Ni nani baba wa taifa?

Dalali444

Member
Feb 7, 2010
7
0
Mimi nimekuwa nikijiuliza sana kuhusu hii dhana ya Baba wa Taifa na hasa kwa nchi yetu ya Tanzania. Ninavyofahamu mimi mtu anayepewa heshima ya kuwa Baba wa Taifa ni yule muasisi wa mwanzo ambaye alifanikisha kuzaliwa kwa hilo Taifa lenyewe.Hapa kwetu Tanzania tunaambiwa kuwa Mwalimu Nyerere ndiye Baba wa Taifa (officially).

Mimi nimekuwa nikisita kidogo kukubali kumwita Nyerere Baba.Si kwa utovu wa adabu au ukorofi lakini naona haingii akilini kabisa.Naweza kukubali shingo upande kuwa ni Baba wa Taifa la Tanganyika(ambalo liliundwa baada ya uhuru wa 1961). Nasema shingo upande kwa sababu naelewa kuwa walikuwepo watu waliomtangulia kupigania uhuru wa Tanganyika ambao waliongoza mapambano kabla ya yeye hajatoka kijijini kwao na kuja Dar na baadae kukabidhiwa usukani. Nyerere hakuanzisha na wala hakuwa mwenyekiti wa mwanzo wa TAA.

Kwa upande wa Tanzania mimi nashindwa kunyanyua ulimi wangu kumwita Baba. Kwa kauli zake mwenyewe Nyerere ametamka mara nyingi kuwa alikuwa ni Karume ndiye aliyemfuata Dar-es-Salaam na kumshauri waungane.Hili Nyerere amelisema mara nyingi kila alipokuwa akisakamwa na Wazanzibari kuhusu mashaka ya Muungano. Sasa ikiwa ni Karume aliyekuja kumtaka Nyerere wafunge ndoa na nyerere akakubali, mbona leo tunaambiwa Nyerere ndiye baba?

Kwa mila na desturi zetu za kiafrika ni mume ndiye anayetoka kwenda kuposa mke na si vyenginevyo. Na kwa kauli za Nyerere mwenyewe, ni Karume ndiye aliyetoka kwenda kupeleka posa Dar na kwa bahati posa zikapokelewa na harusi ikafungwa haraka haraka na Taifa la Tanzania likazaliwa.

Kwa mtizamo wangu hapa naona karume ndiye mume (mposaji na muowaji) na mume ndiye kwa mila na desturi zetu huitwa BABA. Nitakubali ikiwa tutaambiwa Nyerere tumwite MAMA wa Taifa.
Dalali
 
Ubaba,umama,ujomba,ushangazi,ukaka n.k Utatusaidia vipi kuwaondoa maadui zetu wakubwa ufisadi na rushwa?Naomba nijuze ewe mtoa hoja.
 
Kwa mila na desturi zetu za kiafrika......

Haya tuendeleze hii ngano yako ya kitoto. Ndoa hiyo ikajaliwa kupata wana wawili wa jinsi tofauti.Kwa mila na desturi zetu za kiafrika, watoto wa kike ndiwo huwa legelege na wa kiume hugangamala. Hivyo Wazanzibari ndio mtoto wa kike na Wabara ni wa kiume. Na tukumbuke kuwa mama na baba hawapo hapa duniani ni sisi tumebaki!
 
Ubaba,umama,ujomba,ushangazi,ukaka n.k Utatusaidia vipi kuwaondoa maadui zetu wakubwa ufisadi na rushwa?Naomba nijuze ewe mtoa hoja.
I second that... Muacheni Nyerere apumzike bwana... :confused:
 
We ni mpemba nini? kuposa na kuposwa kunaingiaje hapa?.

Cha msingi ongelea kuondoa hawa maadui watatu ambao ni Ujinga, Umaskini, Maradhi ambao bado vinawatafuta watanzania hadi karne hii tunayoita eti ya sayansi na technologia.
Kuongelea nani baba nani mama wa taifa hili - haina tija kwa sasa.
 
Mimi nimekuwa nikijiuliza sana kuhusu hii dhana ya Baba wa Taifa na hasa kwa nchi yetu ya Tanzania. Ninavyofahamu mimi mtu anayepewa heshima ya kuwa Baba wa Taifa ni yule muasisi wa mwanzo ambaye alifanikisha kuzaliwa kwa hilo Taifa lenyewe.Hapa kwetu Tanzania tunaambiwa kuwa Mwalimu Nyerere ndiye Baba wa Taifa (officially).

Mimi nimekuwa nikisita kidogo kukubali kumwita Nyerere Baba.Si kwa utovu wa adabu au ukorofi lakini naona haingii akilini kabisa.Naweza kukubali shingo upande kuwa ni Baba wa Taifa la Tanganyika(ambalo liliundwa baada ya uhuru wa 1961). Nasema shingo upande kwa sababu naelewa kuwa walikuwepo watu waliomtangulia kupigania uhuru wa Tanganyika ambao waliongoza mapambano kabla ya yeye hajatoka kijijini kwao na kuja Dar na baadae kukabidhiwa usukani. Nyerere hakuanzisha na wala hakuwa mwenyekiti wa mwanzo wa TAA.

Kwa upande wa Tanzania mimi nashindwa kunyanyua ulimi wangu kumwita Baba. Kwa kauli zake mwenyewe Nyerere ametamka mara nyingi kuwa alikuwa ni Karume ndiye aliyemfuata Dar-es-Salaam na kumshauri waungane.Hili Nyerere amelisema mara nyingi kila alipokuwa akisakamwa na Wazanzibari kuhusu mashaka ya Muungano. Sasa ikiwa ni Karume aliyekuja kumtaka Nyerere wafunge ndoa na nyerere akakubali, mbona leo tunaambiwa Nyerere ndiye baba?

