Ni nini kinafanya Kenya (KRA) kukusanya mapato zaidi ya Tanzania (TRA)?

Mapank

JF-Expert Member
Mar 8, 2011
4,074
5,911
Kama kichwa cha uzi kinavyojieleza "Ni nini kinafanya Kenya kukusanya mapato zaidi ya Tanzania?" Kwa muda nimekuwa mfuatiliaji wa Budget wa nchi za Jumuiya ya AFRIKA MASHARIKI. Katika ufuatiliaji huo nimekutana na maswali ambayo nimekuwa siyapatii majibu. Kwa kutumia nchi mbili KENYA na TANZANIA.

Nchi hizi mbili zimekuwa washindani wakubwa kiuchumi katika ukanda wa AFRIKA MASHARIKI. Maajabu ni wenzetu KENYA hawajabahatika kuwa na rasimali nyingi kama wenzao TANZANIA. Ila kupitia mamlaka yao ya mapato KRA wamekuwa wakikusanya mapato mengi kuliko majirani zao TANZANIA kupitia mamlaka yao ya mapato TRA. Mfano ni mwezi wa December 2020 TRA walijipongeza kwa kukusanya TZS 2.088 trilioni na wenzao KRA walikusanya TZS 3.4 trilioni katika kipindi cha mwezi Desemba, 2020.

Kwa upande wa idadi ya watu TANZANIA inakadiriwa kuwa na watu million 60 wakati KENYA wanakadiriwa kufikia million 53. Ni nini kinasababisha huo utofauti wa mapato?

1611000422003.png


1611000463779.png
 
Kenya ni Capitalist Country na Ina strong industrial base tangia zamani Iyo ndo sababu ya wao kutuzidi.
Tuna dhahabu na Tanzanite ambayo Kenya hawana. Hivyo viwanda vya Kenya vinauza wapi bidhaa zao ambazo hatuzijui?
 
Tuna dhahabu na Tanzanite ambayo Kenya hawana. Hivyo viwanda vya Kenya vinauza wapi bidhaa zao ambazo hatuzijui?
mzee unasema unafuatilia budget za hizi nchi mbili unashindwa jua vitu basic hivyo..makampuni mengi ya bidhaa za chakula yapo kenya toka zamani...ndo maana Mzee baba magufuri anapush ili tuweze industrialize zaidi nchi.
 
mzee unasema unafuatilia budget za hizi nchi mbili unashindwa jua vitu basic hivyo..makampuni mengi ya bidhaa za chakula yapo kenya toka zamani...ndo maana Mzee baba magufuri anapush ili tuweze industrialize zaidi nchi.
Tunakwama wapi miaka yote awamu zote, kufanya industrialization au kuzidi hata Kenya?
 
Kenya ni Capitalist Country na Ina strong industrial base tangia zamani Iyo ndo sababu ya wao kutuzidi.
Hata mlima kilimanjaro tangu zamani upo ks, na matanzanite, na gesi pia.
Mfumo wa tra sio rafiki.
 
Nakumbuka bidhaa nyingi sana zilikuwa zinakuja kwa njia halali miaka ya 70 ambavyo vinatengenezwa Kenya
Kama waliweza kutangaza biashara zao miaka hiyo na kuleta mpaka cinema kwa kuhamasisha na kuuza bidhaa zao hapo ndio wanapotuzidi
Sisi bado tuko mbali sana kulinganisha na wao
Huwa napingana nao kwa mengi ila kwa biashara na ukusanyaji wako mbali
 
Nakumbuka bidhaa nyingi sana zilikuwa zinakuja kwa njia halali miaka ya 70 ambavyo vinatengenezwa Kenya
Kama waliweza kutangaza biashara zao miaka hiyo na kuleta mpaka cinema kwa kuhamasisha na kuuza bidhaa zao hapo ndio wanapotuzidi
Sisi bado tuko mbali sana kulinganisha na wao
Huwa napingana nao kwa mengi ila kwa biashara na ukusanyaji wako mbali
Unaweza kuwa na industry bado market ikawa ni changamoto, population ya Kenya haikidhi idadi ya viwanda mnavyodai vipo Kenya. Soko la bidhaa za Kenya liko wapi au kwenye nchi zipi? Kwa maana hata sasa kwenye ma supermarket ya kwetu nchini bidhaa za Kenya sio nyingi kama za Tanzania. Je soko la bidhaa za Kenya, Tanzania hairuhusiwi kupeleka bidhaa?
 
Back
Top Bottom