Luqman mohamedy
JF-Expert Member
- Jul 24, 2016
- 892
- 1,226
Vurugu baina ya wanachama wa CUF mahakama kuu leo hii imethibitisha ya kwamba wanaCUF wanakula nyumba yao ya mikate walioijenga kwa miongo miwili kwa njaa ya masaa tu.
Na kwa kipindi kirefu chama hiki kilionekana kama muhimili usiotikisika kwenye kambi ya upinzani kabla ya kuingia kwa mdudu pesa na tamaa.
Nimekaa nikijiuliza bila kupata jibu ya hoja za pande hizi mbili huku zote zikilalamikia wakubwa wao wameuza chama kwa pande mbili tofauti moja kauzia dola mwingine kauza UKAWA.
Ieleweke hawa jamaa wanapigania jina la CUF walitumie kama daraja la kuvuka kisiasa,jina lililojengwa kitambo la sivyo wangehama.
Ubara na uzenji umeonekana kutawala mijadala ya pande hizi
Mpaka kufikia sasa haieleweki CUF watafanya nini kwenye uchaguzi wa 2020 ikiwa wenyewe wameshindwana.
CUF kimepungua sifa kutoka chama kikuu cha upinzani na kua chama kikuu cha upigani.
Nani kawaloga hawa jamaa??!!
Sent using Jamii Forums mobile app
Na kwa kipindi kirefu chama hiki kilionekana kama muhimili usiotikisika kwenye kambi ya upinzani kabla ya kuingia kwa mdudu pesa na tamaa.
Nimekaa nikijiuliza bila kupata jibu ya hoja za pande hizi mbili huku zote zikilalamikia wakubwa wao wameuza chama kwa pande mbili tofauti moja kauzia dola mwingine kauza UKAWA.
Ieleweke hawa jamaa wanapigania jina la CUF walitumie kama daraja la kuvuka kisiasa,jina lililojengwa kitambo la sivyo wangehama.
Ubara na uzenji umeonekana kutawala mijadala ya pande hizi
Mpaka kufikia sasa haieleweki CUF watafanya nini kwenye uchaguzi wa 2020 ikiwa wenyewe wameshindwana.
CUF kimepungua sifa kutoka chama kikuu cha upinzani na kua chama kikuu cha upigani.
Nani kawaloga hawa jamaa??!!
Sent using Jamii Forums mobile app