Kwa mila na desturi zetu za kiafrika ni mume ndiye anayetoka kwenda kuposa mke na si vyenginevyo. Na kwa kauli za Nyerere mwenyewe, ni Karume ndiye aliyetoka kwenda kupeleka posa Dar na kwa bahati posa zikapokelewa na harusi ikafungwa haraka haraka na Taifa la Tanzania likazaliwa.

Kwa mtizamo wangu hapa naona karume ndiye mume (mposaji na muowaji) na mume ndiye kwa mila na desturi zetu huitwa BABA. Nitakubali ikiwa tutaambiwa Nyerere tumwite MAMA wa Taifa.
Dalali
Mjomba leo dawa zako kunywa asubuhi naona ulipitilizwa
 
Ebu mjibuni ndugu huyu acheni kuruka ruka au kuwafananisha zanzibar na binti!

Dalali, kuna mambo katika jamii yanayokea tu kutokana na inluence ya huyo mtu katika kila maisha ya Mtanzania. JN ameinfluence maisha ya kila mtu nchi hii, even today more than ten years of his absence we still have his effects. Ni kama bado anaishi , maana kila mtu Nyerere,Nyerere, he was simply a great leader

Ila sijaona sehemu imeandikwa kuwa lazima umuite baba wa taifa ni rais wa kwanza a.k.a baba wa taifa, mchonga,wakatoliki wanataka kumwita mtakatifu etc

so kama hautaki hana shida, ila ataitwa hivyo kwa vizazi vijavyo vyote wakiwemo watoto wako.
 
Jamani mmemuona KIBUNANGO amebadilsha avatar yake!!! Naona ni mmoja wa waanzilishi wa CCJ kwani ameondokana na kijani!! Hongera Kibunango umejikomboa na harufu ya kifisadi!!
 
Mtoa mada ana point inabidi zijibiwe kwa standard za kitaalam za JF, vinginevyo jf itapoteza credibility yake kama majibu ya maswali muhimu yanakuwa kama yaliyojibiwa hapo nyuma, kweli inasikitisha

Wana jf kama hii kweli ni think tank forum inabidi tuumize vichwa na kutoa hoja nzuri zitazo elimisha jamii sio ilimradi kujibu

Naomba tusome mada vizuri na kujibu kwa hoja na sio kijeli kama wafanyavyo wanasiasa wa CCM
 
Nyerere baba wa taifa officially?

Kasema nani? Kwa kifungu gani cha katiba au sheria ipi? Unajua maana ya neno "officially"?
 
We ni mpemba nini? kuposa na kuposwa kunaingiaje hapa?.

Cha msingi ongelea kuondoa hawa maadui watatu ambao ni Ujinga, Umaskini, Maradhi ambao bado vinawatafuta watanzania hadi karne hii tunayoita eti ya sayansi na technologia.
Kuongelea nani baba nani mama wa taifa hili - haina tija kwa sasa.

wewe ni mTANGANYIKA nini!
 
Haya tuendeleze hii ngano yako ya kitoto. Ndoa hiyo ikajaliwa kupata wana wawili wa jinsi tofauti.Kwa mila na desturi zetu za kiafrika, watoto wa kike ndiwo huwa legelege na wa kiume hugangamala. Hivyo Wazanzibari ndio mtoto wa kike na Wabara ni wa kiume. Na tukumbuke kuwa mama na baba hawapo hapa duniani ni sisi tumebaki!


Hii ngano na mie nimeipenda yakhe wacha nichangie kidogo.Baada ya Baba na Mama kufariki waliwaachia watoto mali nyingi, badala ya kuzitunza wakaanza kugombana kila mmoja akidai mali hii ilikuwa ya wote na hii ni ya kwangu baba alinipa. Ugomvi ukakua ukakomaa watoto wakatoana pua wakataka kuachana undugu...
 
..jamani Karume alitoa wazo la kuungana.

..lakini Mwalimu alikuwa ndiye Raisi wa kwanza wa Jamhuri yetu.

..ninavyoelewa mimi Raisi wa Kwanza mara nyingi ndiye anayepewa jina la "Baba wa Taifa."

..pia kama jina "Baba wa Taifa" linawakwaza baadhi yetu basi bora tuachane nalo tu tumie jina "Waasisi" kuwatambulisha viongozi wote waliotoa mchango wao kwa Uhuru wa Tanganyika,Mapinduzi ya Zenj, na Muungano.
 
U could be reasable if u couldn't mention ur incorrect and unreasonable belief inside urself, go and read again 4 ur own knowledge, b4 zanzibar independence, revolution and even b4 the formulation of asp mwalimu was indirectly leading the struggle in zanzibar, he had the idea of uniting the all east africa even b4 1960. Read, read and read, use ur head and not ur stomach!
 
Haya tuendeleze hii ngano yako ya kitoto. Ndoa hiyo ikajaliwa kupata wana wawili wa jinsi tofauti.Kwa mila na desturi zetu za kiafrika, watoto wa kike ndiwo huwa legelege na wa kiume hugangamala. Hivyo Wazanzibari ndio mtoto wa kike na Wabara ni wa kiume. Na tukumbuke kuwa mama na baba hawapo hapa duniani ni sisi tumebaki!
Na wao(wazanzibar) wakiwa kama dada zetu hawatafanya maamuzi yoyote bila kutuomba ushauri cc kaka zao,na endapo tukikataa hakuna watakachobadili,na mara atakapo tokea mume(wazungu)atakayetaka kuoa(kuinunua) cc ndio tutakao chukua posa mara watakapo kamilisha masharti ya posa hiyo!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom