Ni nani hasa mmiliki wa Simba Trust?

Abuka

JF-Expert Member
Sep 17, 2013
247
241
Nipende kuwapa mwanga tu mpate japo kujiridhisha na kufuatilia ni nani hasa mmiliki wa Simba Trust.

Wamiliki wa Simba trust Taasisi iliotajwa kubeba nusu ya mgao kwenye pesa za umma zilizoibwa kwenye akaunti ya Escrow sio kwamba ni wamiliki tu, wako na mtandao mkubwa wa either kumiliki au kuwa na hisa katika makampuni yafuatayo.

1: Precision Air:
Hao hao wamiliki wa Simba trust na genge lao wanaonekana kuwa na hisa ndani ya kampuni hii ya ndege.

2: TSN + GSM :
Ndio pia wamiliki wa makampuni yote ikiwemo TSN super market Kwa kununua hisa na kumiliki share ndani ya makampuni hayo.

3: Azania Bank:
Wamewekeza hisa nyingi pia kwenye hii bank ya Azania amabayo ilikua kwa kasi ndani ya utawala wa awamu ya 4

4: GAPCO+ LAKE OIL
Ni wawekezaji pia kwenye suala la mafuta kwa kuwa na hisa au umiliki wa moja kwa moja

5: TULAWAKA GOLD MINE:
Wawekezaji ndani ya mgodi wa Tulawaka walifanikisha kuwafukuza wananchi katika mgodi uo na kujenga uzio .

6: Mgodi wa Tanzanite Arusha :
Pia wamewekeza kwenye mgodi huu baada ya mikataba ya Makaburu kuisha .

7: Ndio wamiliki wa UDA pia ambayo pia ni Kampuni yenye utata wa umiliki wake kwenye hisa zake.

8 : Baadhi ya makampuni ya clearing na forwarding hapo bandarini.

9 : Ndio walishinda zabuni ya ujenzi wa soko la kisasa kule Mwanza (Rock city shopping Mail) kupitia uchochoro wa wachina na kukwapua mamilioni .

10: Ndio wamiliki wa makampuni ya kufanya usafi kwenye halmashauri nyingi nchini karibu kwa asilimia 75% hawa ndio upewa tenda.

Wanahusishwa pia na hisa kwenye kiwanda cha Dangote cha cement kilichojengwa mtwara.

Pia ni wawekezaji kwenye shirika letu la nyuma NHC kama mnakumbuka shirika la Nyumba la taifa limekuwa likikopa pesa kwa ajiri ya kujenga Nyumba hasa miradi ya Dodoma kuna mkono wa hawa jamaa.

Pamoja na kwamba umiliki unabadilika badilika kiasi lakini mtandao ndio ule ule unaomiliki Simba Trust.

Wanacho kifanya ni kuwatumia watu kufanikisha mambo yao hasa watu wenye asili ya Asia .

Hata ukiangalia kwenye list ya pesa za escrow account zilizogawiwa pale Stanibic bank list ya watu hao ilikuwepo .

Nimetoa kwa ufupi kuepuka kutaja majina kwa sababu za kisheria lakini mkifuatilia kwa makini mtagundua ni wakina Nani wapo nyuma ya hii michezo yote inayoendelea...

Hao ndio wanachukua milioni zetu 400 kila siku pale Tanesco.

Wanao zungumzwa hapo nao hawatofautiani na Mzee Wa Vijisenti Kila Mahala wapo! Ukitaja Lugumi wapo
 
Inasemekana ni familia ya mstaafu mmoja. Wengine huku hatujui. Labda ukamuulize mwanaye ambaye ni maarufu atakuwa na majibu.
 
Watanzania tupo anti-investment na anti-rich. Kila mwenye mafanikio popote ataandamwa na kuitwa mwizi.
Mjinga wewe, anti-investment ndiyo nini? Escrow money ilikuwa money laundering, mkiguswa kidogo maanza kusingizia anti-investment! Escrow, stimulus ile ya kikwete walifanya money laundering!
 
Maajabu haya nayaona mm pekeangu au tuko wengi! Huu uzi ni wa Juni 2017 mwaka juzi afu comment ya kwanza kabisa ni ya leo 17/02/2018!!! Aisee!
Hata hivyo big up sana mkuu kwa uzi murua kabisa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Write your reply...mindset za ujamaa na kujitegemea zilishapitwa na wakati,waulizeni venezuela,
 
Write your reply...@interestedobserver,una maana gani unaposema moneylaundry?,au ndo imekuwa fasheni tu sikuhizi kusema moneylaundry?
 
Back
Top Bottom