo nikawaza kwa kina sana nikapata tafsiri zifuatazo zinaweza kuwa sahihi kuhusu hii susa susa.

1. Ni njia mojawapo ya kufitini baadhi ya viongozi wasiingie kwenye vinyang'anyiro na kuwa viongozi.

2. Wanahofia hakuna tume huru hivyo hakuna haja ya kushiriki uchaguzi huku washindi wanajulikana.

3. Viongozi wa vyama wananunuliwa ili uchaguzi uwe rahisi kama inavyofanywa na baadhi ya viongozi kujitoa.

4. Wanajua hawatashinda hivyo wanaona hakuna haja kushiriki.

Hivi nini maana ya hizi susia huku hatuoni suluhisho lolote linatafutwa? Na je, kuna mwanachama anayehitaji kugombea uongozi atabaki CHADEMA huku hajui kama watashiriki uchaguzi au la?
 
Hawako tayari kushiriki dhambi kwa namna nyingine ni tume kutokuwa huru ndo maana sehemu yoyote walipowahi kushinda Chadema na vyama vingine huwa wanatumia nguvu ya umma kutangazwa bila nguvu hiyo ndo inakotokea hiyo dhambi.
 
Watu wanalamba Asali huko wanachama mnazuiwa kujiexpose kwa wananchi
 
Cha kushangaza ni kwamba vyama vingine Kama CUF na ACT wameshiriki Kama vyama pinzani kitendo cha CDM kukataa imekuwa mjadala mkubwa tukisema humu ndani kwamba CDM ndo chama Cha upinzani ndani ya nchi hii muwe mnaelewa enyi mataga wa chama Cha fisiemu mtu Kama Pasco Mayalla kada mtiifu wa CCM kila uchwao kuandika ushauri kuhusu cdm
 
Uchaguzi wa CCM, tume ya CCM, polisi wa CCM, walimu wengi ni wahesabu kura za CCM sa wengine washiriki ili iweje.
 
Back
Top Bottom