Ni nchi gani yenye mipango miji mibovu zaidi ya Tanzania?

Tomaa Mireni

JF-Expert Member
Sep 8, 2015
2,328
2,283
Nilikua napita pita kwenye Google Earth nimegundua miji mingi Tanzania imekaa hovyo hovyo sana.

Kuna nchi ziko jangwani kabisa lakini wamejenga kwa mpango mzuri. Hata DRC ambayo kuna migogoro kila mara bado kumepangwa vizuri. Tanzania badala ya kujenga miji mipya wanabomoa ya zamani na kujenga nyumba mpya sijui hili limekaaje.

IMG_20210515_175504.jpg


Kwanini kila serikali ya mji isisimamie na kupima maeneo yake? Huenda labda wananchi wanaogopa kwenda kuchukua kibali cha ujenzi sababu ya gharama kwanini serikali isitoe vibali hivyo bure kama ni ujenzi wa nyumba ya kawaida kwa ajili ya makazi?

Kwanini kusiwe na sheria kali kabisa hakuna kujenga sehemu isiyopimwa? Wakati huo huo serikali ipime maeneo mengi ili kuepuka usumbufu wa ujenzi kwa wanunuzi?

Nini kifanyike ili miji inayokuwa sasa ikae kwenye mpango mzuri tofauti na mwanzoni?

Nani wa kulaumiwa kwa mipango mibovu ya miji? Serikali kuu au za manispaa?
 
Inaonekana watendaji wa ardhi wameshamua ku-surrender na kuacha mambo yajiendeshe yenyewe baada ya kuelemewa na upimaji wa ardhi ndani ya nchi hii.

Matatizo ni mengi. Mojawapo ni pale halmashauri kutaka kutengeneza pesa kwa kupima ardhi na kuwauzia viwanja wananchi kwa bei kubwa, hivyo wananchi wanakimbilia maeneo ambayo hayajapimwa.

Suluhisho;

Serikali ipime viwanja bure au kwa bei nafuu ili mwananchi mwenye kipato cha chini amudu kununua.

Vibali vya ujenzi vitolewe kwa bei nafuu na kwa haraka.

Kuna kipindi waziri Lukuvi alisema serikali itakopa hela benki ya Dunia ili kuipima ardhi yote Tanzania hii. Sijui ule mpango uliishia wapi!

Hata huko vijijini inatakiwa kupimwa na kujenga kwa mipango kwa sababu vijiji hivyo ndiyo mijini ya baadae.
 
Ungeweka sasa na aerial photograph ya bongo ili hoja yako iwe na mashiko zaidi.
 
Inaonekana watendaji wa ardhi wameshamua ku-surrender na kuacha mambo yajiendeshe yenyewe baada ya kuelemewa na upimaji wa ardhi ndani ya nchi hii.

Matatizo ni mengi. Mojawapo ni pale halmashauri kutaka kutengeneza pesa kwa kupima ardhi na kuwauzia viwanja wananchi kwa bei kubwa, hivyo wananchi wanakimbilia maeneo ambayo hayajapimwa.

Suluhisho;

Serikali ipime viwanja bure au kwa bei nafuu ili mwananchi mwenye kipato cha chini amudu kununua.

Vibali vya ujenzi vitolewe kwa bei nafuu na kwa haraka.

Kuna kipindi waziri Lukuvi alisema serikali itakopa hela benki ya Dunia ili kuipima ardhi yote Tanzania hii. Sijui ule mpango uliishia wapi!

Hata huko vijijini inatakiwa kupimwa na kujenga kwa mipango kwa sababu vijiji hivyo ndiyo mijini ya baadae.
Asee unastahili kazi pale wizarani,umeongea pointi sana,kweli wengi wanakimbia viwanja vilivyopimwa sababu ya bei
 
Kitengo cha mipango miji kipo tuu kwenye makaratasi but in reality ni sifuri kabisa.
 
Tz ni nchi iliyozoea mambo ovyo ovyo na holela. Ukija na wazo la kufanya vitu kwa mipango na utaratibu wanakushangaa. Angalia Machinga walivyoachwa kufanya biashara maeneo yasiyo rasmi. Angalia Ndugai anavyovunja sheria kwa nguvu! And no one cares!
Wamezoea vibaya sana kias hata serikali ikifanya jambo fulani wanahisi wamepewa haikuwa haki yao
 
Nilikua napita pita kwenye Google Earth nimegundua miji mingi Tanzania imekaa hovyo hovyo sana.

Kuna nchi ziko jangwani kabisa lakini wamejenga kwa mpango mzuri. Hata DRC ambayo kuna migogoro kila mara bado kumepangwa vizuri. Tanzania badala ya kujenga miji mipya wanabomoa ya zamani na kujenga nyumba mpya sijui hili limekaaje.

View attachment 1786133

Kwanini kila serikali ya mji isisimamie na kupima maeneo yake? Huenda labda wananchi wanaogopa kwenda kuchukua kibali cha ujenzi sababu ya gharama kwanini serikali isitoe vibali hivyo bure kama ni ujenzi wa nyumba ya kawaida kwa ajili ya makazi?

Kwanini kusiwe na sheria kali kabisa hakuna kujenga sehemu isiyopimwa? Wakati huo huo serikali ipime maeneo mengi ili kuepuka usumbufu wa ujenzi kwa wanunuzi?

Nini kifanyike ili miji inayokuwa sasa ikae kwenye mpango mzuri tofauti na mwanzoni?

Nani wa kulaumiwa kwa mipango mibovu ya miji? Serikali kuu au za manispaa?
Umasikini kwa kipato unasabisha umasikini wa akili
 
Serikali kuu Ndio tatizo, mipango miji wanafuata amri order kutoka kwa mamlaka za juu, Mfano suala la Machinga kuzagaa barabarani sio kwamba mipango miji hawaoni, wanaona lakini kuwatoa tu hawawezi kwa sababu alietoa amri wakae hapo ni Kiongozi wa ngazi ya juu, hakufuata Sheria.

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom