Ni ngumu kufurahia mapenzi ikiwa una hofu au visasi vya kuumizwa

Ncha Kali

JF-Expert Member
Sep 19, 2019
14,361
26,661
Ndugu zangu!

Tujilazimishe tu kusamehe na kuachilia. Sio kitu rahisi, lakini faida zake ni kwa maslahi ya kesho yako. Kwenye mapenzi unakutana na mtu ambaye humjui, unajifariji eti utamfahamu kupitia maelezo yake! Hii ni kujitekenya pakubwa.

Wengi wana yao mioyoni na hutoweza kuyajua, wenye majuto na hofu ya kuumizwa wapo. Wenye visasi vya kulipiza wapo, wale waliokata tamaa na kuona 'itakavyokuwa' tu nao ni wengi tu.

Kwa namna hizi na nyingine, iwe ni wewe au yeye. Ukiingia kwenye mahusiano mapya na kumbukizi mbovu au machale machale huwezi kufaidi mema walahi.

Tujifunze kusamehe na kujitakasa, waliokuumiza ni wengine sio huyu mwingine. Anza upya, na ufurahie maisha.

Ncha Kali.
 
Tujifunze kusamehe na kujitakasa, waliokuumiza ni wengine sio huyu mwingine. Anza upya, na ufurahie maisha.
Barikiwa sana

IMG_20210619_195307.jpg
 
Shanny baada ya kuachana na mpenzi wake aliye interim kwa sasa akanikubalia mimi. Nilikuwa namtafuta kwa mwaka hivi na attention yote nampa, wakati huo nina short term contracts na wadada wengine. Tatizo likaja pale nimeanza kuwa nae analeta kumbukumbu za ex wake.

Mara ya mwisho naonana nae alitoa kauli eti hawezi kunipenda kama alivyomoenda yeye. Akatoa sababu eti alimshauri huyo MD mambo mengi akafanikiwa alafu kamuacha yakiwa yameanza kutiki. Hebu niishie hapa kueleza
 
Tiba sahihi ktk mapenzi ni kupata mtu wa kufanana (kuendana) naye kisawasawa.

Lkn hata ujitie kusahau vipi kama ukimpata mtibua nyongo lazima ukumbuke yaliyopita.

Sexless kungwi la kitaa
 
Shanny baada ya kuachana na mpenzi wake aliye interim kwa sasa akanikubalia mimi. Nilikuwa namtafuta kwa mwaka hivi na attention yote nampa, wakati huo nina short term contracts na wadada wengine. Tatizo likaja pale nimeanza kuwa nae analeta kumbukumbu za ex wake.

Mara ya mwisho naonana nae alitoa kauli eti hawezi kunipenda kama alivyomoenda yeye. Akatoa sababu eti alimshauri huyo MD mambo mengi akafanikiwa alafu kamuacha yakiwa yameanza kutiki. Hebu niishie hapa kueleza
Usiwaze komaa naye atamsahau akikuzoea, hizo mbwembwe za short run
 
Ni kweli waliokuumiza ni wengine lakin jua kuwa hawatoki sayari nyingine ni hii hii na unatakiwa kujifunza kutokana na makosa machale muhimu sana hase siwezi umizwa kipuuzi mara ya kwanza na njia hiyo niumizwe mara ya pili, Ila sintakaa nihangaike kulipa kisasi kwenye mapenz et kisa nimeumizwa huko na mm nkaumize mtu baada yakugundu amenipenda
 
Ni kweli waliokuumiza ni wengine lakin jua kuwa hawatoki sayari nyingine ni hii hii na unatakiwa kujifunza kutokana na makosa machale muhimu sana hase siwez umizwa kipuuzi mara ya kwanza na njia hiyo niumizwe mara ya pili, Ila sintakaa nihangaike kulipa kisasi kwenye mapenz et kisa nimeumizwa huko na mm nkaumize mtu baada yakugundu amenipenda

Huo sio uungwana classic!
 
Wengi wanakosea sana wanapolazimisha mapenzi, wengine wanapewa ishara zote kuwa hawakubaliki lakini bado wanakuwa ving'ang'anizi
 
Vidada vinavyosoma MD vinajiona kama dunia hii ni yao peke yao
Shanny baada ya kuachana na mpenzi wake aliye interim kwa sasa akanikubalia mimi. Nilikuwa namtafuta kwa mwaka hivi na attention yote nampa, wakati huo nina short term contracts na wadada wengine. Tatizo likaja pale nimeanza kuwa nae analeta kumbukumbu za ex wake.

Mara ya mwisho naonana nae alitoa kauli eti hawezi kunipenda kama alivyomoenda yeye. Akatoa sababu eti alimshauri huyo MD mambo mengi akafanikiwa alafu kamuacha yakiwa yameanza kutiki. Hebu niishie ha
 
Ndugu zangu!

Tujilazimishe tu kusamehe na kuachilia. Sio kitu rahisi, lakini faida zake ni kwa maslahi ya kesho yako.

Kwenye mapenzi unakutana na mtu ambaye humjui, unajifariji eti utamfahamu kupitia maelezo yake! Hii ni kujitekenya pakubwa.

Wengi wana yao mioyoni na hutoweza kuyajua, wenye majuto na hofu ya kuumizwa wapo. Wenye visasi vya kulipiza wapo, wale waliokata tamaa na kuona 'itakavyokuwa' tu nao ni wengi tu.

Kwa namna hizi na nyingine, iwe ni wewe au yeye. Ukiingia kwenye mahusiano mapya na kumbukizi mbovu au machale machale huwezi kufaidi mema walahi.

Tujifunze kusamehe na kujitakasa, waliokuumiza ni wengine sio huyu mwingine. Anza upya, na ufurahie maisha.

Ncha Kali.
UKOKIKI (UKOSEFU WA KINGA KIMAPENZI), hili ndiyo tatizo kubwa Kwa watu wengi , watu walio na kinga za kutosha ktk mapenzi hawawezi kuwa Lia Lia Kwa kuwa kinga imara huwapa nguvu ya kuzuia mfadhaiko unaweza kupatikana kwenye relationship ya KIMAPENZI yeyote

Hawa ni watu ambao hawapati shida ukijifaragua kinywako anakuongezea na mwendo

Ukitaka kifurahia mapenzi uwe na kinga imara

Narudia Kwa wanaume; ukiwa na mwanamke hesabu ni wako unapokuwa naye Tu , ukiachana naye usihesabu . Fanya hivi haitakuja kutokea umejuta
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom