Elections 2010 Ni nini hatma ya uswahiba wa JK na Rostam Aziz...?

PhD

JF-Expert Member
Jul 15, 2009
4,599
3,673
kama inavyofahamika kwa wengi, Ndugu Hussein Bashe ni kijana wa karibu sana na Rostam Aziz yeye ndio msimamizi wa miradi mikubwa pale Caspian na kwingineko kwa niaba ya RA, izingatiwe pia RA ndiye aliyefadhili kampeni za Bashe Nzega kwa muda mrefu.

nachojaribu kuhoji ni hatua gani Rostam ataanza kuchukua dhidi ya JK baada ya kijana wake kuondolewa kwenye uchaguzi kwa kashfa za kutokuwa raia, lakini pia suala la uraia limewahi kujitokeza kwa Rostam mwenyewe je kwa sasa hawezi kuanza kujikinga kwa namna yoyote ile ili na yeye asije ambiwa sio raia.

na je kama Rostam akianza kujikinga na kuchukua tahadhari ikizingatiwa kuwa maamuzi ya kamati kuu juu ya Bashe hayakumpendeza kabisa, huu utakuwa ndo mwisho wa uswahiba na JK, Je rostam akikosana na JK Nchi itakuwa salama?, TAFAKARI
 
Hakuna Tafakuri hapa, RA itabidi anyamaze kwani Bashe alitofautiana na RIZ mtoto wa mwenye kaya
 
Je rostam akikosana na JK Nchi itakuwa salama?, TAFAKARI

Wakati mwingine nadhani tunajaribu kufanya vichuguu kuwa milima Kilimanjaro. Rostam ni nani hasa hata aweze kufanya nchi ishindwe kuwa salama kwa yeye kukosana na Kikwete? Kinachotokea na kilichotokea ni "DHAMBI" ya dhuluma Rostam na genge lake waliyowatenda kwa wananchi wenye dhiki na wasio na hatia, imeanza kuwatafuna, itaendelea kuwatafuna na wataendelea kutafunana wenyewe kwa wenyewe na wananchi wataendelea kubaki salama wasalimini!
 
kama inavyofahamika kwa wengi, Ndugu Hussein Bashe ni kijana wa karibu sana na Rostam Aziz yeye ndio msimamizi wa miradi mikubwa pale Caspian na kwingineko kwa niaba ya RA, izingatiwe pia RA ndiye aliyefadhili kampeni za Bashe Nzega kwa muda mrefu.

nachojaribu kuhoji ni hatua gani Rostam ataanza kuchukua dhidi ya JK baada ya kijana wake kuondolewa kwenye uchaguzi kwa kashfa za kutokuwa raia, lakini pia suala la uraia limewahi kujitokeza kwa Rostam mwenyewe je kwa sasa hawezi kuanza kujikinga kwa namna yoyote ile ili na yeye asije ambiwa sio raia.

na je kama Rostam akianza kujikinga na kuchukua tahadhari ikizingatiwa kuwa maamuzi ya kamati kuu juu ya Bashe hayakumpendeza kabisa, huu utakuwa ndo mwisho wa uswahiba na JK, Je rostam akikosana na JK Nchi itakuwa salama?, TAFAKARI

Hatima ya uswahiba huu ni kuipeleka nchi hii pabaya. Hadi sasa hii triumvirate -- JK-RA-EL inaiweke mustakabali wa nchi hii katika hali ya wasiwasi mkubwa na Watz wenye akili timamu wanaona kwamba matatizo mengi ya kisiasa ya sasa hivi yanatokana na uswahiba wa utatu huu -- kwani matatizo hayo yanachangiowa na ufisadi ambao unaelekezwa katika uswahiba huu. Utatu huu umekuwa unahbusishwa na kashfa kubwa kubwa za ufisadi -- kuanzia tamko la Mwembe Yanga -- EPA, Richmond na mengineyo -- either kwa ujumla wao au kwa mmoja mmoja.

Lakini hakuna kitu kinachoonyesha kuhusika kwa kikundi hiki na ufisadi kuliko mapungufu makubwa ya namna JK (kama kiongozi wa muhimili wa utawala) alivyoshughulikia kashfa mbili kubwa za ufisadi: Richmond -- kukwepa kutimiza kutimiza mapendekezo ya Kamati ya Bunge, na Kagoda -- kushindwa kumfikisha mhusika mahakamani kama vile wengine -- kwa sababu tu mhusika wa Kagoda ni RA.
 
Wakati mwingine nadhani tunajaribu kufanya vichuguu kuwa milima Kilimanjaro. Rostam ni nani hasa hata aweze kufanya nchi ishindwe kuwa salama kwa yeye kukosana na Kikwete? Kinachotokea na kilichotokea ni "DHAMBI" ya dhuluma Rostam na genge lake waliyowatenda kwa wananchi wenye dhiki na wasio na hatia, imeanza kuwatafuna, itaendelea kuwatafuna na wataendelea kutafunana wenyewe kwa wenyewe na wananchi wataendelea kubaki salama wasalimini!

ndugu BORA MAISHA hapo kwenye Bold ni vema nikaeleweka sahihi, uliza yeyote yule anayeingia kwenye vikao vya juu vya CCM na Baraza la Mawaziri ndio utaelewa nguvu ya Rostam katika utawala wa Nchi hii, kwa taarifa yako hata viongozi wa usalama wa taifa wanamuogopa bingwa huyo wa kimafia, na kama haitoshi angalia anavyonyenyekewa na wazee wa CCM kama Msekwa na Kingunge, hitimisho RA ni hatari kwa usalama wa Taifa letu ana siri kubwa ya kuingia madarakani JK hivyo akicharuka nahisi Nchi itapata mshtuko.
 
wale wale tu. Huo urafiki hautaisha ndugu yangu. wanabebana wote. RA halipi kodi. na JK anapewa pesa za Campaign na RA.
 
Back
Top Bottom