Ni nini hasa itapelekea mwanaume uliyenaye akupe heshima ya ndoa?

Wakuu kwema

Moja kwa moja kwenye mada.

Ikiwa kumpa ngono haimfanyi mwanaume kukuoa, wala kumzalia mwana pia haimfanyi mwanaume kukuoa je, nini hasa itapelekea mwanaume ulie nae akupe heshima ya ndoa?

Maana wengine wanabadili hadi dini ili kumridhisha mwanaume lakini bado haolewi. Hata ukijitahidi kuwa mwenye heshima au tabia njema utakuta anaenda oa kwingine. Au ndoa ni fate?

Karibuni kwa ushauri

am better here
Tabia njema, unyenyekevu kwa mmeo, utii,jua nafasi yako kama mwanamke, binafsi mke wangu wakati tunatongozona sikuwahi kuwaza nikishapata ningedumu nae hata week 2 lakini nilibadili gia njiani nikaamua kuoa kabisa baada ya kuona ana hivyo vyote niendelee kuangaika natafuta nini???
 
Unadhani huko kufeel utayari wa kutaka kuoa unatoka wapi?? Usiongee mambo usiyoyafahamu! Hakuna Mwanaume mjinga ambaye atakutana na mwanamke sahihi akiwa katika umri na wakati sahihi alafu aendeleze uplayer! Hata kama hakuwa na plan hiyo ila akikutana na mwanamke anayemheshimu na kujiheshimu mwenye hofu ya Mungu Mwaminifu anayemsaidia katika harakati za maisha ni vichocheo tosha kumfanya mwanaume yeyote aanze kuja kwenye line.
Ruge huyo alikuwa na Zamaradi...mpaka kaolewa ndo analia hadi makamasi wakati alikuwa kila siku anasema atapeleka barua atapeleka barua. Kwamba alikuwa hajafika umri sahihi? Alikuwa Zama alikuwa hajiheshimu na kumheshimu?

Wanaume wana utayari wao usiotokana na mwanamke kabisa.
 
Back
Top Bottom