Ni nini kimeifanya CCM kushindwa kabisa kufanya lolote juu ya Mipango Miji?

Lord denning

JF-Expert Member
Jun 3, 2015
13,221
26,031
Amani iwe nanyi wadau!!

Leo naomba niulize hili swali kwenu wanajamvi maana kwa kweli mie nimetafakari hadi nimeshindwa kupata majibu.

kuna shida gani kwa Chama cha Mapinduzi juu ya Mipango miji??? Ukitembea Tanzania nzima, karibu asilimia 85 ya makazi ya watanzania ni makazi holela. Tatizo ni nini? Kama Tatizo ni kukosekana kwa pesa au wataalamu wa kupima ardhi na Makazi ndo tuseme,

1. Je CCM wameshindwa kabisa hata kusema hakuna ruhusa ya mtu kujenga mahali huku akizuia njia au barabara na kuziamulu serikali za mitaa kumvunjia mtu yeyote aliyejenga mahali kwa kuziba njia na barabara?

2. Je serikali ya CCM wameshindwa kabisa hata kuziamuru serikali za mitaa na vijiji kusimamia suala la watu wanaouza ardhi zao kuhakikisha kuwa wanapopima viwanja au mashamba wahakikishe wanaweka barabara zenye ukubwa wa kutosha kuwezesha hata gari mbili kubwa kupishana kwa kuzingatia endapo majanga yatatokea?

3. Je serikali kupitia wizara ya ardhi na Makazi wameshindwa kutoa hata mwongozo juu ya jinsi gani ujenzi wa mitaani uwe?? Na kusambaza mwongozo huo kwa serikali za mitaa kwa usimamizi?

Hii nchi kusema kweli imefika hatua inasikitisha. Ukimsikiliza waziri wa Ardhi ni kama ameshushwa leo Tanzania na hajui kuwa hili ndo Tatizo kuu linaloikabili Tanzania ya leo.

Ukitembea mitaani kuanzia Dar, Mwanza, Mbeya , Arusha , Iringa , Pwani, Zanzibar , Tabora, Kigoma na maeneo mengi ya Tanzania unaweza kusema nchi hii nzima haina watu wenye akili au hata waliotembea na kufika duniani huko kuona kukoje? Watu wamejijengea hovyo tu na wanazidi kujijengea hovyo tu. Unapita Ada estate kumepimwa ila mtaa wa nyuma kinondoni shamba kuna sehemu hata pikipiki haipiti kwa kujengwa vibaya.

Mbaya zaidi kwenye hili imefika hatua mpaka kinatokea kizazi cha watu ambao wao wanaona ufahali kujisifu kuishi maeneo ya hovyo( wanaita uswahilini au uswazi).

Hivi leo niwaulize CCM na makada wao mliopo humu kina GUSSIE Crimea YEHODAYA Barbarosa , HAMY-D Ritz chagu wa malunde Bia yetu Mudawote Kitila Mkumbo Mwigulu Nchemba Team JPM johnthebaptist Tatizo ni nini??? Imekuwaje kwa miaka yote hii mmekuwa madarakani na mmeshindwa kufanya jambo dogo tu kama hili?
 
Mipango miji duniani kote hutegemea uwezo wa kipato wa jamiii husika

Usiite ujenzi holela kuna maenro ya wenye nazo mipango miji iko vizuri kaishi huko kama uwezo sababu huko nyumba kujenga ramani tu yaweza kugharimu hata milioni kumi sababu nyumba unatakiwa kujenga kwa specific specification na kunakuwa na maeneo ya supermarkets sio magenge au duka la mang au mpemba l na kunakuwa na hotels sio mama nitilie

Ukikomaa copy and paste sio rahisi

Nchi ili duniani ya dunia ya tatu isiyp na makazi holela?taja hata moja tu
 
Madalali wa ukawa ndio wanaharibu miji wanauza viwanja kama maandazi
Amani iwe nanyi wadau!!

Leo naomba niulize hili swali kwenu wanajamvi maana kwa kweli mie nimetafakari hadi nimeshindwa kupata majibu...
 
CHADEMA wenyewe wamepanga makao yao makuu kwenye makazi holela midimbwi kibao nyumba utafikiri Choo cha city
 
Mipango miji duniani kote hutegemea uwezo wa kipato wa jamiii husika...
Kwa iyo kwa akili zenu hamuoni kuwa ni muhimu wananchi wote, wenye Nacho na wasio nacho wakae sehemu zilizojengwa vizuri kwa ustaarabu na mpangilio wa kuacha njia kubwa ya kufika kwa kila mtu?

Unasema kila sehemu duniani kuna makazi holela, una uhakika au unaropoka tu? Umefika Israel?? Umefika German? Umefika UK??

Kwa akili zako hizo basi ni sahihi kuna walakini sana kwenye bongo za wana Ccm?
 
Madalali wa ukawa ndio wanaharibu miji wanauza viwanja kama maandazi
Unatia huruma. We kila sehemu kuleta ushabiki maandazi wako??? Wenyeviti wa serikali za mitaa wanaosimamia hovyo uuzwaji wa maeneo nao ni wa ukawa??
 
Watakuambia Chadema ndiyo wamewachelewesha.

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
Inasikitisha kwa kweli. Kama miji mikubwa saivi ni shida, na tuendako huko ndo itakuwa balaaa. Mfano Dar maeneo mapya yote ukienda chanika, kinyerezi, mpiji majohe, makabe, mapwepande, kigamboni watu wanajijengea hovyo tu na wala hakuna anayejali.

Dodoma ndo usiseme, kuna maeneo watu wansjijengea tu na itakuwa Kama manzese na Tandale au mwananyamala . Ni upuuzi mtupu
 
Mipango miji itakujaje wakati viongozi wa ufipa wanajenga kwenye vyanzo vya maji.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom