Mallata Jr.
JF-Expert Member
- Feb 24, 2014
- 461
- 392
View attachment 205133
Kulikuwa na duka Kuubwa la Vyakula na Vinywaji katika mji. Panya Wengi waliishi katika duka hilo la vyakula na vinywaji. Chakula kilikuwa ni kingi sana kwa ajili yao. Walikula kila kitu na kuharibu mifuko yote ya vyakula. Waliharibu pia mikate, biskuti na matunda ya duka.
Mwenye duka alishikwa na wasiwasi kweli. Hivyo, yeye alipata wazo "mimi lazima ninunue paka na atakaa humu ndani ya hili duka. Kufanya hivo naweza kuokoa mambo yangu."
Alimnunua Paka mmoja mzuri, mkubwa na kisha kumwacha pale. Paka alikuwa na wakati mzuri wa kuwinda panya na kuwaua. Panya hawakuweza kuzunguka kwa uhuru sasa. Waliogopa kwamba wakati wowote paka ange wakamata na kuwala.
Panya walitaka kufanya kitu fulani. Wakaitisha mkutano na wote wakasema "Ni lazima kujikwamua na paka. Je, kuna mtu ana maoni? mwenyekiti aliuliza.
Panya wote wameketi kimya na kuogopa. panya mmoja mwelevu alisimama na akasema, "paka hatembea kwa upole. Hilo ni tatizo. Kama tunaweza kumfunga kengele kwenye shingo yake, basi mambo yatakuwa mazuri. Tunaweza kujua harakati zake zote ".
"Ndiyo, hilo ni jibu sahihi," walisema panya wote. panya wa miaka mingi alisimama polepole na akauliza, "Ni Nani atakaye Mfunga paka kengele? " Baada ya muda mchache hakukuwa na yeyote wa kujibu swali hili.
Swali:
Sasa tuulizane wasomi nini mafundisho ya hadithi hii ambayo kila mmoja wetu aliichukulia ya watoto wa shule ya msingi yaani kuleeeeeeee tuliko pita zamani.Kwa upande wangu inanifundisha ya kwamba UFUMBUZI MTUPU HAUNA THAMANI. Nini mafundisho yake kwa upande wako?
Kulikuwa na duka Kuubwa la Vyakula na Vinywaji katika mji. Panya Wengi waliishi katika duka hilo la vyakula na vinywaji. Chakula kilikuwa ni kingi sana kwa ajili yao. Walikula kila kitu na kuharibu mifuko yote ya vyakula. Waliharibu pia mikate, biskuti na matunda ya duka.
Mwenye duka alishikwa na wasiwasi kweli. Hivyo, yeye alipata wazo "mimi lazima ninunue paka na atakaa humu ndani ya hili duka. Kufanya hivo naweza kuokoa mambo yangu."
Alimnunua Paka mmoja mzuri, mkubwa na kisha kumwacha pale. Paka alikuwa na wakati mzuri wa kuwinda panya na kuwaua. Panya hawakuweza kuzunguka kwa uhuru sasa. Waliogopa kwamba wakati wowote paka ange wakamata na kuwala.
Panya walitaka kufanya kitu fulani. Wakaitisha mkutano na wote wakasema "Ni lazima kujikwamua na paka. Je, kuna mtu ana maoni? mwenyekiti aliuliza.
Panya wote wameketi kimya na kuogopa. panya mmoja mwelevu alisimama na akasema, "paka hatembea kwa upole. Hilo ni tatizo. Kama tunaweza kumfunga kengele kwenye shingo yake, basi mambo yatakuwa mazuri. Tunaweza kujua harakati zake zote ".
"Ndiyo, hilo ni jibu sahihi," walisema panya wote. panya wa miaka mingi alisimama polepole na akauliza, "Ni Nani atakaye Mfunga paka kengele? " Baada ya muda mchache hakukuwa na yeyote wa kujibu swali hili.
Swali:
Sasa tuulizane wasomi nini mafundisho ya hadithi hii ambayo kila mmoja wetu aliichukulia ya watoto wa shule ya msingi yaani kuleeeeeeee tuliko pita zamani.Kwa upande wangu inanifundisha ya kwamba UFUMBUZI MTUPU HAUNA THAMANI. Nini mafundisho yake kwa upande wako?